Siendi Mkoani Ng'ooo!! Dar es salaam is the future! Mikoani ni didimizo la uchumi binafsi

Nyie mnaosema Mikoani nje ya Dar hakuna fursa mnaongelea mikoa gani maana inaonekana mnataka kutuaminisha kwamba mikoa yote iko nyuma kiuchumi ukiacha Dar. Huenda Dar ina fursa zaidi ya mikoani lakini kuna mikoa kama Arusha, Mwanza, Morogoro, Mbeya n.k. nako kuna fursa nyingi kama akili yako inachaji.

Na kama ugumu wa maisha Arusha nadhani inakaribiana kabisa na Dar hivyo ukiishi huko ubongo lazima uchemke. Juzi nilikuwa Iringa, nilipotajiwa bei za kupanga nyumba nilishangaa sana, sikuamini kama nao wamefikia hapo. Nadhani ni kwa sababu ya vyuo vikuu vilivyoko huko.
 
Sehemu nyingine ukitembeza nyama choma round za bia kwa sana kwa wapambe then ukiwa na Range Rover tatu na ndege ndogo na nyumba kadhaa basi wewe ni billionaire wakati the number one richest man in Tanzania hajathubutu kujiita billionaire

aaaha ngoja vijana wa A-town wakusikie
 
Miaka kumi nyuma nilikuwa na wazo kama wewe na point kama hizo.. Nilishangaa sana kwa kijana kupata kazi mikoani na kukubalii.. ILA BAADA YA KWENDA KUISHI EUROPE KWA 4YRS NA USA KWA ZAIDI YA MIAKA MINNE.. Niliporudi nilianza kuangalia fursa na kuzitumia.. katika mikoa 15 niliyozunguka Dar ulikuwa mkoa wa mwisho kabisa katika list... Inategemea fursa unaziangalia vipi? na njia gani unapenda kupatia fedha..
Nipo mikoani na nina expand kuelekea mikoani na soko ninalolenga ni zaidi ya dsm.. SINA TATIZO LA FOLENI(sipotezi muda) SIKAI MAENEO YA MABONDE NA MILIMA(kimara, goba na kunapofanana)
Ingawaje ninakiri kitu kimoja RASILIMALI WATU WA MIKOANI WAPO WAZEMBE SANA NA WANARIDHIKA KWA VITU VIDOGO. ila hili sasa si tatizo kwangu kuna wakenya wengi TZ na wanaishi kama WATZ hakuna haja ya kibali cha kazi...
 

Mikoani wakati mwingine ni kama sehemu ya kuchukulia umaarufu alafu ukirudi jijini unakuwa umejipanga hata CV yako inakuwa kubwa
 
Ila kama munagusa penyewe ...hivi leo hata hao ma RPC, DC, RC au Wakurugenzi "mkulu wa kaya" akiwapa karatsi ya kujaza mahala wanapopenda kufanyia kazi, hakika zaidi ya asilimia 95 watajaza na kuchagua "kituo cha kazi-DAR ES SALAAM".
 
mdau lara 1 umefunguka madini muhimu sn,but mimi nakichanga huku huku niliko natafuta mtaji na ninawekeza mjini,nina principal moja kuwa siku nikirudi narud km enterpreneur na si employee tena,mjini ndo kila kitu,ila fursa ni kutokana na mtazamo,nia na malengo,hivyo fursa zimetawanyika.
 
Watu mnachanganya madesa,mwanzisha mada hajasema mikoani hakuna fursa bali hakuna changamoto nzito kama Dar hivyo mafanikio kidogo yanakufanya ubweteke.

Mimi nimefanya kazi mikoani najua hili.mtu ukiwa na viji gari viwili na uwezo wa kunywa bia kila siku na kamjengo ka wastani unaheshimika sana while ungekuwa Dar hata jirani yako hakujui hivyo Dar daima unapigana kufikia level fulani walau uonekane upo mjini!!!
 
Sio tu mkoani hata hapa dar kuna maeneo hakuna ushindani wala inspiration,mie naishi uswahilin nina miaka 24 tu nina gari na vipesa flani basi naonekana matawi mtaani balaa naheshimika yote hii ni kwasababu nimezungukwa na maskini na wenye elimu duni kama na mie ningekua mtu wa kuridhika ahh mbona ningejiachia tu.sasa mie nimesoma shule nzuri since primary so nimesoma na watu ambao wanatokea familia nzuri na wana ambitions za hatari kila tukikutana na wenzangu naona wanazidi kupiga hatua tu iwe kielimu,kipesa,kikazi hao ndio wanakua inspiration yangu coz sitaki kupitwa nao kwa hiyo najiona bado naendelea kuhustle hard.laiti kama ningekua nimezaliwa na kusoma kiswaziswazi nadhan pia ningekua nisharidhika kitambo coz wenzangu wengine wangekua labda wana kazi na elimu ya kawaida tu mie ningekua top wao lol!!
 
