Sijui kwanini nimeumia hivi

Pole sana huruma muda mwingine inaponza mumgu akutie nguvu
 
DuuhπŸ€”πŸ€”
 
Kaka one day atakuja2
 
Nimeumia sana mkuu, ameshindwa kunishukuru basi hata angenipigia Simu anijulishe kama wanaendelea vizuri.. Nimeumia haki ya Mungu tenaπŸ₯Ί
Pole Lee, kiukweli kuumizwa na hilo ni haki yako maana linaumiza.

Umia halafu jipe muda utapona. Lakini wakati unaumia chukua huo muda kumpigia simu na kumuuliza imekuwajee. Maana inawezekana alitenga muda wa kuwashukuru akakumbuka tu miamala akasahau keshi

Au alikuweka wa mwishoo kiitifaki ili aje aweke status kuubwa ya ma rangirangi.

Au anasubiria ukawatembelee apige picha mkiwa wote afu ndo aseme. Huyu ndiye amekuwa zaidi ya ndugu maana yupo hapa pamoja nami.

Mpigie/mtembelee halafu mueleze hisia(mwanamke to mwanamke) zako naye ataeleza majibu yake
 
Mkuu kwa jinsi alivyo atarudi tu,, maana hij ni mara ya pili namsaidia halafu inatokea vilevile.. Sijui hata natakiwa kufanya nini, ila ngoja nimpigie kwanza simu nitarudi
Usipigie simu achana huyo ndo tabia huwezi badilisha kitu songa jitenge nae hana upendo na wewe .ila ana upendo akiwa na shida tu
 
Jamani weweπŸ˜ƒπŸ˜ƒ
siku nyingine akija muonyeshe ukatili.
kuna single mom alinitapeli elfu 30, akanitapeli tena laki 1. siku moja bwana akapata ajali akavunjika pua. mamaye hana hata hela ya hospital. kapiga simu, akatuma mpaka video akiwa hosp kweli ukiangalia kavunjika.
anaomba msaada nimsaidie huku analia. hana hela ku clear bill. mm nilimwambia atafute hela alizonitapeli azitumie kulipa bill. alimpa mpaka mdogo wake simu anibembeleze mm nimeweka ngumu. nadhani walisema huyu mmeru ni mtoa roho
 
Nitafanya hivyo nikipata mda wa kwenda kwao.. Maana kwenye simu nahisi haitakua sawa
 
Mungu anakuona mkuuπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…