Sijui kwanini nimeumia hivi

Sijui kwanini nimeumia hivi

Habari za asubuhi wana JF,

Iko hivi, nina rafiki yangu ana mtoto (naweza nikasema ni single mom) ila isieleweke vibaya, nilisomaga nae O level huko ila nikama bahati tu tumejikuta tunaishi tena mtaa mmoja.

Ijumaa jioni wakati natoka tu ofisini alinipigia Simu akaniambia anashida kama naweza nipitie nyumbani kwao nikamuone, kwakua nilikua sina ratiba nyingine nikasema isiwe tabu kabla sijafika nyumbani nikapitia.

Nilimkuta yuko good ila mwanaye alikua anaumwa sana ile mtoto kazidiwa na akaniambia ameshindwa kwenda hospitali hana hela na almost kila aliyempigia simu wamemuahidi tu tangu asubuhi na hakuna aliyemtumia mpaka muda huo sa 1 jioni inaelekea saa 2.

Kiukweli sikua na hela and i was totally broke, yaani wiki ile iliyoisha mwenyewe nimeishi tu kwasababu nina wazazi maana nilikua nina mambo mengi yananihitaji hela kiasi kwamba sikua nimebakiwa na hata Mia mbovu. Lakini nikasema kwenye suala la kuokoa maisha ya mtoto isiwe kesi nikamwambia ngoja nirudi kwanza nyumbani, nikamsimulia mama tukaongea na dada yangu wakasema tu hapa kwa harakaharaka hatuna namna tumdanganye tu mzee kitu chochote jioni hii atupe hela, kweli tukamshawishi mzee bila hiyana akanipa 150k nikamfata kwao tukaenda hospitali usiku uleule.

Mtoto akapewa huduma ya kwanza na baadhi ya vipimo wakamlaza ili asubuhi aendelee na matibabu mengine (muda wote huo anawapigia ndugu zake wakiwemo na baba wa mtoto hata simu hawampokelei wengine), asubuhi yake niliomba ruhusa kazini nikawaambia nitachelewa ili nione mtoto atakua anaendeleaje.

Case ya mtoto ikawa kubwa wakasema tuende nae hospitali nyingine kubwa (Peramiho nadhani watu wa songea wanaijua), kuna vipimo alivyoambiwa wampime vilikua vinahitaji hela almost kama laki 2 tena nikamwambia mama akanitumia tukafanikisha. Kwasababu kazini walikua wanapigapiga sana simu na nikaona wanaendelea vizuri na mama yake alikua ashafika nikamwambia naenda ofisini incase kimetokea chochote utatuambia nikampa na namba ya mama kama mimi nisipopokea ampigie, nikaondoka. The bad thing is nilikua busy busy sana hadi siku ikaisha sikuwatafuta tena.

Kinachoniumiza ni kwamba, jana mchana nilimpigia simu hakupokea nikaenda kwao sikukuta mtu, nikaenda hadi Peramiho tena kulivyo mbali nikaambiwa wameruhusiwa na hakunipa taarifa. Jioni nimeingia WhatsApp naona ameweka status nyingi nyingi kufungua nikawa naona amescreenshot miamala yote ya watu waliokua wanamtumia hela na kuwapa credits Mungu awabariki sana kwa kuokoa maisha ya mwanae maana alikua kwenye hali mbaya sana na nini nini. Screenshot kama kumi na kitu hivi na amewataja na majina kabisa...

Cha ajabu hiyo miamala hakuna hata wa mtu mmoja uliofikia hata 30k, wote ni hizo hizo tu efu10 ef5 ef7, kawaandikia macaption mazito mazito. Nimebaki najiuliza mbona alikua ananiambia hawapokei simu, na hela inaonekana walimtumia siku ileile ambayo aliniambia na mimi niende kwake kumuona( Nilikua nasoma tarehe na muda wa zile transactions ).

Mimi ambaye nilikua nae kuanzia siku ile hadi usiku nikaacha na kwenda kazini na tumeclear bills zote hata asante hajaniambia na wala taarifa kama wameruhusiwa hajanipa. Nimesubiri jana yote hadi leo saizi hajanipigia hata simu, Kina mama wananiuliza wanaendeaje nawaambia tu wanaendelea vizuri huku roho inauma.

