Sidhani kama Wabunge huwa wanaelewa maana ya Finance Bill, wangeelewa wasingekuwa wanasema hela zinatolewa na viongozi wa serikali

Sidhani kama Wabunge huwa wanaelewa maana ya Finance Bill, wangeelewa wasingekuwa wanasema hela zinatolewa na viongozi wa serikali

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Muswada wa Fedha(Finance Bill) ikishapitishwa na Bunge na kusainiwa na Rais wa JMT inakuwa Sheria.

Kwahiyo kila Matumizi yatakayofanywa yanakuwa ni Kwa mujibu wa sheria na ndivyo ilivyokuwa hadi Mzee Kikwete anamaliza muda wake.

Ilipoingia awamu ya 5 ndio tukaanza kusikia Wabunge wanamshukiru Shujaa Maguful Kwa kupeleka Fedha za kununua Madawa kwenye majimbo yao nk.

Na ukiwasikiliza Wabunge wa sasa wanapokaa kama Kamati utaona Kabisa wanajilazimisha tu lakini hawajui tofauti na Wakati Ule wa J J Mnyika, Zitto Kabwe na James Mbatia.

Mungu wa Mbinguni awabariki!
 
Hayo yote yaliletwa na mwendazake kutuletea bunge mbumbumbu.
 
Watanzania tupiganie kulirudisha Bunge lenye watu wanaojitambua. Viti maalum tupiganie vifutwe. Wabunge wasiojielewa wao, kila kitu ndiyo wasirudi bungeni. Ila watanzania ni wazito uwiiii 🙆‍♂️🙆‍♂️🙆‍♂️🙆‍♂️🙆‍♂️🙆‍♂️
 
Back
Top Bottom