Siasa-muziki bado pengo la marehemu Komba halijazibwa sio CCM wenyewe wala sio CHADEMA

Siasa-muziki bado pengo la marehemu Komba halijazibwa sio CCM wenyewe wala sio CHADEMA

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Wakuu Kwema.

Wiki iliyopita nilikuwa kwenye sherehe ya Harusi ambayo maharusi ni wanachama wa CHADEMA na CCM.
MC akaitisha challenge baina ya CCM na CHADEMA kulingana na maharusi.

Waliaanza CHADEMA, ikapigwa nyimbo mbili za CHADEMA. Wala hazikuwa na amshaamsha licha ya wafuasi na wanachama wa chama hiko kujitahidi kuonyesha mapenzi.

Ikaja zamu ya CCM ikapigwa ya Kwanza sijui ya Nani kaiimba, wafuasi na wanachama wa CCM wakatoka Kwa mbwembwe wakijitahidi kuamshaamsha na kufanya waonekane wao ni zaidi ya washindani wao.

Wimbo wa pili ulipigwa wa Marehemu Komba. Doooh! Sio mchezo, Vibe yake haikuwa ya nchi hii. Ukumbi mzima ulilipuka Kwa vigelegele na shangwe kila mmoja akicheza bila kujali ni chama gani. Wimbo wenyewe ni " CCM mbele Kwa mbele"

Kiukweli nyimbo za Marehemu komba zinamsisimko mkubwa mno. Nyimbo za kuomba zinamchango mkubwa katika kukua na kuenea Kwa CCM.

Kwa sasa sioni WA kuziba pengo lake sio Kwa wanasanaa wa CCM wenyewe au Vyama vya upinzani.

Baadhi ya nyimbo za Marehemu Komba ambazo zilikuwa na msisimko na vibe Kwa wafuasi na wasiowafuasi wa Siasa.

1. CCM mbelembele
2. Jogoo limewika chimwaga (sijui Kama napatia
3. Nambari one ni CCM

Wengine mtaendelea kunitajia hapo chini.

Kwenye Siasa-muziki Komba ndiye Legend na ndiye Baba. Hakuna mpaka sasa WA kuziba pengo lake.
Pengine sauti ya kipekee ndio iliyokuwa inambeba mbali na Promo.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Back
Top Bottom