Sijajutia kabisa safari yangu ya Morogoro kuangalia maeneo (ardhi) ya uwekezaji

Sijajutia kabisa safari yangu ya Morogoro kuangalia maeneo (ardhi) ya uwekezaji

Wachawi wala awasumbui kama una jua code wewe ni kuwakamata wazee ilo limeisha . Kuna sehemu tulikuwa na mradi mkubwa wa kilimo wakawa wamekausha bwawa la maji ikabidi tuwaibukie wazee wakafanya yao na kuchinja ngombe na wakawatahadhalisha kuwa wazee wametoa baraka zote asije akajaribu mtu yoyote kuleta mchezo baadae maji yakaludi bwawa lote likafilika na kilimo kinaendelea hadi leo
Shida ya vijana wenzatu wakienda kwenye maeneo ya watu wanakuwa na element zilezile za mjini. Wakati ukifika huko Kwa watu kituo Cha kwanza ni kwenye uongozi katika huo uongozi hukoswi wazee kamwe jioni waombe uwatoe hata kama kilabuni au bar au kwenye kijiwe nunua pombe wanywe ama kahawa Hadi wakimbie. Halafu waachie na 5000 Kila mmoja Kazi kwisha. Jambo lolote ukiwafata hata Hela hawakuombi Tena!
 
Wachawi wala awasumbui kama una jua code wewe ni kuwakamata wazee ilo limeisha . Kuna sehemu tulikuwa na mradi mkubwa wa kilimo wakawa wamekausha bwawa la maji ikabidi tuwaibukie wazee wakafanya yao na kuchinja ngombe na wakawatahadhalisha kuwa wazee wametoa baraka zote asije akajaribu mtu yoyote kuleta mchezo baadae maji yakaludi bwawa lote likafilika na kilimo kinaendelea hadi leo
Aiseeeeh sijui kwa kule maana hata wao kwa wao wanaogopana
 
Shida ya vijana wenzatu wakienda kwenye maeneo ya watu wanakuwa na element zilezile za mjini. Wakati ukifika huko Kwa watu kituo Cha kwanza ni kwenye uongozi katika huo uongozi hukoswi wazee kamwe jioni waombe uwatoe hata kama kilabuni au bar au kwenye kijiwe nunua pombe wanywe ama kahawa Hadi wakimbie. Halafu waachie na 5000 Kila mmoja Kazi kwisha. Jambo lolote ukiwafata hata Hela hawakuombi Tena!
Ni kweli kabisa heshima aikuondolei chochote katika maisha haya. Wazee wa muhimu kuwaona .
 
Katika Maisha yangu natamani niishi Morogoro Vijijini, kazi ninayotamani ni Kilimo na Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji tu.

Naamini nitatoboa, ni vile mambo bado hayajakaa sawa.

Kwa kifupi umenipa ramani halisi ya Kile natamani
Ukipata hela nenda nunua mapema zaidi maana siku hizi usafiri wa SGR umerahisisha mambo unaenda na kurudi fasta. Kuoshi huko imekuwa rahisi zaidi ukiweka mikakati yako vizuri mzee
 
Wakati mwingine uje na Kilosa nikutembeze vijijini ujionee fursa za wazi kuanzia:-
Dumila na mateteni-kilimo Cha Nyanya
Kilangali, Tindiga, Kivungu- Kilimo Cha mpunga
Zombo, Ulaya-kilimo Cha mahindi
Lumuma, Pwaga, Mnozi, Ruaha mbuyuni, Kitati, Kidete n.k - kilimo Cha vitunguu na Mahindi

Sehemu zote hizo mazao mchanganyiko kama mbaazi, ufuta, kunde, maharage, alizeti n.k yanalimwa sana pia ufugaji wa kuku, Bata, kanga, mbuzi, nguruwe, Ng'ombe, punda n.k

Karibu Kilosa
Mwezi wa 4 nilikuwa pwaga, sikuina fursa nilikuwa na kama 40M nilirudi nazo town
 
umetisha sana mzee, umenikumbuka mwaka 2022 nilifanyanga hii tour nilianziaga mang'ula mpaka ifakara, nilibadili mawazo yangu kabisa kuishi dar nilikutana na utajiri mkubwa sana, nilinunuaga mashamba ya kutosha, eneo la kiegea, nikarudi dar najichangachanga mambo yakiwa safi narudi zangu , term hii tuliani nikajichimbie huko,
 
Back
Top Bottom