Sijawahi kuwa na rafiki wa kudumu

Sijawahi kuwa na rafiki wa kudumu

Hivi kuna watu humu wapo kama mimi? Mimi bhana katika maisha yangu sijawahi kuwa na rafiki wa kudumu eti niseme huyu nilicheza nae, nilisoma nae shule ya msingi au secondary alaf mpaka sasa tunawasiliana.

Katika kila hatua ya maisha yangu nakua na marafiki ambao naelewana nao vizuri, ila hiyo hatua ikiisha tu na urafiki unaishia hapo. Kunakua hakuna mwendelezo wa urafiki wetu.

Ata nikihama kazi wale watu ambao nilifanya nao kazi pamoja ndo inakua imeishia hapo hakuna mwemdelezo.

Sina tabia ya kujiattach kwa mtu mpaka ile mtu anizoee kupitiliza. Mtaani wananiita usalama wa taifa 😂😂 Nimejikuta tu nawaza hivi kuna watu wapo kama mimi nataka nianzishe chama letu chama la wana 😂
Changamoto kubwa iliyopo siku hizi ni kwamba mtu unayetamani awe rafiki yako wa kudumu naye ana rafiki yake...kwahyo anashindwa ku-balance vitu Fulani....umbea, majungu, masengenyo anashindwa kuviepuka...nadhani Kwa sasa rafiki yangu Mimi binafsi ni SIMU yangu ya mkononi tu..
 
Rafiki yangu wa kweli ni huyu kati kati ya meza
 

Attachments

  • Screenshot_20241202_210519.jpg
    Screenshot_20241202_210519.jpg
    233.9 KB · Views: 4
Si kweli,

Bila mawasiliano na kuonana urafiki hupungua na kufa. Leo unaweza ukakutana na rafiki wa utotoni mkajikuta hata hamna story kivile

Ila utashangaa mfanyakazi mwenzake yuko karibu naye kuliko wewe mliyetoka mbali
Nadhani tunatofautiana mitizamo, mimi napenda sana ukaribu na watu, bt hua sipendi mazoea, coz mazoea huondoa kuheshimiana na kusababisha changamoto zisolazima.
 
Mazoea ndiyo nini kwenye urafiki?
Kutokua na mipaka, wengi hudhani ukiwa na urafiki na mtu ni sahih kumweleza kila kitu, jambo ambalo badae huleta changamoto, hasa pale utakapoyasikia kwingine, baadhi ya mambo ambayo ulimweleza rafiki yako.
 
Back
Top Bottom