Siasa na sanaa ni mapacha kama mapambio na mahubiri

Siasa na sanaa ni mapacha kama mapambio na mahubiri

Queen Esther

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2012
Posts
2,206
Reaction score
1,464
Leo nimemuona Askofu fulani anasema hawezi kuhubiri mpaka wanakwaya waimbe, pia kikundi cha sifa na kuabudu kiimbe nyimbo za kutosha na nzuri. Pia, muimbishaji yule mwenye uwezo mkubwa afanye huduma hiyo.

Nimejaribu kuangalia siasa za CCM ambapo nyimbo za wasanii zinaimbwa nyingi zikieleza utekelezaji wa Ilani kabla mgombea hajasimama kumwaga sera akionesha tulipotoka, tulipo na tunapoelekea.

Vilevile kwa vyama vingine wanatumia sana mziki wa CD na miondoko mbalimbali kama Reggae nk. Baada ya hapo ndipo mgombea anaongea anachoongea hata kama hana sera.

Nimejaribu kuoanisha matukio haya mawili nikakumbuka hata kwenye maandiko waliobomoa kuta za Yeriko waliwatanguliza wazee wa mapambio mbele! Hongera Rais Magufuli kwani unabomoa ngome za adui zako kupitia sanaa ya uimbaji. Tangu enzi za Capt. John Komba sanaa ya uimbaji imekuwa ni sanaa ya CCM wakati wa matukio yote zikiwemo kampeni, kama kwa Maaskofu, Mitume na Manabii, Wachungaji, Mashekhe na Kaswida nk Hata mchawi anaanza na kuimba kabla ya kuloga au kuagua!!

Queen Esther
 
..Kunatakiwa kuwe na balance nzuri.

..Kwa sasa hivi CCM wamezidisha sanaa, hawafanyi siasa.

..Hiyo yote ni kuficha mapungufu ya Magufuli kwamba hawezi kuzungumza kwa muda mrefu bila kutoa boko.
 
..Kunatakiwa kuwe na balance nzuri.

..Kwa sasa hivi CCM wamezidisha sanaa, hawafanyi siasa.

..Hiyo yote ni kuficha mapungufu ya Magufuli kwamba hawezi kuzungumza kwa muda mrefu bila kutoa boko.
Subiri tarehe 28 Oct ndio utajua wamezidisha au imelipa! Hata kampeni za Mataifa makubwa wasanii tena wale maarufu wanaalikwa!!
 
Malkia Jezibel asiyeyajua maandiko ni mama wa makahaba.
Tunapoimba kanisani, tunamuimbia Mungu mkuu jehova, sifa na utukufu ni kwake, sio kwa mahubiri.
Mnalawitiwa na wachungaji feki wenu kwasababu mnawasifu wao na kuwatukuza wao badala ya Mungu.
 
Subiri tarehe 28 Oct ndio utajua wamezidisha au imelipa! Hata kampeni za Mataifa makubwa wasanii tena wale maarufu wanaalikwa!!

..mahusiano ya mwanasiasa na msanii kwa hapa Tz ni ya bwana na mtwana.

..kwenye mataifa ya wenzetu wasanii wana nguvu za kiuchumi na hawaendeshwi na wanasiasa.

..Ni kweli kuna wasanii, lakini sio kuzidisha kama ilivyo hapa Tanzania.

..huwezi kusikia msanii katunga wimbo maalum kwa ajili ya kampeni za Donald Trump, au Boris Johnson.
 
Malkia Jezibel asiyeyajua maandiko ni mama wa makahaba.
Tunapoimba kanisani, tunamuimbia Mungu mkuu jehova, sifa na utukufu ni kwake, sio kwa mahubiri.
Mnalawitiwa na wachungaji feki wenu kwasababu mnawasifu wao na kuwatukuza wao badala ya Mungu.
Nasikitika kusema kwamba hujamwelewa mleta mada.
 
Malkia Jezibel asiyeyajua maandiko ni mama wa makahaba.
Tunapoimba kanisani, tunamuimbia Mungu mkuu jehova, sifa na utukufu ni kwake, sio kwa mahubiri.
Mnalawitiwa na wachungaji feki wenu kwasababu mnawasifu wao na kuwatukuza wao badala ya Mungu.
Duuu!! Povu kama lote!! Sasa ndio ineandika nini? Nawe unajiita "great thinker?". Unakifahamu kivuli cha halisi?

Queen Esther
 
Kwa hilo sikubaliani, maana ccm haijaanza leo kutumia Sanaa. Wasanii wetu hawawezi kaa, kwenye chama ambacho mwenyekiti anaweza kuwageuza deal wakati wowote. Chadema mna hali mbaya sana October 28.
Wewe ndio msemaji wa wasanii?
Queen Esther
 
Fatilia alichoongea Diamond kule Mbea leo hii kuhusu Magufuli na Wasanii. Pia ameeleza namna walivyofanikiwa na hawarudi nyuma.

Queen Esther

..mahusiano ya mwanasiasa na msanii kwa hapa Tz ni ya bwana na mtwana.

..kwenye mataifa ya wenzetu wasanii wana nguvu za kiuchumi na hawaendeshwi na wanasiasa.

..Ni kweli kuna wasanii, lakini sio kuzidisha kama ilivyo hapa Tanzania.

..huwezi kusikia msanii katunga wimbo maalum kwa ajili ya kampeni za Donald Trump, au Boris Johnson.
 
Malkia Jezibel asiyeyajua maandiko ni mama wa makahaba.
Tunapoimba kanisani, tunamuimbia Mungu mkuu jehova, sifa na utukufu ni kwake, sio kwa mahubiri.
Mnalawitiwa na wachungaji feki wenu kwasababu mnawasifu wao na kuwatukuza wao badala ya Mungu.
Kwahiyo wewe ndio Ahab???
Queen Esther
 
Back
Top Bottom