Sehemu nyingine ukitembeza nyama choma round za bia kwa sana kwa wapambe then ukiwa na Range Rover tatu na ndege ndogo na nyumba kadhaa basi wewe ni billionaire wakati the number one richest man in Tanzania hajathubutu kujiita billionaire

hili dongo kwa watu wa arusha
 
...wamasai wa arusha wanabeba maboksi ya pesa kwenda benki,mfano ukienda pale crdb wana sehemu kuna bulk cash,watu wanadeposit tsh mil 200, mia tatu kwa foleni, ukija dar unakuta eti mil50 mwenye duka anasafirisha kwa escott,alaf eti mimi siko benki za wabongo nina akauti barclays na std chatered,ila deposit zake za mwezi ukimtuma statement ni robo page,anazunguka city centre na magazeti...
Kuna siku niko mishe zangu naenda bunju shamba,nkaingia sheri pale bamaga, mhudumu akaja ..niweke kiasi gani??nkamwambia mpaka ijae...akaguna ila akajaza, badae akashindwa kuvumilia,,eti bosi unaenda safari nini?nkamuuliza kwa nini>??eti mhh full tenki uku nadra sana/kawida ni buku 5, 20 au wakijipinda ni half tank//loading!nkajiuliza arusha watu wanavijivisima na na mapipa,...vijana kawaida tunatega pale town kucheza na madili,yasipotiki,gari inalala pale mango garden alaf njemba inakula public,,,wanajisemesha dah foleni siiwezi hii,aaah aahaah! Yani dar wakikata mafuta siku 3 gari zinakata wese barabarani, mara foleni ya madumu sheli,aah ahaa aah....wakikata wiki???

watu wana overdraft za b2 ,5 mpaka kumi wakati dar izo ni kwa ajili ya akina bakhresa!
Arusha ukiwa na lodge yenye rum 10 per day unaondoka na lak4 mpaka6, ukienda kwa manyanya pale unakuta gesti nzuriiii,chumba sh elfu20,25....mapipa pale self nyuma ya sea boys ni sh30 elfu full ac wakati kwa arusha icho chumba utapambana na mbu mpaka asubuhi. Digrii arusha kama pale ESAMI mil16 inapotea ila udsm chuo bora unasoma executive program kwa mil5???? kila mtu ana vigezo vyake vya ku evaluate maisha...dar unakuta mtu kala suti ila anaishi bunju ,mpaka jioni yuko pale city centre pale georges anavizia mzee flani agongee lift mpaka bunju,hapo sala kubwa ni mzee asimfiksi maana wazee wa mujini nao balaa tupu...arusha unakuta mhuni anauza jiwe pale mnara wa mwenge,amekula kipensi na sendo ila amepaki tx ya 2005,au range sports...wakati mission tauni akila timing anunuliwe mshikaki pale shibamu,hapo ni baada ya kufanya udalali na kuuza toyota vitz ya mteja ,hapo hapo anaulizia kwa cm kibaa chake cha tandika kimeingiza sh ngapi? dah nimeishi dar for 75% ya maisha yangu,arusha kama 5%ila naikubali arusha saaaaaana. Yani unakuta salary za vijana take hom usd 3000 na per diem kibao,nenda eac, un ,ictr...njoo dar iyo ni salary ya commissioner au jaji,nadeclare interst mimi ni lawyer na accountant ila unakuta departmental leader kama pale crdb mtu anakula take home 4m na housing loan ya 80m,uku govt salay za ajabu na kukimbiza na taakukuru eti hakima kapewa lak3???nenda pale exim viajan wamepaki ma bmw ,alaf teller/cashier...watu wanakimbilia kimara kununua ploti4m wanaenda bar kujisifia nina kiwanja sasa nasimamisha ghorofa mbili,,,uliza value ya ploti na value ya ardhi pamoja na mjengo!!!!!

Lori la mchanga tan12 arusha sh laki2 ulizia dar tegeta kwenda kinyerezi sh 120...sijui mwenzangu ubora wa maisha mnaupimaje???nenda aggrey pale kariakoo uone vijana wanaojisifia kwa mafanikio ni wale wenye vibanda vya simu kuuza housing na motherboard toka china,mtaji sh mil4 mkopo wa azania au akiba,kila siku afisa mikopo anaranda na makufuri .....dar darslama.

Dar ndo kwetu ila dah naadmire maendeleo ya arusha kuliko dar,,,watu wanaponda eti kuwa na chopa na kuchoma mbuzi waili watatu na vogue nje si ishu wakati dar vogue tu wanaendesha watu kichele,unaweza kukaa magomeni mataa masaa3 haijakatiza vogue, ni gx90,100,e100 navitz,arusha kila mtaa utaona range,Q7, nk. Acheni dharau jamani, nani dar anaenda kwenye shughuli za biashara zake na chopa kama si kumsikia kwenye redio bob sambeke anaenda shambani na chopa?dar ni wazungu au basi helikopta ya jeshi la kova...kuna siku kijihelikopta cha souther sun kimetua pale juu ya jengo,yani city centre ilizizima kupiga picha na kuload internet wakti hapa arusha watu wameegesha chopa,asubuhi wanaenda mashambani na jioni kurudi pale arusha port kuegesha, na hamna mwenye time...

