Siasa za Umeme: Kwa vile Umeme wa Stigler's utatosha na ziada kuuza nje. Je, TANESCO kusaini PPA mpya 6 toka kwa 6 IPPs, sio ufisadi mpya wa kisasa?

CHA MSINGI MKATABA UWE OPEN WANAUZIWA UNIT 1 KWA SHILINGI NGAPI SIYO KUTULETEA MAMBO RICHMOND NA IPTL HAPA>>unit 1 ISIZIDI sh 100

NA KULE RUFIJI WANACHIMBACHIMBA TU
NUCLEAR NDIO SOLUTION PEKEE YA UMEME HAO MABEBERU WANATUMIA HALAFU WANAZUGIA KWENYE UPEPO NA MAJI KUTUDANGANYA SISI WAAFRICA
 
Majibu ya Pascal yapo hapa,Welldone!!
 
Ninaona aidha uko confused au unataka kwa makusudi ku confuse watu kwa lugha hiyo ya capacity factor, installed capacity, generated energy capacity, delivered energy capacity and so on. Nadhani lengo lako ni ku justify tanesco kununua umeme huo wa wamachinga na kuja kutuuzia sisi badala ya wamachinga hao kutuuzia sisi mojamkwa moja hiyo bidhaa yao ya umeme.

Nimejaribu kutumia lugha nyepesi kurlezea logic ya biashara hiyo. Nitatoa ufafanuzi na mifano rahisi kama ifuatavyo;

1. Chukulia grid ya taifa kama ni lori la tani 10. Yaani lori hili lina uwezo wa kubeba mzigo wa tani 10. Hivyo installed capacity ya lori hili ni tani 10. Wateja waliopatikana jumla ya mzigo wao wanaotaka kuusafirisha ni tani 8 tu. Hivyo litasafirisha tani nane kwa operating expense hiyo hiyo kama lingesafirisha tani 10 hususani idadi ya lita za diseal nk. Delivery capacity ya tani 8 au hata tani 1 linayo. Sasa itakuwa ni uendawazimu kwa mmiliki wa lori hilo la tani kumi kukodisha bajaji sita kutoka watu binafsi kumsaidia kusafirisha mzigo huo wa tani 8 wa wateja wake. Yaani lori hilo na bajaji hizo 6 zitumike kusafirisha mzigo huo.

2. Ukiacha umeme wa jua kuchaji mabetri (solar electricity), umeme huzalishwa na mashine zinazoitwa power generators ambazo hutumia (kuwaka) aidha mafuta ya petroli, diseal, gas, makaa ya mawe, nguvu za atomic au nguvu za upepo. Kila mashine ya hizi generators ina uwezo wake wa kiasi cha umeme itakaoutoa pale itakapowashwa (installed capacity) kama hilo lori la tani 10. Chukulia generator yako ya nyumbani yenye capacity ya 5,000 kw. Ukiiwasha umeme inaotoa unawezo wa kuwasha jiko lako la umeme, taa zako zote za nyumbani, fridge zako za nyumbani, washing machine yako, water heaters za bafuni kwako, microwave yako, tv zako zote, computer zako zote nyumbani na pasi yako zote kwa wakati mmoja. Kama utawasha taa chache tu fridge moja na tv moja tu, umeme mwingi utakaokuwa unazalishwa na hiyo generator yako ukiwa umeiwasha ndiyo tunaouita uko iddle. Yaani kwenye grid yetu ya taifa hadi sasa ina umeme wa 550 MW ambao uko iddle hatuutumii. Sababu kubwa hatuutumii ni kwamba bei ya kilowatt hour moja ya tanaesco ni kubwa sana kuliko nchi zote duniani. Hii imetokana na ufisadi wa miaka mingi katika shirika hili.

3. Kahama imekuwa ikipata umeme wa kutosha kutoka mgodi wa.almasi wa William Diamonds kabla hata tanesco haijazaliwa. Sasa hivi inapata umeme wa kumwagwa kutoka grid ya taifa ya tanesco. Sasa eti kuna jamaa anazalisha 10Mw za umeme wa solar ambao atakuwa anawauzia wanakahama kupitia tanesco! Yaani tanesco mnatuona sisi ni wajinga sana? Kuzalisha 10MW za umeme wa solar unahitaji solar panel 10,000 zenye capacity ya 100 watts kila moja na betri 60,000 za 300A au panel 5,000 zenye capacity ya 200W kila moja na betri 30,000 za 300Amps. Kiasi hicho cha ma solar panels na ma betri ku occupy eneo lote la mji wa kahama na pasitoshe. Huyo jamaa hana kiasi hicho cha ma panels na ma betri. Halafu what for and why all this expense?