Nimetenda wema nimeenda zangu wakuu, lakini bado roho inaniuma aisee, sijui nifanye nini nikae sawa😥😥
Pole sana mkuu,mi nakuelewa huwa inauma kweli sio kwamba ulitaka akulipe chochote lakini kibinadamu mtu aliekutendea mema inapaswa umshukuru. Hasa ukizingatia wewe sio baba wa mtoto wala ndugu yake. Hatumuombei shida lakini bado ana mengi yanayomkabili duniani hakupaswa kufanya huu ujinga. Kama aliweza kuscreenshot meseji za wengine na kupost,alishindwa nini kupiga simu ya kuaga kwamba anatoka hospitali. Mi nakushauri mpigie au mtumie meseji mwambie nimesikia umetoka hospitali,nafurahi kujua hilo, Msalimie mtoto
 
Pole sana mkuu ila kubali au ukatae huyo rafiki ako ana kitu rohoni mwake juu yako. Angeshindwa kukupost bas hata sim ya taarifa tu kuwa hospital wamesharuhusiwa ili usihangaike tena kuwafuata huko napo ameshindwa.

Huyo ni wale marafiki ambao unamsaidia alafu anakuona kama unajipendekeza au kama unajifanya una hela sana wanakuaga na roho za wivu mbaya sana. Usishangae hata anakukalia kitako huyu anakusema vibaya kwa watu, ni kawaida yao anaona wewe una kaz ye hana bas anajikuta kama we ndo mwanga wake hawez kukushukuru hata siku moja.

NB. Kaa nae mbali usipige tena sim wala sms ili siku akipata shida tena ashindwe jins ya kukuanza.
 
Habari za asubuhi wana JF,

Iko hivi, nina rafiki yangu ana mtoto (naweza nikasema ni single mom) ila isieleweke vibaya, nilisomaga nae O level huko ila nikama bahati tu tumejikuta tunaishi tena mtaa mmoja.

Ijumaa jioni wakati natoka tu ofisini alinipigia Simu akaniambia anashida kama naweza nipitie nyumbani kwao nikamuone, kwakua nilikua sina ratiba nyingine nikasema isiwe tabu kabla sijafika nyumbani nikapitia.

Nilimkuta yuko good ila mwanaye alikua anaumwa sana ile mtoto kazidiwa na akaniambia ameshindwa kwenda hospitali hana hela na almost kila aliyempigia simu wamemuahidi tu tangu asubuhi na hakuna aliyemtumia mpaka muda huo sa 1 jioni inaelekea saa 2.

Kiukweli sikua na hela and i was totally broke, yaani wiki ile iliyoisha mwenyewe nimeishi tu kwasababu nina wazazi maana nilikua nina mambo mengi yananihitaji hela kiasi kwamba sikua nimebakiwa na hata Mia mbovu. Lakini nikasema kwenye suala la kuokoa maisha ya mtoto isiwe kesi nikamwambia ngoja nirudi kwanza nyumbani, nikamsimulia mama tukaongea na dada yangu wakasema tu hapa kwa harakaharaka hatuna namna tumdanganye tu mzee kitu chochote jioni hii atupe hela, kweli tukamshawishi mzee bila hiyana akanipa 150k nikamfata kwao tukaenda hospitali usiku uleule.

Mtoto akapewa huduma ya kwanza na baadhi ya vipimo wakamlaza ili asubuhi aendelee na matibabu mengine (muda wote huo anawapigia ndugu zake wakiwemo na baba wa mtoto hata simu hawampokelei wengine), asubuhi yake niliomba ruhusa kazini nikawaambia nitachelewa ili nione mtoto atakua anaendeleaje.

Case ya mtoto ikawa kubwa wakasema tuende nae hospitali nyingine kubwa (Peramiho nadhani watu wa songea wanaijua), kuna vipimo alivyoambiwa wampime vilikua vinahitaji hela almost kama laki 2 tena nikamwambia mama akanitumia tukafanikisha. Kwasababu kazini walikua wanapigapiga sana simu na nikaona wanaendelea vizuri na mama yake alikua ashafika nikamwambia naenda ofisini incase kimetokea chochote utatuambia nikampa na namba ya mama kama mimi nisipopokea ampigie, nikaondoka. The bad thing is nilikua busy busy sana hadi siku ikaisha sikuwatafuta tena.

