mukama talemwa
Senior Member
- Jun 14, 2011
- 160
- 29
Tangia kampuni ya sigara tanzania imepata mkuruzenzi mpya wa masoko na mauzo mtanzania baada ya kuondoka Mkenya kulizuka wimbi la kufukuza wafanyakazi,mkurugenzi huyu mtanzania alianza na kuahakikisha anafukuza wafanyakazi woote watawi la Shinyanga ambao walikuwa siyo rafiki wake,alifukuza wafanyakazi saba wakiwemo viongozi wote wa tawi nawoote waliokuwa wanahusika na mauzo ila akahakikisha aliyekuwa cashier ambaye watoka mkoa mmoja anabaki kazini.Tawi la Mwanza akafukuza wafanyakazi watatu na matawi mengine akahakikisha ambao hawataki wanafukuzwa kazi.Wote waliofukuzwa kazi walifungua kesi CMA na wote walishinda maana wote walifukuzwa kwa hila tu,lakini Mkurugenzi huyoaliwa agiza wanasheria wakate rufaa&Mahakama kuu,Rufaa zimekatwa ila kitu chakufurahisha au kusikitisha upande mwingine Kesi zote zilizotolewa maamuzi na Mahakama kuu zimewataka Sigara kuwarudisha kazini wafanyakazi wote na kuwalipa mishahara pamoja na marupurupu yao yote tangu walipofukuzwa kwa kounewa.Kesi iliyotolewa maamuzi jana ni ISSA NZILAIWE nayeye Mahakama imeamuru arudishwe kazini,miezi miwili iliyopita wale washinyanga nawenyewe Mahakama iliamuru warudishwe kazizi,mwezi mmoja uliopita Mahakama ilamuru mfanyakazi mwingine aitwaye AGGREY GOMBANILA arudishwe kazini ni aibu kwa kitengo cha sheria cha kampuni na ni aibu kubwa kwa mkurugenzi ambaye hadi sasa hizi ameisha isababishia hasara kubwa Kampuni kuendesha kesi zisizokuwa na tija pamoja na kulipwa watu bila kuwafanyia kazi Kampuni.Mie nilinunua hisa katika kampuni hii za shilingi milioni tatu,nimfanyakazi bado katika kampuni hii kwahiyo kitendo cha kutumia pesa zetu wana hisa bila tija yoyote nikitu ambacho hakikubaliki kabisa.
Wataalam wa sheria tusaidie tufanyenye wanahisa kudhibiti utumiaji holela wa pesa zetu?
Wataalam wa sheria tusaidie tufanyenye wanahisa kudhibiti utumiaji holela wa pesa zetu?