Sijawahi kuona vijana wa Mzumbe na Ardhi wakifa njaa mtaani

AdvocateFi

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2012
Posts
11,492
Reaction score
5,047
Shalom makamanda!

Mbali ya kuwa na changamoto za ukosefu wa ajira na kushuhudia wimbi la vijana wakizunguka na bahasha mitaani,

Lakini hali ni tofauti hasa kwa vijana waliomaliza vyuo vya Mzumbe ( Military university) na Ardhi University wakifa njaa mtaani, hii inatokana na utija wa kozi zinazotolewa kwenye vyuo hivyo pamoja na kuwaandaa vijana vizuri katika soko la ushindani wa ajira.

Kiufupi mwanafunzi yeyote anayepata Neema ya kusoma vyuo hivyo katika kozi yeyote ana haki ya kujiita mwenye bahati sana.
 
bado ujana unakusumbua.
 
Ha ha ha. Kwani umewaona wa UD wanakufa njaa? Hao ndio vijana wanaoongoza kumiliki Altezza na IST hapa mujini. Pia ni vijana wanaoongoza kwa kumiliki Smart fone za maana zile za S5, Iphone 5.

Mujini huwaoni vijana wa Mzumbe na Ardhi kwa kuwa hawapo. Wanafia njaa kijijini kusiko na mwandishi wa habari wa kuripoti njaa na vifo vyao...

Just jokin wakuuu!
 
mdogo wangu ame maliza mzumbe 2011, mpaka sasa yupo mtaani tu, na ana upper second, ameamuwa kusoma masters lakini haikusaidia, bado yupo mtaani.

Tatizo la ajira tanzania ni kubwa sana.
 
Vipi waliobahatika kusoma vyuo vya nje ya tz, wanakufa njaa?.

ila msisahau, vijana wanaozungumza kwa ufasaha lugha ya kizungu, hata kama hawakusoma mzumbe na UDSM, ni nadra sana kukuta wanalia njaa.

Wengi wao wana confidence ya kuingia wao wenyewe front (bila kusubiri tangazo la kazi) ofisi ya shrika/kampuni yoyote kuomba apointment na CEO ili kueleza idea/shida zao na huwa wanafanikiwa.

Nimelishudia hili kwa rafiki zangu watatu waliosomea nje ya nchi.

Ni ukweli mchungu japo unauma.
 

Ifikie kipindi nyie wasomi mtumie akili kuleta vitu vyenye research kwa mtu aliepita shule na kuzijua degree programme za MZUMBE atakubaliana na Mimi kuwa kilichoandikwa na mleta mada ni ushabiki yaani MZUMBE chuo kinachotoa wahitimu dhaifu na course zao ambazo zimetapakaa kila chuo hapa nchini afu anataka kutuaminisha uongo kwa ardhi nakubali ila sio mzumbe
 

Mkuu acha utani aisee, Vijana wa UDSM wana njaa kali mjini hapa kila siku wanatemwa kwenye interview hadi huruma.
 
mdogo wangu ame maliza mzumbe 2011, mpaka sasa yupo mtaani tu, na ana upper second, ameamuwa kusoma masters lakini haikusaidia, bado yupo mtaani..
tatizo la ajira tanzania ni kubwa sana.

Mkuu nina mashaka na habari hii, Hakuna kijana aliyesoma Mzumbe akalia lia njaa, sababu ntaleta badae.
 

Mkuu naona unaongea usichokijua, Chuo cha mzumbe kimebobea kwenye fani kama za utawala na usimamizi, uhasibu.
 

Mkuu hao pia ni waganga njaa mjini hakuna ukweli wowote hapo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…