Kinachoniumiza ni kwamba, jana mchana nilimpigia simu hakupokea nikaenda kwao sikukuta mtu, nikaenda hadi Peramiho tena kulivyo mbali nikaambiwa wameruhusiwa na hakunipa taarifa. Jioni nimeingia WhatsApp naona ameweka status nyingi nyingi kufungua nikawa naona amescreenshot miamala yote ya watu waliokua wanamtumia hela na kuwapa credits Mungu awabariki sana kwa kuokoa maisha ya mwanae maana alikua kwenye hali mbaya sana na nini nini. Screenshot kama kumi na kitu hivi na amewataja na majina kabisa...

Cha ajabu hiyo miamala hakuna hata wa mtu mmoja uliofikia hata 30k, wote ni hizo hizo tu efu10 ef5 ef7, kawaandikia macaption mazito mazito. Nimebaki najiuliza mbona alikua ananiambia hawapokei simu, na hela inaonekana walimtumia siku ileile ambayo aliniambia na mimi niende kwake kumuona( Nilikua nasoma tarehe na muda wa zile transactions ).

Mimi ambaye nilikua nae kuanzia siku ile hadi usiku nikaacha na kwenda kazini na tumeclear bills zote hata asante hajaniambia na wala taarifa kama wameruhusiwa hajanipa. Nimesubiri jana yote hadi leo saizi hajanipigia hata simu, Kina mama wananiuliza wanaendeaje nawaambia tu wanaendelea vizuri huku roho inauma.

Nimetenda wema nimeenda zangu wakuu, lakini bado roho inaniuma aisee, sijui nifanye nini nikae sawa😥😥
Kama unamsaidia mtu do it for good and for godsake, maana yeye ndiye analipa yote.

Pole sana.
 
Hapa duniani watu watenda mema huishia kuumia au kuumizwa tena huumizwa na watu wao wakaribu! Yani kwa tafsiri ya dunia watu watenda mema au wanao watendea mema wengine huonekana na kuchukuliwa watu dhaifu ila watenda mabaya na wanao tendea watu mabaya huonekana ni strong sana!

Ndugu Kanuni za dunia zinawakataa kabisa na zinakataa kabisa watu wanaotenda mema ndio maana wengi huishia kuumia na kuumizwa tena na walio watendea mema….

Dunia ni kama inahitaji watu makatili wasiojali na wenye roho ya kutu na ndio asilimia kubwa wana furahia maisha …kama unabisha kawatafute watu unaowajua ni wema halafu kawaulize idadi na walivyo na maumivu tena ya watu wao wa karibu

Dunia hii inawafanya watu na inafundisha watu kutotenda au kutotendea watu mema maana asilimia kubwa waliotenda au kuwatendea watu wema waliishia kuumizwa…pole sana hakika dunia sio sehemu salama kabisa kwa watu wanaowatendea mema wengine….

Pole sana usiache kuwatendea mema wengine na wala usitende mema ukitegemea jambo jema bali iwe ni part and parcel of your life….

Pole sana Mkuu dunia haina huruma uwezi amini kuna mtu nimetoka kumsaidia muda huu sasa najiuliza na mimi nitaumia au lah?

Ukipata muda soma hiki kitabu “who will cry when you die”
 

Attachments

Yaani nashindwa kueleza ninavyojiskia,, sihitaji anilipe chochote wala chochote ila tu nimeumia ndomana najishangaa kwanini inakua hivi hadi nashindwa kujizuia.. Hata sielewi naumia nini yani
Kwa mtindo wako huu wa kutendea watu wema na kuhakikishia utakufa mapema kwa maumivu ya moyo kabisa!
Dunia haitaki kabisa watu wema kama wewe utachofaidi hapa duniani ni maumivu tuu…
Pole sana
 
Habari za asubuhi wana JF,

Iko hivi, nina rafiki yangu ana mtoto (naweza nikasema ni single mom) ila isieleweke vibaya, nilisomaga nae O level huko ila nikama bahati tu tumejikuta tunaishi tena mtaa mmoja.