Dar is good,kwa hasa civilized life, but for success si kivile. Uku arusha kukutana na escalade za mwale,ranges na nk ni kawaida si kama dar mpaka watu wanapiga picha. Ivi dar kama si akina masawe, msofe,nk wenye mafanikio ya utata , nani unamadmire anakula bata na ana investment za uakika,utasikia mengi,bahkresa,mohamed...wote hawa wapo mpaka mikoani,ww unataka dar tu.....utasubiri sana....

Lara1,Karibu arusha a land of suceess and bata kwa sana...uje ule mbuzi,samaki na kuku,si wale wa mlimani city wa plastic na wafugwao kwenye mabwawa bandia ya mbweni.!
Nawatakia usiku mwema bandugu.
 

Mie tena mchagga unaniambia ninni kuhusu A town. Mbuzi choma @ NDORO enzi hizo tumeteketeza sanaa, na kuku choma za wahindi pale town. Ila A town bado inapanga folleni kwa DSM, japo niliwahi kumuona Babu Sambeke (R.I.P) akidesposit 200m, standard chattered ya moshi town, na alikuja nazo kwa rambo! Daaaaaaaaah! Na kipensi chake na chini kobasi! Misha hayaaaaa! Hapo namngoja bi mkubwa achukue hela ya mboga! Hahahaaa!
 

kazi kwelikweli
 

Huko unakoita mikoani au shamba kutakuja kuwa mjini pia. Thanks to watu wanaovumilia kuishi shamba. Dar es salaam kulikuwa shamba pia, kipindi hicho sijui ungelidai kuwa utete ndio kila kitu kwenye fortress ya Dr. Kraph
 
Hii ni dalili nzuri kwamba watanzania wengi ni wa hapa hapa.Dar nini bhana!huku mikoani kuna wengi tu tena wafanyabiashara wa kawaida sana dili zao international.We jidanganye uje na sijui CPA yako hapa bila euro halafu udhani eti watu watakuheshimu,hiyo kitu haipo!Sana uanze kuibia wananchi tu halmashauri zetu,ama utoe mikopo benki kwa rushwa.Wapo wengi tu mikoani kwenda kla,Nairobi,Dubai ni kama kwenda kariakoo na posta tu hapo Dar.Tofauti ninayoiona sasa,kutokana na spirit kama hii hasa kwa wasomi waliosoma udsm,wengi wamekuwa majizi wa pesa za serikali na kurudi Dar kutambiana eti mnashindana maisha.Mipango mingi imekuwa ikikamua sana watu wa mikoani na kupelekea mapato mengi yabaki Dar.Siku mfumo mbaya wa uchumi uliopo ukivunjwa,wengi mtakuwa maharamia.Ukipima uelewa asilimia kubwa ya watu wa Dar hawajui kwa nini wanaishi,wengi wanadhani ni mashindano ya Olympic!kushindana uzinzi,kushindana ulevi,umaarufu,ujuaji(wakati hakuna lolote)wenyewe mnaita ujanja!Kushindana vyeti wakati wengine wanashindania elimu,kujifanya wazungu kumbe ni utumwa tu,kujiona mna akili na watu muhimu sana(dellusion of glandeur).Saw jifarijini.Muda unakuja,nao upo,mfumo utabadilika na umeanza kubadilika.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 

Ungekuwa Mzungu wewe! Kumbuka Industrial revolution, ndo uje na mibangi yako hapa!
 
lara 1 tutabanana hapa hapa, mi nilishajiwekea principal ya maisha.. Ili unitoe Dar es salaam lazima unilipe mshahara mara 5 ya nitaoweza kuupata Dar..

Lazima uzilipie opportunity cost zote nitazokosa nikiondoka Dar,,

Tukubali tukatae.. Kuna tofauti kubwa sana kati ya mikoani na Dar es salaam...

Mi mchuchu ni bank officer tu mkoa flani hivi maarufu lakini anavyoheshimika huko hadi unashangaaa..

Dar hata uwe CEO watu hawakutambui wanakuona mwehu tu, ukijenga ghorofa, jirani yako anajenga mansion, ukinunua Range sports unakuta mwenzako ana AUDI Q-7 ya 2013 lazima ufyate mkia...

Kuondoka Dar es salaam ni kama nimekubali kushindwa maisha kitu ambacho hakipo akilini.. Kama unajiamini we mkali njoo Dar es salaam ucheze CHAMPIONS LEAGUE NA BIG BOYS,,, kama Mikoani ni NBA season basi DAR ES SALAAM ni NBA PLAYOFFS...

Haushangai kila Head office inawekwa DAR hadi ya kampuni kama Barrick etc, maana yake Ma bosi wanataka wabaki town wa compete na big boys
 
Last edited by a moderator:
Kwa mara ya kwanza Lara 1 naomba kuunga mkono hoja yako 100%. Ingawaje hivi karibuni nilipokuwa Mkoani Kigoma na kupata bahati yakutembelea Wilaya ya Kibondo nilishangaa kukuta pale Wilayani Maafisa wengi wako bize wengine wakichukua Masters, wengine Uzamivu nk. Wameshtuka bhanaaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…