doctor mwanafunzi
Member
- Jun 16, 2024
- 45
- 56
Uvutaji wa sigara hadharani umekuwa kero kubwa sana mitaani na katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu kama vile vituo vya daladala na baadhi ya maduka ya rejareja.
Ikumbukwe kuwa sigara ni hatari zaidi kwa asiyetumia (second-hand smoker), yaani yule ambaye ametulia zake mara ghafla moshi wa sigara unampitia pale alipo.
Wauza maduka nao wamekuwa na utaratibu mbaya sana kwani wanatundika kibiriti au lighter kwenye maduka yao, hivyo mvuta sigara anawashia pale dukani na wakati mwingine kuna wamama na watoto wadogo.
Ushauri: Tustaarabike. Kama unavuta sana sigara, kajifungie chumbani ili upate moshi wote wewe mwenyewe au nenda sehemu ambazo hazina watu.
Na wauza maduka mnaotundika viwashio (kibiriti au lighter), tafuteni utaratibu mwingine.
Nchi za wenzetu kuna maeneo maalum ya kuvutia sigara.
Ni kwa sababu wanaelewa vitu hivi vina madhara, siyo kwa mvutaji tu. Sigara inaweza kusababisha kansa ya mapafu (lung cancer) baada ya kutumia kwa muda mrefu.
Ikumbukwe kuwa sigara ni hatari zaidi kwa asiyetumia (second-hand smoker), yaani yule ambaye ametulia zake mara ghafla moshi wa sigara unampitia pale alipo.
Wauza maduka nao wamekuwa na utaratibu mbaya sana kwani wanatundika kibiriti au lighter kwenye maduka yao, hivyo mvuta sigara anawashia pale dukani na wakati mwingine kuna wamama na watoto wadogo.
Ushauri: Tustaarabike. Kama unavuta sana sigara, kajifungie chumbani ili upate moshi wote wewe mwenyewe au nenda sehemu ambazo hazina watu.
Na wauza maduka mnaotundika viwashio (kibiriti au lighter), tafuteni utaratibu mwingine.
Nchi za wenzetu kuna maeneo maalum ya kuvutia sigara.
Ni kwa sababu wanaelewa vitu hivi vina madhara, siyo kwa mvutaji tu. Sigara inaweza kusababisha kansa ya mapafu (lung cancer) baada ya kutumia kwa muda mrefu.