Pre GE2025 Sijawahi kumsikia Mbunge wa jimbo langu Orani Manase Njenza, wa Mbeya vijijini akiuliza swali hata kuchangia hoja Bungeni

Pre GE2025 Sijawahi kumsikia Mbunge wa jimbo langu Orani Manase Njenza, wa Mbeya vijijini akiuliza swali hata kuchangia hoja Bungeni

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kote si Mbeya au ulitaka awe na kiherehere mbele ya mkubwa wake wa kazi then ionekane mbeya vijijini ni ya moto kuliko mbeya mjini..
Majimbo yote yana haki sawa, haijalishi mbunge wake ni nani wananchi tunataka maendeleo
 
Aulize nini?
Wakati kila kitu kinafanywa na mbunge wa mbeya mjini.
Mbunge wa Mbeya Mjini mwisho wake ni Uyole, Iwambi na Kawetere.

Mbeya Vijijini ni kubwa mno, acha kupotosha na kumfagilia Bi Kidude wenu
 
hakuna alilofanya
Kujuwa alichofanya Mbunge Oran Njeza ni mpaka uwe na akili kichwani. Kwa namna ya uandishi wako na uwasilishaji mada wako, yaonekana wewe ni tabula rasa.
 
Huyu mbunge Orani Manase Njenza yupo bungeni tangu 2015 mpaka sasa na sijawahi kumsikia akizungumza bungeni, iwe kuuliza swali au kuchangia hoja licha ya jimbo lake kuwa na mzigo wa kero.

wabunge wa aina hii hawatufai hawana msaada kwa wananchi.

Mdau vipi wewe mbunge wa jimbo lako anakuwakilisha ipasavyo?


Soma: Kwanini Mbunge Job Ndugai huwa hachangii chochote bungeni?
Takwimu rasmi za Bunge hizi hapa kutoka kwenye tovuti yao:

Screenshot_20241105_094107_Chrome.jpg
Amechangia mara 123, ameuliza maswali 119 na ni mjumbe wa Kamati za Bunge.

Unataka afanye nini zaidi ya hayo?
 

kama unasubiri kumsikia kupitia millard Ayo na ITV utasubiri sana.Hili jamvi lina vilaza sana kwa sasa yaani pamoja na U-Gen Z unashindwa kufuatilia vitu kutoka vyanzo sahihi kabla ya kuja na hoja ya kupost.

Kwa hakika naona athari ya kuondosha viboko shuleni
Kaanza kampeni kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao 2025 anaye mtu anayemtaka kuwa mbunge wa jimbo lao, kaamua kwanza kumchafua huyo aliyepo hivi sasa.
 
Kama alipita bila kupingwa ni makosa yenu wana jimbo!
 
Ameleta maendeleo?
Kero haziwezi kuisha coz kila siku watu wanazaliana na mahitaji yanaongezeka.
Kuongea bungeni siyo njia pekee ya kutatua kero za wananchi.
Fuatilia Hansard za bunge labda anawasikisha hoja zake kwa maandishi.
Tunaelekea uchaguzi ni vizuri kumtathimin kwa kina mgombea wako kabla ya kumchagua.
 
Mbunge wa Mbeya Mjini mwisho wake ni Uyole, Iwambi na Kawetere.

Mbeya Vijijini ni kubwa mno, acha kupotosha na kumfagilia Bi Kidude wenu
Acha hasira mkuu
Uyo ni mbunge wa mabunge ya dunia kumbuka.
 
Acha hasira mkuu
Uyo ni mbunge wa mabunge ya dunia kumbuka.
Mabunge ya dunia yako wapi? IPU haina maamuzi yoyote dhidi ya nchi yeyote. Ile ni club tu sawa na Mabatini Veteran FC. Inacheza kupasha misuli lakini haishiriki ligi yeyote.

Mabwege mnadanganywa na Betina mkidhani ana cheo cha maana
 
Back
Top Bottom