4. Tanesco ina off grid power plants kwenye maeneo mengi tu nchini ambayo aidha hayajafikiwa na grid ya taifa au yako kwa ajili ya standby operation during national grid cut off. Off- grid power plants hizi hutumia diseal fired generating engines zenye capacity mbali mbali. Kwa mfano uwezo wa off grid power plant ya Mwanza iliyoko Nyakato ni MW 60, ya Kigoma ni 6.25MW from 5 generating units, Kasulu 2.5MW from 2 units. Plants za aina hii zipo pia kule Biharamulo, Mafia, Ludewa, Mpanda, Bukoba in case of the Uganda grid cut off, Liwale, Sumbawanga, Tunduru na Namtumbo. Hakuna sehemu ambako tanesco inahitaji huo umeme wa hao IPP sita.
 
Hii mada imekaa kitaalamu, ila nimeshangaa huko juu nimeona mtu mmoja anadai ya kuwa uhitaji utaalamu kung'amua kadhia hii.

Mabadiliko na mahitaji hayamsubirii mtu, bali kujiandaa ndiyo jambo bora zaidi. Hapa ingekuwa ni hoja ya msingi kujadili uwezo wa hizi kampuni ndogo,je zina uwezo au (Hili wahusika watalifanyia kazi).

Kwa nchi yetu ni ngumu au itachukua muda mrefu sana Umeme wa gridi ya Taifa kuwafikia watu wote na hii si lazima sana, ndiyo maana kuna wakati kununua Umeme kwa nchi jirani au kwa kampuni huwa ni gharama ndogo sana kuliko sisi kupeleka umeme wa gridi sehemu husika. Mathalani kwa eneo la Wilaya ya Kalambo kwa kipindi kile ilikuwa ni gharama sana kupeleka umeme wa gridi kuliko kununua umeme toka Zambia. Ndiyo maana tulikuwa tunanunua Umeme toka huko.

Lakini pia hivyo vyanzo vingine vinaweza kutumika kama "Stand by".

Nina mengi ya kuandika juu ya kadhia hii, ila nisiwachoshe sana, nakomea hapa.
 
Mimi binafsi nimekuelewa.
 
Uwe na Akili na wewe. Kuna sehemu Grid ya Taifa haijafka,,maana yake wanaweka umeme wa jenereta sehemu ambazo hakuna muunganiko na gridi ya Taifa.,,na hapo baadae wataunganishwa na grid
 
Stiglers Gorge haijazalisha umeme na watu wanataka umeme leo. Tutajadiliana tena mambao haya huko mbeleni tukishakuwa na umeme wa ziada, ila kwa sasa hivi tuna upungufu wa mahitaji.
 
Nadhani lengo lako ni ku justify tanesco kununua umeme huo wa wamachinga na kuja kutuuzia sisi badala ya wamachinga hao kutuuzia sisi mojamkwa moja hiyo bidhaa yao ya umeme.
Kwa taarifa yako uuzaji wa umeme kutoka kwa hao unawaita 'wamachinga' unaongozwa na kanuni maalumu zilizowekwa na muangalizi wa mambo haya, EWURA. Hata Tanesco bei yao ya umeme inaratibiwa/ridhiwa na EWURA. Suala la bei ya umeme ama kutoka kwa hao unaowaita 'wamachinga' ama TANESCO siyo suala la kusumbua 'akili' kiasi cha kuanza kuulizana bei ya umeme ya pande hizi mbili!

