Sijui kwanini nimeumia hivi

Sijui kwanini nimeumia hivi

Nilivyokua nasoma nilikua nahisi kuna kibaya kimewakuta hospitalini kumbe alipona mtoto na kuruhusiwa, nimeshukuru kwa hilo.

My dear binadamu hatuma wema, binadamu ni wasahaulifu, binadamu tuna wivu na tuna visasi.
Huwezi jua kuna kitu hakikuwa sawa kati yenu mlivyokuwa mnasoma akaweka chuki nawe na alipopata nafasi ya wewe nawe kuumia akaitumia, ni dhana tu lakini.

Yote ya yote jana imepita achana nayo tungojee kesho.
 
Misaada ya kujitoa kwa kujiteketeza mara nyingi huambatana na maumivi.
Ni mara chache mno mtoa msaada wa kujiteketeza akapewa shukran aliyoitegemea toka kwa msaidiwa.

Saidia kile una uwezo nacho, sipendi kujitoa kumsaidia mtu end of the day nikaja kuumia kama hivyo.

Unamsaidia kumbe anakudanganya, msaada wako anautumia kinamna nyingine tofauti na alivyokuomba.
 
Mimi nimekuelewa Sana mleta mada
Kuna binadamu ukisaidiwa hata kidogo hutoa shukrani hata ya mdomo just neno "asante" inafariji na inakupa moyo kwamba ametambua msaada wako Ila kwa hiki kizazi hasa hawa viumbe wa kike hawana huo moyo!
Kuna dada mmoja nlimkuta njiani mvua kubwa inanyesha nikasimamisha kigari changu(kama cha Mr Bean) nikampa lift japo alikuwa keshaanza kuloa na mvua nikamchukua mpaka mtaa anaokwenda nikamshusha lakini cha ajabu hata neno asante hakuna yaani anashuka anashika simu yake na kumpigia mtu kwamba ndo anashuka kwenye "bajaji"😀
Kisha akatokomea uchochoroni akiendelea kuongea na simu hata hakuniaga yaani nilijiskia vibaya Sana nikajilaumu kumpa lift na kuacha njia yangu kumpitisha huku anakoelekea
Mie nadhani malezi ya siku hizi ndo chanzo mtoto tangu akiwa mdogo hajafundishwa kusema samahani anapokosea na hajui kusema Asante anapopewa kitu
Wanaitwa ENTITLED KIDS walifundishwa kuwa ni haki yao kupewa kika kitu walichoomba badala ya ni hisani.

Hivyo kushukuru inakuwa nadra
 
Habari za asubuhi wana JF,

Iko hivi, nina rafiki yangu ana mtoto (naweza nikasema ni single mom) ila isieleweke vibaya, nilisomaga nae O level huko ila nikama bahati tu tumejikuta tunaishi tena mtaa mmoja.

Ijumaa jioni wakati natoka tu ofisini alinipigia Simu akaniambia anashida kama naweza nipitie nyumbani kwao nikamuone, kwakua nilikua sina ratiba nyingine nikasema isiwe tabu kabla sijafika nyumbani nikapitia.

Nilimkuta yuko good ila mwanaye alikua anaumwa sana ile mtoto kazidiwa na akaniambia ameshindwa kwenda hospitali hana hela na almost kila aliyempigia simu wamemuahidi tu tangu asubuhi na hakuna aliyemtumia mpaka muda huo sa 1 jioni inaelekea saa 2.

Kiukweli sikua na hela and i was totally broke, yaani wiki ile iliyoisha mwenyewe nimeishi tu kwasababu nina wazazi maana nilikua nina mambo mengi yananihitaji hela kiasi kwamba sikua nimebakiwa na hata Mia mbovu. Lakini nikasema kwenye suala la kuokoa maisha ya mtoto isiwe kesi nikamwambia ngoja nirudi kwanza nyumbani, nikamsimulia mama tukaongea na dada yangu wakasema tu hapa kwa harakaharaka hatuna namna tumdanganye tu mzee kitu chochote jioni hii atupe hela, kweli tukamshawishi mzee bila hiyana akanipa 150k nikamfata kwao tukaenda hospitali usiku uleule.

Mtoto akapewa huduma ya kwanza na baadhi ya vipimo wakamlaza ili asubuhi aendelee na matibabu mengine (muda wote huo anawapigia ndugu zake wakiwemo na baba wa mtoto hata simu hawampokelei wengine), asubuhi yake niliomba tu ruhusa kazini nikawaambia nitachelewa ili nione mtoto atakua anaendeleaje.

Case ya mtoto ikawa kubwa wakasema tuende nae hospitali nyingine kubwa (Peramiho nadhani watu wa songea wanaijua), kuna vipimo alivyoambiwa wampime vilikua vinahitaji hela almost kama laki 2 tena nikamwambia mama akanitumia tukafanikisha. Kwasababu kazini walikua wanapigapiga sana simu na nikaona wanaendelea vizuri na mama yake alikua ashafika nikamwambia naenda ofisini incase kimetokea chochote utatuambia nikampa na namba ya mama kama mimi nisipopokea ampigie, nikaondoka. The bad thing is nilikua busy busy sana hadi siku ikaisha sikuwatafuta tena.

