Megalodon
JF-Expert Member
- Apr 9, 2021
- 3,534
- 7,866
Simba ya sasa ni bora, na tuseme kuwa Yanga ikajipange.
magoli kama yale ni kweli Manula anaugonjwa nayo, hata Morrison alimfunga sana Manula kwa mtindo ule, lakini haindoi uhalisia kuwa bado ni golikipa bora.
Mgunda amefanya mageuzi makubwa ya klabu yetu pendwa na kurudisha tumaini ambalo liliondolewa na makocha wa kigeni wasioelewa Chemistry ya soka letu.
Nafasi ya Juma kushinda huu mchezo ilikuwa ni zaidi ya 60%, changamoto ya Dabi inaenda na presha hivyo utulivu unakuwa hafifu. Hongereni simba kwa soka bora, siyo lazima kila mechi ushinde, kupiga kandanda ya kujiamini inatia moyo.
Ninaamini Mgunda anacheza nusu fainali CAF, kumbuka maneno yangu.
Katika kufanya motisha ya makocha wa kizawa, SSC waache mbambambamba na wamtangaze Juma kama Kocha Mkuu haraka sana.
Mshahara wa Kocha Mkuu SSC si chini ya mil. 25 pamoja na benefits zote kama Kocha Mkuu ikiwa ni pamoja na kumpatia makazi tena Masaki au Oysterbay na usafiri binafsi kama jinsi ambavyo makocha wa kigeni hupewa hizo huduma.
Hii pia itatengeneza career path nzuri na motisha kwa makocha wengine wa ndani.
SSC na Yanga, kabla hamjaanza kuhangaika na makocha wa nje angalieni kwanza ndani, achaneni na mambo ya uzoefu, toeni uzoefu kwa kuwajenga makocha wa ndani ambao kwa asilimia kubwa watakuwa na uelewa mkubwa wa soka la Afrika na kujua hitaji la mashabiki.
Yanga huu mchezo ilikuwa tuwapige nyingi, ni presha tu ya Dabi, lakini huu mchezo leo ilikuwa tuwapige hata tatu.
Mjipime upya, maana kuna uwezekano mkubwa hata makundi ya shirikisho msicheze, siamini na sitokuja kuamini kama mtaweza kuwatoa Africa Club. Maana ile timu inapambana na timu kama Widady na Raja.
Huyu Nabi sasa anaenda kujaribiwa kwa mara ya pili, na safari yake ya makundi itaishia Tunisia, ndiyo mtajua kuwa kumbe shirikisho siyo ya maloser, na kuna haja ya kukukuza vipaji vya ndani.
Na nyie makocha wa ndani anzeni kujiamini na kujiongeza kielimu.
magoli kama yale ni kweli Manula anaugonjwa nayo, hata Morrison alimfunga sana Manula kwa mtindo ule, lakini haindoi uhalisia kuwa bado ni golikipa bora.
Mgunda amefanya mageuzi makubwa ya klabu yetu pendwa na kurudisha tumaini ambalo liliondolewa na makocha wa kigeni wasioelewa Chemistry ya soka letu.
Nafasi ya Juma kushinda huu mchezo ilikuwa ni zaidi ya 60%, changamoto ya Dabi inaenda na presha hivyo utulivu unakuwa hafifu. Hongereni simba kwa soka bora, siyo lazima kila mechi ushinde, kupiga kandanda ya kujiamini inatia moyo.
Ninaamini Mgunda anacheza nusu fainali CAF, kumbuka maneno yangu.
Katika kufanya motisha ya makocha wa kizawa, SSC waache mbambambamba na wamtangaze Juma kama Kocha Mkuu haraka sana.
Mshahara wa Kocha Mkuu SSC si chini ya mil. 25 pamoja na benefits zote kama Kocha Mkuu ikiwa ni pamoja na kumpatia makazi tena Masaki au Oysterbay na usafiri binafsi kama jinsi ambavyo makocha wa kigeni hupewa hizo huduma.
Hii pia itatengeneza career path nzuri na motisha kwa makocha wengine wa ndani.
SSC na Yanga, kabla hamjaanza kuhangaika na makocha wa nje angalieni kwanza ndani, achaneni na mambo ya uzoefu, toeni uzoefu kwa kuwajenga makocha wa ndani ambao kwa asilimia kubwa watakuwa na uelewa mkubwa wa soka la Afrika na kujua hitaji la mashabiki.
Yanga huu mchezo ilikuwa tuwapige nyingi, ni presha tu ya Dabi, lakini huu mchezo leo ilikuwa tuwapige hata tatu.
Mjipime upya, maana kuna uwezekano mkubwa hata makundi ya shirikisho msicheze, siamini na sitokuja kuamini kama mtaweza kuwatoa Africa Club. Maana ile timu inapambana na timu kama Widady na Raja.
Huyu Nabi sasa anaenda kujaribiwa kwa mara ya pili, na safari yake ya makundi itaishia Tunisia, ndiyo mtajua kuwa kumbe shirikisho siyo ya maloser, na kuna haja ya kukukuza vipaji vya ndani.
Na nyie makocha wa ndani anzeni kujiamini na kujiongeza kielimu.