Hivyo litasafirisha tani nane kwa operating expense hiyo hiyo kama lingesafirisha tani 10 hususani idadi ya lita za diseal nk
Nadhani hapa ndipo tunapoanza kupishana!!
===
Yaani lita za mafuta ya diesel zitakazotumika kusafirisha mzigo wa tani 10 kutoka (mfano) Dar kwenda Mbeya ni sawa na kiasi hicho kwa kusafilisha mzigo wa tani nane! Kwa taarifa yako ni kuwa gari likiwa limebeba mzigo mzito huwa linalazimika kutembea kwenye gia kubwa. Gia kubwa hufyonza mafuta zaidi, ili injini iwe na uwezo wa kuhimili mzigo huo. Gari likiwa na mzigo mdogo mara nyingi linatembelea kwenye gia ndogo kwani injini haihitaji nguvu kubwa hivyo haifyonzi mafuta mengi.

Mapungufu haya uliyoyaonyesha katika hili yana ua kabisa morali ya kuamini kuwa unatosha kabisa kufafanua suala lilipo mezani bila 'upendeleo'!

Kwa maelezo hayo hapo juu, nadhani wanaJF wataamua wenyewe ni nani wanamuona "... aidha yuko confused au anataka kwa makusudi ku confuse watu kwa lugha hiyo...."
 
No mimi sioni tatizo la TANESCO kwa kuingia mikataba kwa wazalishaji wadodo wa ndani kuwauzia umeme hata kidogo. Umeme wa maji mara njingi huwa rahisi kuliko wa mafuta, kinachotakiwa kulinda hapo ni mikataba imekaaje iwapo TANESCO wataweza kupata umeme wa kutosha toka kwenye vyanzo vyao. Now here comes back to capacity charges. Najua TANESCO wameingia kwenye migogoro mingi kwa kuingiliwa na wanasiasa sio wao wenyewe. Na hili ni uzembe wa TANESCO yenyewe kwa kuwa na poor strategic plan na kuacha mianya ya wanasiasa kujichomeka kwenye mambo yao. Nahisi watanielewa.
 
Paskali, Ujinga wa Tanesco ni kung'ang'ania solar. Solar is a stupid alternative. Ni umeme unaozalishwa mchana tu! Kwa 10 MW huwezi nieleza kwamba utakuwa na storage yake kwa miaka 10. Kinachowashawishi saana ni rushwa. Ukiangalia kazi zote za solar TANESCO na REA wao huwapa makampuni binafsi maana ni kazi ambazo wao wenyewe hawawezi kuzifanya, hapo wana 10% yao.

Kuna kampuni kama CAMCO wanaojiita clean energy wamewashika utadhani ni taasisi ya serikali na kumejaa usanii tu! Inatia uchungu lakini sijui kuna nini hadi Kalemani na TANESCO hawasikii. Kalemani anaweza kuwa na immunity ya Chato lakini kwa kiwango kikubwa kabisa naweza kusema kuna ufisadi nyuma yake.
 
Bado nasisitiza uamuzi wa TANESCO ni safi kwasababu kubwa moja hii ku encourage private operators kusaidia uzalishaji wa power. Niliwahi kukaa kidogo Europe, nilishangaa nyumba tuliokuwa tukiishi mwenyenyumba alikuwa ameweka solar pannel zake nyingi sana juu ya mapaa ya nyumba zetu. Nikapata wasaa wa kuonge nae inakuwaje ana solar pannels nyingi vile na zinamsaidiaje?. Akaniambia zinamsaidia sana hasa kipindi cha kiangazi kwani kipindi hicho yeye huuza umeme kwa shirika lao la umeme. Kwahiyo kipindi hicho analipwa yeye badala ya yeye kilipia umeme. Hili nalo tulitazame hivi badala ya kuwa wagumu kuelewa na kuangalia the darkest part of TANESCO.
 

Tuliambiwa Taasisi za dini zisijihusishe na siasa, hapa naona taratibu Yesu akiwekwa kando (...Padre Luciano Mpoma na Nicholas Richardson wameishukuru Serikali kupitia TANESCO kwa kukubali kufanya nao biashara ya umeme).

Labda sadaka hailipi
 
Paskali bila kupunguza ladha ya uzi wako, nilishangaa na kuchanganyikiwa kusikia kuwa huu mradi wa umeme wa SG hauko kwenye miradi ya umeme inayofahamika na TANESCO!
Hivi katika nchi yetu hii kuna Umeme wa SG ndugu yangu si kila jambo unatakiwa uchangie kama hujui jambo kaa kimya ufiche ukilaza wako.
 