Ijumaa jioni wakati natoka tu ofisini alinipigia Simu akaniambia anashida kama naweza nipitie nyumbani kwao nikamuone, kwakua nilikua sina ratiba nyingine nikasema isiwe tabu kabla sijafika nyumbani nikapitia.

Nilimkuta yuko good ila mwanaye alikua anaumwa sana ile mtoto kazidiwa na akaniambia ameshindwa kwenda hospitali hana hela na almost kila aliyempigia simu wamemuahidi tu tangu asubuhi na hakuna aliyemtumia mpaka muda huo sa 1 jioni inaelekea saa 2.

Kiukweli sikua na hela and i was totally broke, yaani wiki ile iliyoisha mwenyewe nimeishi tu kwasababu nina wazazi maana nilikua nina mambo mengi yananihitaji hela kiasi kwamba sikua nimebakiwa na hata Mia mbovu. Lakini nikasema kwenye suala la kuokoa maisha ya mtoto isiwe kesi nikamwambia ngoja nirudi kwanza nyumbani, nikamsimulia mama tukaongea na dada yangu wakasema tu hapa kwa harakaharaka hatuna namna tumdanganye tu mzee kitu chochote jioni hii atupe hela, kweli tukamshawishi mzee bila hiyana akanipa 150k nikamfata kwao tukaenda hospitali usiku uleule.

Mtoto akapewa huduma ya kwanza na baadhi ya vipimo wakamlaza ili asubuhi aendelee na matibabu mengine (muda wote huo anawapigia ndugu zake wakiwemo na baba wa mtoto hata simu hawampokelei wengine), asubuhi yake niliomba ruhusa kazini nikawaambia nitachelewa ili nione mtoto atakua anaendeleaje.

Case ya mtoto ikawa kubwa wakasema tuende nae hospitali nyingine kubwa (Peramiho nadhani watu wa songea wanaijua), kuna vipimo alivyoambiwa wampime vilikua vinahitaji hela almost kama laki 2 tena nikamwambia mama akanitumia tukafanikisha. Kwasababu kazini walikua wanapigapiga sana simu na nikaona wanaendelea vizuri na mama yake alikua ashafika nikamwambia naenda ofisini incase kimetokea chochote utatuambia nikampa na namba ya mama kama mimi nisipopokea ampigie, nikaondoka. The bad thing is nilikua busy busy sana hadi siku ikaisha sikuwatafuta tena.

Kinachoniumiza ni kwamba, jana mchana nilimpigia simu hakupokea nikaenda kwao sikukuta mtu, nikaenda hadi Peramiho tena kulivyo mbali nikaambiwa wameruhusiwa na hakunipa taarifa. Jioni nimeingia WhatsApp naona ameweka status nyingi nyingi kufungua nikawa naona amescreenshot miamala yote ya watu waliokua wanamtumia hela na kuwapa credits Mungu awabariki sana kwa kuokoa maisha ya mwanae maana alikua kwenye hali mbaya sana na nini nini. Screenshot kama kumi na kitu hivi na amewataja na majina kabisa...

Cha ajabu hiyo miamala hakuna hata wa mtu mmoja uliofikia hata 30k, wote ni hizo hizo tu efu10 ef5 ef7, kawaandikia macaption mazito mazito. Nimebaki najiuliza mbona alikua ananiambia hawapokei simu, na hela inaonekana walimtumia siku ileile ambayo aliniambia na mimi niende kwake kumuona( Nilikua nasoma tarehe na muda wa zile transactions ).

Mimi ambaye nilikua nae kuanzia siku ile hadi usiku nikaacha na kwenda kazini na tumeclear bills zote hata asante hajaniambia na wala taarifa kama wameruhusiwa hajanipa. Nimesubiri jana yote hadi leo saizi hajanipigia hata simu, Kina mama wananiuliza wanaendeaje nawaambia tu wanaendelea vizuri huku roho inauma.

Nimetenda wema nimeenda zangu wakuu, lakini bado roho inaniuma aisee, sijui nifanye nini nikae sawa😥😥
Wanaume wakilalamika masingo maza sio watu muwe mnaelewa. Fikiri hapo ungemsomeshea na kumlelea mwanae alafu mwisho wa siku anakuja kuchukuliwa na baba wa mtoto kirahisi tu na wewe kupewa maneno ya kuuudhi. Singo maza is a no go zone chapa sepa
 
Nadhani tabia yake mbaya Haina uhusiano na usingle mama wake.

