MK254
JF-Expert Member
- May 11, 2013
- 32,408
- 50,809
Binafsi huwa nimekata tamaa likija kwenye suala la bunge letu na siasa za kwetu hapa Kenya, ila kila nikipitia jukwaa la siasa za majirani zetu yaani najikuta nikikubali siasa zetu na kuziona nafuu. Yaani kule Tanzania Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuna kipindi alihojiwa kuhusu ucheweleshwaji wa taarifa alizotoa zilizo onekana kuumbua ufisadi, akajibu kwa kutamka maneno 'udhaifu wa bunge', yaani hakusema 'bunge dhaifu' ila 'udhaifu wa bunge'.
Hayo maneno yamesababisha amebamizwa na bunge lenyewe, ilhali wakati yalikua maoni yake kwenye mahojiano.
Dunia hii kila taasisi ina udhaifu wake, hivyo sio kosa kusema 'udhaifu wa urais', lakini itakua kosa kusema 'rais dhaifu'.
Siasa zingine ziskie tu huko kwa majirani na zibaki huko huko......
Hayo maneno yamesababisha amebamizwa na bunge lenyewe, ilhali wakati yalikua maoni yake kwenye mahojiano.
Dunia hii kila taasisi ina udhaifu wake, hivyo sio kosa kusema 'udhaifu wa urais', lakini itakua kosa kusema 'rais dhaifu'.
Siasa zingine ziskie tu huko kwa majirani na zibaki huko huko......