Logic thinking inatakiwa izingatie ukweli. Siyo kweli kwamba ukiwasha generator lako la nyumbani litatumia mafuta machache kama utazima vifaa vyako vyote vya nyumbani na kubakiza taa chache za watts 5 kila moja. Siyo ukweli kwamba basi lako lenye uwezo wa kubeba abiria 60 kutoka Dar hadi Mwanza litatumia mafuta machache kama utabeba abiria 30. Kwamba kama linatumia mafuta ya lita 200 likiwa limebeba abiria 60 kwa hiyo likiwa limebeba abiria 30 litatumia mafuta ya lita 100; ni logics za vilaza wa hisabati za shule ya msingi watakaokuambia kuwa kilo moja ya mawe ni nzito kuliko kilo moja ya pamba.

Lengo letu hapa si kwa wana Jf kuamua. Lengo letu ni kuijulisha serikali kuhusu ufisadi katika shirika letu la umeme. Wameanza IPPs ndogo ndogo 6. Wataendelea na zingine na zingine, hatujui mwisho wake. Hata zile IPPs kubwa kubwa zitakuja. Tunarejea huko huko kwenye maumivu tuliyoyapata kutoka kwa IPPs za akina Songas, Simbion, Dowans, Rugemalila na yule singasinga.

Tunachosema ni kuwa shirika letu la umeme linaingia mikataba na IPPs hizi tukiwa:

1. Tuna umeme wa ziada wa kiasi cha 550MW zilizo iddle kwenye grid yetu ya taifa.

2. Tuna off grid standby power plants zenye diseal fired generators za kisasa kwenye maeneo yote Tanzania, zilizo na capacity ya jumla ya MW sisizopungua 200MW.

3. Tunaendelea na ujenzi wa hydro power plants huko Rusumo (180 MW), Kikongwe - Ruvuma (300 MW), Songwe - Mbeya (180 MW) na Julius Nyerere - Morogoro (2,115). Hydro power plants ambazo kwa ujumla wake zitatoa MW 2,775 zinatarajiwa kukamilika ndani ya miaka 2 ijayo na kuingizwa kwenye grid ya taifa. Hivyo tuki assume kwamba ndani ya miaka 2 ijayo kama matumizi yetu ya umeme yatabaki kama yalivyo sasa, grid yetu ya taifa itakuwa na umeme wa ziada ulio iddle wa kiasi cha MW 550 + 2,775 = 3,325 MW. Ni umeme mwingi sana ambao utakuwa hauna wateja na utakuwa umekaa tu iddle.

Tunachosema ni kuwa shirika letu la umeme linachotakiwa kufanya ni kuhangaika kupata soko la kuuza huo umeme ulio iddle. Na soko kuu ni kwa sisi watanzania. Watuuzie kwa bei ndogo. Wakipunguza sana bei zao, umeme huo utauzika hapa hapa nchini. Wangaliweza hata kutupa bure kuliko kuuacha iddle.

Tatizo kubwa ni kwamba wafanyakazi wa tanesco hujigawia umeme bure. Ndiyo maana hawajui machungu ya bei zao za umeme. It is high time now wafanyakazi wa tanesco watakiwe kulipa umeme wanaotumia majumbani kwao. Mbona madaktari na manesi wakiugua hawajitibu bure? Mbona walimu watoto wao walikuwa hawasomi bure? (kabla ya jpm kusomesha watoto wote bure). Mbona wafanyakazi wa mamlaka ya kodi wanalipa kodi? (sina uhakika kama wanalipa). Mbona mapolisi wanaokamata watu nao hukamatwa? Mbona maaskari wa magereza nao hufungwa magerezani? Kwa nini hawa wafanyakazi wa tanesco wajigawie umeme uliotokana na jasho (kodi) letu wote wao wanajichotea bure? Halafu wanatuletea figisu figisu wa umachinga kwenye umeme wetu.

Serikali ichukue hatua dhidi ya wahusika katika mikataba hiyo ya kifisadi ndani ya tanesco. Sasa ni muda muafaka bei ya umeme ianze kupunguzwa. Kupunguza kwa bei ya umeme itachochea sana ukuaji wa uchumi wa nchi yetu. Nina uhakika bei ya umeme ikipunguzwa hadi kuwa TSh 50 kwa unit, kasi ya kuongezeka kwa ukuaji wa uchumi wa nchi yetu itakuwa kubwa sana na kutuwezesha kuwa nchi ya uchumi wa kati wa juu (high middle income country) ifikapo 2025 kama ilivyolengwa kwenye ilani ya uchaguzi ya ccm ya 2020 - 2025.
 
