Sijui kwanini nimeumia hivi

Sijui kwanini nimeumia hivi

Habari za asubuhi wana JF,

Iko hivi, nina rafiki yangu ana mtoto (naweza nikasema ni single mom) ila isieleweke vibaya, nilisomaga nae O level huko ila nikama bahati tu tumejikuta tunaishi tena mtaa mmoja.

Ijumaa jioni wakati natoka tu ofisini alinipigia Simu akaniambia anashida kama naweza nipitie nyumbani kwao nikamuone, kwakua nilikua sina ratiba nyingine nikasema isiwe tabu kabla sijafika nyumbani nikapitia.

Nilimkuta yuko good ila mwanaye alikua anaumwa sana ile mtoto kazidiwa na akaniambia ameshindwa kwenda hospitali hana hela na almost kila aliyempigia simu wamemuahidi tu tangu asubuhi na hakuna aliyemtumia mpaka muda huo sa 1 jioni inaelekea saa 2.

Kiukweli sikua na hela and i was totally broke, yaani wiki ile iliyoisha mwenyewe nimeishi tu kwasababu nina wazazi maana nilikua nina mambo mengi yananihitaji hela kiasi kwamba sikua nimebakiwa na hata Mia mbovu. Lakini nikasema kwenye suala la kuokoa maisha ya mtoto isiwe kesi nikamwambia ngoja nirudi kwanza nyumbani, nikamsimulia mama tukaongea na dada yangu wakasema tu hapa kwa harakaharaka hatuna namna tumdanganye tu mzee kitu chochote jioni hii atupe hela, kweli tukamshawishi mzee bila hiyana akanipa 150k nikamfata kwao tukaenda hospitali usiku uleule.

Mtoto akapewa huduma ya kwanza na baadhi ya vipimo wakamlaza ili asubuhi aendelee na matibabu mengine (muda wote huo anawapigia ndugu zake wakiwemo na baba wa mtoto hata simu hawampokelei wengine), asubuhi yake niliomba ruhusa kazini nikawaambia nitachelewa ili nione mtoto atakua anaendeleaje.

Case ya mtoto ikawa kubwa wakasema tuende nae hospitali nyingine kubwa (Peramiho nadhani watu wa songea wanaijua), kuna vipimo alivyoambiwa wampime vilikua vinahitaji hela almost kama laki 2 tena nikamwambia mama akanitumia tukafanikisha. Kwasababu kazini walikua wanapigapiga sana simu na nikaona wanaendelea vizuri na mama yake alikua ashafika nikamwambia naenda ofisini incase kimetokea chochote utatuambia nikampa na namba ya mama kama mimi nisipopokea ampigie, nikaondoka. The bad thing is nilikua busy busy sana hadi siku ikaisha sikuwatafuta tena.

Kinachoniumiza ni kwamba, jana mchana nilimpigia simu hakupokea nikaenda kwao sikukuta mtu, nikaenda hadi Peramiho tena kulivyo mbali nikaambiwa wameruhusiwa na hakunipa taarifa. Jioni nimeingia WhatsApp naona ameweka status nyingi nyingi kufungua nikawa naona amescreenshot miamala yote ya watu waliokua wanamtumia hela na kuwapa credits Mungu awabariki sana kwa kuokoa maisha ya mwanae maana alikua kwenye hali mbaya sana na nini nini. Screenshot kama kumi na kitu hivi na amewataja na majina kabisa...

Cha ajabu hiyo miamala hakuna hata wa mtu mmoja uliofikia hata 30k, wote ni hizo hizo tu efu10 ef5 ef7, kawaandikia macaption mazito mazito. Nimebaki najiuliza mbona alikua ananiambia hawapokei simu, na hela inaonekana walimtumia siku ileile ambayo aliniambia na mimi niende kwake kumuona( Nilikua nasoma tarehe na muda wa zile transactions ).

Mimi ambaye nilikua nae kuanzia siku ile hadi usiku nikaacha na kwenda kazini na tumeclear bills zote hata asante hajaniambia na wala taarifa kama wameruhusiwa hajanipa. Nimesubiri jana yote hadi leo saizi hajanipigia hata simu, Kina mama wananiuliza wanaendeaje nawaambia tu wanaendelea vizuri huku roho inauma.

Nimetenda wema nimeenda zangu wakuu, lakini bado roho inaniuma aisee, sijui nifanye nini nikae sawa😥😥
Pole sana! Umeshamjua, achana naye, ikibidi waeleze Mama na dada yako kama njia ya kujipa ahueni kwa kutendwa, ila huyo mtu msahau!
 
Habari za asubuhi wana JF,

Iko hivi, nina rafiki yangu ana mtoto (naweza nikasema ni single mom) ila isieleweke vibaya, nilisomaga nae O level huko ila nikama bahati tu tumejikuta tunaishi tena mtaa mmoja.

Ijumaa jioni wakati natoka tu ofisini alinipigia Simu akaniambia anashida kama naweza nipitie nyumbani kwao nikamuone, kwakua nilikua sina ratiba nyingine nikasema isiwe tabu kabla sijafika nyumbani nikapitia.

Nilimkuta yuko good ila mwanaye alikua anaumwa sana ile mtoto kazidiwa na akaniambia ameshindwa kwenda hospitali hana hela na almost kila aliyempigia simu wamemuahidi tu tangu asubuhi na hakuna aliyemtumia mpaka muda huo sa 1 jioni inaelekea saa 2.

