Pre GE2025 Siasa za upinzani zimefikia kilele kwa CHADEMA, hakuna mbadala wake

Pre GE2025 Siasa za upinzani zimefikia kilele kwa CHADEMA, hakuna mbadala wake

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Ukifuatilia siasa za upinzani za nchi hii utaona NCCR Mageuzi ilianza kama chama mahiri cha upinzani Tanzania kikapotea katika ramani kisha CUF ikafuatia kama chama kikuu cha upinzani nacho kikapotea katika ramani ikafuatia CHADEMA ambayo imekuwa chama kikuu cha upinzani kwa karibia miaka 15 sasa.

Inavyoonekana ni kwamba endapo CHADEMA itafifia kipindi hiki hakuna chama mbadala cha siasa cha upinzani kwa sasa kuchukua nafasi yake.

Wanachama na wapenzi wake wengi wana machaguo makubwa matatu ambayo ni kubaki CHADEMA kupambania ndani kwa ndani, kwenda CCM au kuachana na siasa kabisa.
 
Ukifuatilia siasa za upinzani za nchi hii utaona NCCR Mageuzi ilianza kama chama mahiri cha upinzani Tanzania kikapotea katika ramani kisha CUF ikafuatia kama chama kikuu cha upinzani nacho kikapotea katika ramani ikafuatia CHADEMA ambayo imekuwa chama kikuu cha upinzani kwa karibia miaka 15 sasa.

Inavyoonekana ni kwamba endapo CHADEMA itafifia kipindi hiki hakuna chama mbadala cha siasa cha upinzani kwa sasa kuchukua nafasi yake.

Wanachama na wapenzi wake wengi wana machaguo makubwa matatu ambayo ni kubaki CHADEMA kupambania ndani kwa ndani, kwenda CCM au kuachana na siasa kabisa.
Niko makini kufuatilia na kujua kama viongozi wanaopiga kula kuamua nani atakua mwenyekiti wa chama hicho kama wana akili timamu ama Wendawazimu wanaotanguliza matumbo mbele bila kutumia akili hata za mtoto wa miaka 4.

Sisi tulioupenda na kufuatilia upinzani Toka enzi hizo tuko makini sana sana!! Hatima ya Chadema iko mikononi mwa hao wajumbe, wakiweka tumbo mbele kweli chama kinazikwa rasmi mlimani city
 
ACT wazalendo ndio Chama kikuu Cha upinzani na kitadumu

Chadema inajizika yenyewe bila mbambamba 21 January 2025

Happy New Year 😄
 
Think Tank ya CHADEMA

1000020998.jpg
 
Ukifuatilia siasa za upinzani za nchi hii utaona NCCR Mageuzi ilianza kama chama mahiri cha upinzani Tanzania kikapotea katika ramani kisha CUF ikafuatia kama chama kikuu cha upinzani nacho kikapotea katika ramani ikafuatia CHADEMA ambayo imekuwa chama kikuu cha upinzani kwa karibia miaka 15 sasa.

Inavyoonekana ni kwamba endapo CHADEMA itafifia kipindi hiki hakuna chama mbadala cha siasa cha upinzani kwa sasa kuchukua nafasi yake.

Wanachama na wapenzi wake wengi wana machaguo makubwa matatu ambayo ni kubaki CHADEMA kupambania ndani kwa ndani, kwenda CCM au kuachana na siasa kabisa.
Swali kwako: Baada ya CHADEMA kufa rasmi na wafuasi wake kusambaratika,

Unaamini roho ya upinzani nchini itakuwa imezima kabisa? Kwamba watanzania wote watakuwa muafaka na yanayoendelea katika utawala uliopo na dola yake? Kwamba watanzania wote watakuwa radhi kukubaliana na kauli zote za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa JMT kuhusu mustakabali wa taifa hili (Totalitarianism)?
 
ACT ikiweka mambo yake sawa na kupata watu wenye majina makubwa ni mbadala mzuri tu.
 
Ukifuatilia siasa za upinzani za nchi hii utaona NCCR Mageuzi ilianza kama chama mahiri cha upinzani Tanzania kikapotea katika ramani kisha CUF ikafuatia kama chama kikuu cha upinzani nacho kikapotea katika ramani ikafuatia CHADEMA ambayo imekuwa chama kikuu cha upinzani kwa karibia miaka 15 sasa.

Inavyoonekana ni kwamba endapo CHADEMA itafifia kipindi hiki hakuna chama mbadala cha siasa cha upinzani kwa sasa kuchukua nafasi yake.

Wanachama na wapenzi wake wengi wana machaguo makubwa matatu ambayo ni kubaki CHADEMA kupambania ndani kwa ndani, kwenda CCM au kuachana na siasa kabisa.
Ndicho Ccm ilikiplani muda mrefu kwa gharama yoyote ili kitokee kwa manufaa yake.