2. Tuna off grid standby power plants zenye diseal fired generators za kisasa kwenye maeneo yote Tanzania, zilizo na capacity ya jumla ya MW sisizopungua 200MW.
Asante kwa ufafanuzi wako na pia kumradhi kwa kuchelewa kujibu bandiko lako. Nimelisoma lote. Kikubwa hapa, mengine 'gentlemanly' tukubaliane kutokukubaliana.

Hata hivyo, msingi wa hoja yangu ya kuunga mkono TANESCO kuingia mikataba hiyo sita ni kuwa hatua hiyo, kama nilivyoeleza awali, inaambata na utekelezaji wa maelekezo yaliyo katika sera ya Nishati nchini ya mwaka 2015. Maelezo ambayo ni kuongeza matumizi ya nishati jadidifu ( renewable energy) katika matumizi ya jumla ya nishati nchi. Tanesco wana tekeleza sera hiyo ambayo kama nchi tuliikubali kuifuata.

Pia nimeishaeleza kuwa Tanzania imeridhia utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu(sustainable development goals i.e. SDGs). SDGs hizi zinahusisha lengo namba saba linalohimiza kuongeza matumizi ya nishati jadidifu.

Faida za matumizi ya nishati jadidifu zimeelezwa ikiwemo kupunguza athari hasi ya mabadiliko ya tabia nchi yaani kwa kupunguza gesi za ukaa hewani zinazoongeza joto duniani. Na athari za mabadiliko hasi ya tabia nchi yameishaonekana. Gesi za ukaa uharakisha sana mabadiliko haya hasi ya tabia nchi. Na chanzo kikuu cha gesi hizi ni matumizi ya nishati ya ukaa yaani " fossil fuel" kwa lugha ya kimombo. Fossil fuels moja wapo ni mafuta ya dizeli, ambayo umeeleza kuwa bado Tanzania tunazalisha umeme wa 200 MW( takwimu hii sikuwa nayo) kwa kutumia mafuta haya. Kwa sera na malengo tuliyokubali kuyafuata juu ya matumizi ya nishati jadidifu, hizi 200 MW inabidi ziondolewe kwenye ukokotoaji wa matumizi ya Nishati nchini. Tanesco wameanza kupunguza 19 MW ( kama ulivyoeleza) kutoka hiyo 200 MW kwa kuingia mikataba sita ya uzalishaji wa nishati jadidifu. Kwa taarifa yako tu, tunafikiria sasa kupata umeme kutoka kwenye gesi ya Hydrogen kwa kuchakata maji endapo upembuzi yakinifu utaonyesha kuwa Tanzania ipo kwenye nafasi ya kufaidika na teknolojia hiyo. Teknolojia hii inaangukia kwenye teknolojia za nishati jadidifu. Kwa hiyo andaa mashambulizi yako sawa sawa!

Sasa, Mkuu, kwa kuhitimisha, kama hukubaliani na kinachofanywa na serikali kupitia TANESCO juu ya uongezaji wa matumizi ya nishati jadidifu, basi kwa ustaarabu na utaratibu makini unatakiwa uanze kampeni ya kwanza kubadilisha sera ya nishati ya mwaka 2015 ili iakisi matakwa yako ya kupinga matumizi ya nishati jadidifu; pili uanze mkakati wa kuishawishi serikali ijitoe kwenye utekelezaji wa SDGs. Mimi nakuahidi kuwa nitakupinga kwa nguvu zote usifanikiwe mpango wako huo kwa sababu faida za matumizi ya nishati jadidifu ni kubwa sana kwa ustawi endelevu wa uwepo wa binadamu duniani.
 
Pamoja na juhudi za kumwimbia mapambio, Jiwe kaenda zake akiwa amelowa damu mwili mzima na kabeba mzigo wa manung'uniko na laana kutoka binadamu, watz wenzie.
Kama huo ukandamizaji na unyanyasaji, ndio moyo wa kukemea na kumaanisha uliyotaka kutuaminisha, basi mtazamo wako UTAENDELEA kutia shaka sana. AMEN
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…