Kuna watu kwa asili tu hawanaga shukrani.

Msamehe tu,kisha endelea na mambo yako.

Usimtafute tena.
Mbona wengine kuwashukuru ila main character katupa mbali
 
Wanaume wakilalamika masingo maza sio watu muwe mnaelewa. Fikiri hapo ungemsomeshea na kumlelea mwanae alafu mwisho wa siku anakuja kuchukuliwa na baba wa mtoto kirahisi tu na wewe kupewa maneno ya kuuudhi. Singo maza is a no go zone chapa sepa
Kwakweli nimeliona hilo
 
Kwa mtindo wako huu wa kutendea watu wema na kuhakikishia utakufa mapema kwa maumivu ya moyo kabisa!
Dunia haitaki kabisa watu wema kama wewe utachofaidi hapa duniani ni maumivu tuu…
Pole sana
Duuh🤔🤔😔
 
Pole sana mkuu,mi nakuelewa huwa inauma kweli sio kwamba ulitaka akulipe chochote lakini kibinadamu mtu aliekutendea mema inapaswa umshukuru. Hasa ukizingatia wewe sio baba wa mtoto wala ndugu yake. Hatumuombei shida lakini bado ana mengi yanayomkabili duniani hakupaswa kufanya huu ujinga. Kama aliweza kuscreenshot meseji za wengine na kupost,alishindwa nini kupiga simu ya kuaga kwamba anatoka hospitali. Mi nakushauri mpigie au mtumie meseji mwambie nimesikia umetoka hospitali,nafurahi kujua hilo, Msalimie mtoto
Asante kwa ushauri mzuri mkuu, barikiwa sana🙏🙏
 
Pole sana mkuu ila kubali au ukatae huyo rafiki ako ana kitu rohoni mwake juu yako. Angeshindwa kukupost bas hata sim ya taarifa tu kuwa hospital wamesharuhusiwa ili usihangaike tena kuwafuata huko napo ameshindwa.

Huyo ni wale marafiki ambao unamsaidia alafu anakuona kama unajipendekeza au kama unajifanya una hela sana wanakuaga na roho za wivu mbaya sana. Usishangae hata anakukalia kitako huyu anakusema vibaya kwa watu, ni kawaida yao anaona wewe una kaz ye hana bas anajikuta kama we ndo mwanga wake hawez kukushukuru hata siku moja.

NB. Kaa nae mbali usipige tena sim wala sms ili siku akipata shida tena ashindwe jins ya kukuanza.
Kwakweli nitafanya hivyo.. Mungu tu awasaidie waendelee kuwa salama ila sitowatafuta tena
 
Labda kweli
Shida ya akina mama ndio hii sio wote ila baadhi they can’t move on,yaani mm ningekaa kimya tu na ningemuambia mama pia mchezo wote uliotokea ili mumpotezee mazima possible baba mtoto amemuita wakalee mtoto don’t worry they will come back and ile roho yako itakua na Majibu zaidi and never ask her anything kuhusu hilo tukio
 
Me nlishaga acha kuwaonea huruma wanawake, there must be an arrangement where we meet in between, yan kama communication ni iwe back and forth, lazima kuwe na reciprocate ya vitu, yan Quid pro quo. Wanawake tunatakiwa tuwapende sawa ila usiwaonee huruma, yan ukiwaonea huruma kuna namna huwa wanakuja kuona ile huruma ni haki yao, ukitrip kidogo tu anaona umemkosea. Mzee mind your own business wanawake watakupotezea muda huu ni ukweli lakini ni mchungu, once you have solved their problems women dont give a shit about you. Mungu atakulipa masta.
Amen, Nimejifunza kitu
 
Nimeumia sana mkuu, ameshindwa kunishukuru basi hata angenipigia Simu anijulishe kama wanaendelea vizuri.. Nimeumia haki ya Mungu tena[emoji3064]
Pole sana, tenda wema nenda zako usingoje shukrani.....kuna siku atakutafuta tena akiwa na shida.....for now mshukuru Mungu tu kwamba hela za wazazi wako hazikwenda bure mtoto alipona
 
Back
Top Bottom