Lakini cha kushangaza, waTz walio wengi mpaka sasa hawamuelewi kwa jina mchawi aliyepo nyuma ya jambo hili ni nani.

Unamkumbuka Mrema alichokifanya baada ya uchaguzi mkuu 1995?

Kazi yake ilikuwa ni kutengeneza migogoro ndani ya vyama, akikivuruga hiki anahamia chama kingine.

Kaendelea na mtindo huo wa hamia vuruga mpaka mwishoni kabisa karibu na shimo la kaburi lake, ndipo akajidhirisha rasmi kwa kumuunga mgombea wa Ccm, kuwa alikuwa mCcm aliyetumwa vyama vya upinzani kwa kazi maalumu.

Kumbuka matendo ya Ibrahim Lipumba, John Cheyo, James Mbatia na sasa Mbowe katika vyama vyao, utaelewa ninachokiongelea, ni wale wale kasoro ni tarehe tu.

Mtaongea, mtalalamika sana, sijui aachie ngazi kukilinda chama!

Akilinde chama kwa faida ya nani sasa, yeye kazi yake aliyopelekwa na Ccm siyo kujenga chama bali ni kukidhoofisha na kukisambaratisha.

Yaani hata wanachama wote mumkimbie abaki peke yake, hakuna anakachokipoteza, lengo mahsusi anakuwa kashalitimiza , zaidi ni kupewa tuzo ya mfanya kazi bora iliyotukuka.

Muda ndiyo mwalimu mkuu, tuombe uzima kushuhudia hivi vimbwanga vya siasa za Tz.
 
ACT ikiweka mambo yake sawa na kupata watu wenye majina makubwa ni mbadala mzuri tu.
ACT ilipata udumavu muda mfupi tu baada ya kuanzishwa, tofauti na Kigoma kidogo hakuna watu wenye mpango nayo kwa sehemu kubwa ya Tanganyika. Zaidi sana inaonekana CCM B.
 
Swali kwako: Baada ya CHADEMA kufa rasmi na wafuasi wake kusambaratika,

Unaamini roho ya upinzani nchini itakuwa imezima kabisa? Kwamba watanzania wote watakuwa muafaka na yanayoendelea katika utawala uliopo na dola yake? Kwamba watanzania wote watakuwa radhi kukubaliana na kauli zote za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa JMT kuhusu mustakabali wa taifa hili (Totalitarianism)?
Hata CHADEMA ikisambaratika upinzani hauwezi kufa kabisa, itachukua muda tu upinzani kujikusanya upya au hata kuibuka ndani ya CCM. Kukishakuwepo siasa za vyama vingi upinzani hauwezi kukosekana.
 
Hata CHADEMA ikisambaratika upinzani hauwezi kufa kabisa, itachukua muda tu upinzani kujikusanya upya au hata kuibuka ndani ya CCM. Kukishakuwepo siasa za vyama vingi upinzani hauwezi kukosekana.
Ccm haitaki upinzani ufe.
 
Hata CHADEMA ikisambaratika upinzani hauwezi kufa kabisa, itachukua muda tu upinzani kujikusanya upya au hata kuibuka ndani ya CCM. Kukishakuwepo siasa za vyama vingi upinzani hauwezi kukosekana.
Btw, upinzani haujawahi kufa hata katika nchi zinazoongozwa na madikteta katili kiasi gani. North Korea kuna wapinzani wananyongwa kila kukicha kama wasaliti. Ni hulka ya msingi ya binadamu. Mobutu alikuwa ananyonga hadharani hata wenye kuhisiwa tu kutomuunga mkono lakini hakufanikiwa kikamilifu. Aliishia kukimbia nchi.

HIVYO siasa za upinzani hazitafika kilele kwa kifo cha CHADEMA ambacho, hata hivyo, bado hatuna uhakika kama kitatokea.

CCM sio chama cha siasa: ni mamlaka; ni dola. Sio MBADALA wa kukimbilia kwa wanaotaka kufanya kazi ya siasa makini. CCM ni kimbilio la wanaoamua kuingia kwenye mashindano ya kutumika/kujikomba kwa watawala waambulie mgao wa fursa za ulaji wa rasilimali za nchi zinazotolewa kwa upendeleo (patronage).
 
Hata CHADEMA ikisambaratika upinzani hauwezi kufa kabisa, itachukua muda tu upinzani kujikusanya upya au hata kuibuka ndani ya CCM. Kukishakuwepo siasa za vyama vingi upinzani hauwezi kukosekana.
CHADEMA hakisambaratiki. Kilichopo CHADEMA ni mgongano wa kimaslahi baina ya makundi yaliyopo CCM. Kuna kundi linataka kuhamia CHADEMA kugombea urais na kuna kundi linataka CHADEMA kisiwe na nguvu kurahisisha mama apite kirahisi. Lakini hali itakuwa tete siku za usoni.
 
Back
Top Bottom