Kinachoniumiza ni kwamba, jana mchana nilimpigia simu hakupokea nikaenda kwao sikukuta mtu, nikaenda hadi Peramiho tena kulivyo mbali nikaambiwa wameruhusiwa na hakunipa taarifa. Kuanzia jioni nimeingia WhatsApp naona ameweka status nyingi nyingi kufungua nikawa naona amescreenshot miamala yote ya watu waliokua wanamtuma hela na kuwapa credits Mungu awabariki sana kwa kuokoa maisha ya mwanae maana alikua kwenye hali mbaya sana na nini nini. Screenshot kama kumi hivi na kitu na amewataja na majina kabisa...

Cha ajabu hiyo miamala hakuna hata wa mtu mmoja uliofikia hata 30k, wote ni hizo hizo tu efu10 ef5 ef7, kawaandikia macaption mazito mazito. Nimebaki najiuliza mbona alikua ananiambia hawapokei simu, na hela inaonekana walimtumia siku ileile ambayo aliniambja na mimi niende kwake kumuona.

Mimi ambaye nilikua nae kuanzia siku ile hadi usiku nikaacha na kwenda kazini na tumeclear bills zote hata asante hajaniambia na wala taarifa kama wameruhusiwa hajanipa. Nimesubiri jana yote hadi leo saizi hajanipigia hata simu, Kina mama wananiuliza wanaendeaje nawaambia tu wanaendelea vizuri huku roho inauma.

Nimetenda wema nimeenda zangu wakuu, lakini bado roho inaniuma aisee😥😥
umefanya ukarimu kwa tendo la huruma la kipekee sana mkuu,

usiumie sana, ndivyo walimwengu tulivyo.
angekukumbuka zaidi, kama ungemtumia muamala kwenye simu au ungempa cash mkononi.

wema wako umekuponza,

kujitolea muda, fedha na hasara ambayo ungeipata kazini kwako kabisa hajaithamini 🐒

Tenda wema uende Zako..
Kwa Neema na Baraka za Mungu, wema na ukarimu wako Mungu ameuona 🐒
 
Ni jambo jema sana.. Nimejifunza in a hard way
Kila binadamu anapenda appreciation pale anapofanya jambo jema. Ila sasa sisi sisi binadamu pia ni very complex creatures, tuna tabia na malezi/makuzi tofauti tofauti pia.

Ndio ukubwa huo mama, tunajifunza kila siku.
 
Nilivyokua nasoma nilikua nahisi kuna kibaya kimewakuta hospitalini kumbe alipona mtoto na kuruhusiwa, nimeshukuru kwa hilo.

My dear binadamu hatuma wema, binadamu ni wasahaulifu, binadamu tuna wivu na tuna visasi.
Huwezi jua kuna kitu hakikuwa sawa kati yenu mlivyokuwa mnasoma akaweka chuki nawe na alipopata nafasi ya wewe nawe kuumia akaitumia, ni dhana tu lakini.

Yote ya yote jana imepita achana nayo tungojee kesho.
Kwakweli nashukuru Mungu kwa hilo pia
 
Misaada ya kujitoa kwa kujiteketeza mara nyingi huambatana na maumivi.
Ni mara chache mno mtoa msaada wa kujiteketeza akapewa shukran aliyoitegemea toka kwa msaidiwa.

Saidia kile una uwezo nacho, sipendi kujitoa kumsaidia mtu end of the day nikaja kuumia kama hivyo.

Unamsaidia kumbe anakudanganya, msaada wako anautumia kinamna nyingine tofauti na alivyokuomba.
kwakweli nimeliona hilo, nimejifunza kitu kikubwa sana
 
Ukieza kuhandle hizo reaction automatically na huruma inapungua tukio la huyo mate wake limempa introduction tu ya jinsi binadamu walivyo
Huruma isipungue bhana , unajua msaidie mtu kama umeguswa na anayo yapitia kwa kujipa amani yako ww mwenyewe kwa kuona angalau ule ugumu kwa huyo mtu umepungua , bila kuweka matarajio ya malipo ya aina yoyote kutoka kwa yule mtu , matarajio ndio yana waumiza watu pale yanapokwenda kinyume .
 
umefanya ukarimu kwa tendo la huruma la kipekee sana mkuu,

usiumie sana, ndivyo walimwengu tulivyo.
angekukumbuka zaidi, kama ungemtumia muamala kwenye simu au ungempa cash mkononi.

wema wako umekuponza,

kujitolea muda, fedha na hasara ambayo ungeipata kazini kwako kabisa hajaithamini 🐒

Tenda wema uende Zako..
Kwa Neema na Baraka za Mungu, wema na ukarimu wako Mungu ameuona 🐒
Amen🙏
 
Kuna watu wana roho za tofauti sana na huyo shoga ako ana tabia za kiswahili. Ndio umeumia sana lakini overtime utakua sawa.

