Sierra Leonne yapitisha sheria inayolazimisha mashirika ya umma na kibinafsi kuajiri wanawake kwa % 30

Sierra Leonne yapitisha sheria inayolazimisha mashirika ya umma na kibinafsi kuajiri wanawake kwa % 30

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Sierra Leone Alhamisi imepitisha sheria inayolazimisha mashirika ya umma na kibinafsi kutenga asilimia 30 ya kazi zao kwa ajili ya wanawake, katika juhudi za kukabiliana na ukosefu wa usawa wa kijinsia katika jamii inayopendelea wanaume.

Rais Julius Maada Bio alisaini mswada huo kuwa sheria, ambao pia unawahakikishia wanawake angalau wiki 14 za likizo ya uzazi, malipo sawa na fursa za mafunzo.

Bio amesema sheria hiyo “itashughulikia ipasavyo ukosefu wa usawa wa kijinsia katika nchi hii. Tunapaswa kuhakikisha kuwa inafanya kazi.”

“Lazima tukomeshe tabia ya kutoadhibu ukatili dhidi ya wanawake katika uchaguzi na maisha ya umma na kuwaadhibu watu wote na mashirika yanayopatikana na hatia ya ukatili kama huo,” aliongeza.

Wanawake nchini Sierra Leonne wanakabiliwa na ubaguzi wa kimfumo, na kulingana na shirika la kutetea haki za binadamu Human Rights Watch, imekuwa ni jambo la kawaida kuwafuta kazi wanawake kama watapata ujauzito.

Wanawake wengi na wasichana wanakabiliwa pia na viwango vya juu ya ukatili wa kingono, kutokana hasa na tabia ya kutumia ubakaji kama silaha wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vya mwaka wa 1991 hadi 2002.

Sheria hiyo mpya inalenga pia kuboresha mfumo wa kutoa mikopo kwa wanawake katika nchi ambapo wamekuwa hawapati kabisa mikopo.

&&&&&&&&&&&&&


Sierra Leone passes law reserving 30% of positions in public, private sectors for women

The law, called the Gender Equality and Women’s Empowerment Act, was signed by President Julius Maada Bio on Thursday.

According to Bloomberg, the act mandates 30 percent of seats in parliament and cabinet reserved for women.

It also requires companies to set aside 30 percent of senior-level jobs for women, with equal pay and at least 14 weeks of maternity leave.

The law seeks to increase the number of women in decision-making roles in both private and public sectors.

Employers who fail to meet the quota risk a fine of at least 50,000 new leones ($2,580), and jail sentences of at least three years for denying equal financial support.

In a post on Twitter, the Sierra Leone president, who is running for a second and final five-year term in office, described the law as “a real change”.

“Today, Thursday, January 19 2023, I signed into law The Gender Equality and Women’s Empowerment (GEWE) ACT 2022. REAL CHANGE has been ushered into our great nation,” he wrote.

“The Bill will also revolutionise our government’s engagement with WOMEN – making them equal partners in our task to build a strong and vibrant country. Thank you to ALL stakeholders for the actualisation of this landmark ACT. Women’s rights are Human rights.”

Bio has reportedly named just four women to his 28-member cabinet since he first took office in 2018.

Source: Thecable
 
Kwahyo hakuna tena kuangalia uwezo inimladi ww mwanamke
 
Back
Top Bottom