Cha kufanya delete namba yake akikutafuta muulize yeye nani. Mpotezee mazima hafai kabisa. Amekuona wewe ndio chuma ulete wake

Binafsi nimefurahi.

Sikujua kumbe na nyie wanawake mnaumiaga mkifanywa chuma ulete.

Mwanaume akija kulalamika humu kafanywa chuma ulete na mdada, mnamponda mwanaume kuwa hana hela, wanaume wa jf tunanalalamika sana, tunakimbia majukumu, tule kwa jasho etc , mnamtetea mdada aliemchuna uyo mwanaume.

Itabidi mjue how it feels like, mtu ukijua kwamba ulikuwa used.

Ndo mpate taste ya sisi wanaume tunavojisikia Leejay49 Mrs Van
 
Kila binadamu anapenda appreciation pale anapofanya jambo jema. Ila sasa sisi sisi binadamu pia ni very complex creatures, tuna tabia na malezi/makuzi tofauti tofauti pia.

Ndio ukubwa huo mama, tunajifunza kila siku.
Ni kweli, ila walau nimepata ahueni baada ya kusoma comments zenu.. Mbarikiwe sana
 
Amen🙏🙏.. Nitafanya hivyo nikipata nafasi, Barikiwa sana mkuu
Pia nataka nikuambie Leejay49 unajisikia vibaya ni kibinadamu tu,lakini wewe mbele za MUNGU umeshinda kwa tukio hili. Ni jaribu kwako,kipimo chako. Hiyo ni sadaka kubwa. Kuanzia muda wako,gharama zako. Hujapoteza bure.
Mbele za MUNGU umetoa sadaka kubwa. MUNGU ana maajabu yake.
Kitu kizuri utalipwa siku ambayo wewe hukuitarajia,niamini. Utatendewa kitu ambacho wewe hujui kimekujaje.

Hujui tu MUNGU alikuhifadhi maalumu kwa ajili ya kumuokoa huyo mtoto. Achana na mamaake,wewe muwazie yule mtoto jinsi ulivyomuokoa. Tena nataka nikuambie usingefanya Jambo baada ya kuambiwa,na kuona hali ya yule mtoto,angekufa. Hapo ndio ungejisikia vibaya mara mbili ya pain unayoipitia sasa.

Ndio maana MUNGU anazidi kuangalia uvumilivu wako kupitia kukuruka wewe. Kwa mawazo ya kibinadamu unaweza kuliona la kawaida,lakini ukiliwazia hata kidogo linaonekana wazi kabisa ni la ajabu. Umeshinda
 
Ila nimeumia mkuu.. Hajanipigia hadi saizi bado
Na hata kupigia nakuambia,Akipiga atakuja na excuse ya kitoto kweli.Ndivyo walivyo.

Atakuweka karibu akiwa na tatizo tena trust me.

Wewe ni daraja,Kuwa daraja ni kazi sana
Binafsi Nime deal na watu wa hivyo wengi mno.Nilipopata somo kwama mimi ni daraja nikaona.Ila nimepumguza huruma.Sababu mtu wa hivyo hata siku ukiwa na shida ya mia mbili hutaipata kwake.
 
Pia nataka nikuambie Leejay49 unajisikia vibaya ni kibinadamu tu,lakini wewe mbele za MUNGU umeshinda kwa tukio hili. Ni jaribu kwako,kipimo chako. Hiyo ni sadaka kubwa. Kuanzia muda wako,gharama zako. Hujapoteza bure.
Mbele za MUNGU umetoa sadaka kubwa. MUNGU ana maajabu yake.
Kitu kizuri utalipwa siku ambayo wewe hukuitarajia,niamini. Utatendewa kitu ambacho wewe hujui kimekujaje.

Hujui tu MUNGU alikuhifadhi maalumu kwa ajili ya kumuokoa huyo mtoto. Achana na mamaake,wewe muwazie yule mtoto jinsi ulivyomuokoa. Tena nataka nikuambie usingefanya Jambo baada ya kuambiwa,na kuona hali ya yule mtoto,angekufa. Hapo ndio ungejisikia vibaya mara mbili ya pain unayoipitia sasa.

Ndio maana MUNGU anazidi kuangalia uvumilivu wako kupitia kukuruka wewe. Kwa mawazo ya kibinadamu unaweza kuliona la kawaida,lakini ukiliwazia hata kidogo linaonekana wazi kabisa ni la ajabu. Umeshinda
Amen 🙏🙏.. Hakika nimejiskia vizuri baada ya kusoma maneno yako mkuu.. ubarikiwe sana kwa hekima hizi
 
Back
Top Bottom