Kiukweli sikua na hela and i was totally broke, yaani wiki ile iliyoisha mwenyewe nimeishi tu kwasababu nina wazazi maana nilikua nina mambo mengi yananihitaji hela kiasi kwamba sikua nimebakiwa na hata Mia mbovu. Lakini nikasema kwenye suala la kuokoa maisha ya mtoto isiwe kesi nikamwambia ngoja nirudi kwanza nyumbani, nikamsimulia mama tukaongea na dada yangu wakasema tu hapa kwa harakaharaka hatuna namna tumdanganye tu mzee kitu chochote jioni hii atupe hela, kweli tukamshawishi mzee bila hiyana akanipa 150k nikamfata kwao tukaenda hospitali usiku uleule.

Mtoto akapewa huduma ya kwanza na baadhi ya vipimo wakamlaza ili asubuhi aendelee na matibabu mengine (muda wote huo anawapigia ndugu zake wakiwemo na baba wa mtoto hata simu hawampokelei wengine), asubuhi yake niliomba ruhusa kazini nikawaambia nitachelewa ili nione mtoto atakua anaendeleaje.

Case ya mtoto ikawa kubwa wakasema tuende nae hospitali nyingine kubwa (Peramiho nadhani watu wa songea wanaijua), kuna vipimo alivyoambiwa wampime vilikua vinahitaji hela almost kama laki 2 tena nikamwambia mama akanitumia tukafanikisha. Kwasababu kazini walikua wanapigapiga sana simu na nikaona wanaendelea vizuri na mama yake alikua ashafika nikamwambia naenda ofisini incase kimetokea chochote utatuambia nikampa na namba ya mama kama mimi nisipopokea ampigie, nikaondoka. The bad thing is nilikua busy busy sana hadi siku ikaisha sikuwatafuta tena.

Kinachoniumiza ni kwamba, jana mchana nilimpigia simu hakupokea nikaenda kwao sikukuta mtu, nikaenda hadi Peramiho tena kulivyo mbali nikaambiwa wameruhusiwa na hakunipa taarifa. Jioni nimeingia WhatsApp naona ameweka status nyingi nyingi kufungua nikawa naona amescreenshot miamala yote ya watu waliokua wanamtumia hela na kuwapa credits Mungu awabariki sana kwa kuokoa maisha ya mwanae maana alikua kwenye hali mbaya sana na nini nini. Screenshot kama kumi na kitu hivi na amewataja na majina kabisa...

Cha ajabu hiyo miamala hakuna hata wa mtu mmoja uliofikia hata 30k, wote ni hizo hizo tu efu10 ef5 ef7, kawaandikia macaption mazito mazito. Nimebaki najiuliza mbona alikua ananiambia hawapokei simu, na hela inaonekana walimtumia siku ileile ambayo aliniambia na mimi niende kwake kumuona( Nilikua nasoma tarehe na muda wa zile transactions ).

Mimi ambaye nilikua nae kuanzia siku ile hadi usiku nikaacha na kwenda kazini na tumeclear bills zote hata asante hajaniambia na wala taarifa kama wameruhusiwa hajanipa. Nimesubiri jana yote hadi leo saizi hajanipigia hata simu, Kina mama wananiuliza wanaendeaje nawaambia tu wanaendelea vizuri huku roho inauma.

Nimetenda wema nimeenda zangu wakuu, lakini bado roho inaniuma aisee, sijui nifanye nini nikae sawa😥😥


Ndugu yangu Mimi ni Mkarimu sana, ila sasa nimekuwa mbaya zaidi ya Mnyama, kuna Mdada alikuwa mke wa rafiki yangu, aka paralyse, akiwa katika hali hiyo, nikampalaki 8, kumbe lishamtelekeza rafiki yangu, akaenda kwao kijijini na alishakufa.

Kuna sababu kwa nini watu huwa wana shida, nakueleza ukweli mimi naweza enda mahali nikasaidia mtu nisiyemjua kiasi kikubwa cha hela, ila ni ngumu SANA saidia mtu ataayekuja nililia shida.
 
Ndugu yangu Mimi ni Mkarimu sana, ila sasa nimekuwa mbaya zaidi ya Mnyama, kuna Mdada alikuwa mke wa rafiki yangu, aka paralyse, akiwa katika hali hiyo, nikampalaki 8, kumbe lishamtelekeza rafiki yangu, akaenda kwao kijijini na alishakufa.

Kuna sababu kwa nini watu huwa wana shida, nakueleza ukweli mimi naweza enda mahali nikasaidia mtu nisiyemjua kiasi kikubwa cha hela, ila ni ngumu SANA saidia mtu ataayekuja nililia shida.
Nimejifunza kitu aisee.. Nitaanza kua na roho mbaya na mimi
 
Pole sana! Umeshamjua, achana naye, ikibidi waeleze Mama na dada yako kama njia ya kujipa ahueni kwa kutendwa, ila huyo mtu msahau!
Nilishafaya hivyo mkuu.. Niko good now
 
Dada Leejay49 nimeyavaa maumivu yako yamenishinda na mimi nimejikuta naumia kama vile yamwnikuta mimi .
Watu wema ila watu wabaya , njia nzuri jitahidi kusahau hayo , futq namba ya huyo mchawi , anza maisha mapya bila kukumbuka uliwahi kujuana na Shetani wa aina hiyo
Usimpe tena hata chance ya kupiga story na wewe mfute maishani mwako huyo sio rafiki , sio ndugu , sio mtu mwema hata kidogo .
Wahenga walisema tenda mema nenda zako ila haikuwa utende wema uende kama hivi ulivyoondoshwa dada Leejay49 samehe ila usimsahau .
Pole sana , nasikitika na wewe na pia naumia na wewe , karibu Chabruma tupige story
Asante mkuu, siku nyingine ukipita Bombambili uje tupige stori huko naogopa wanajeshi😃😃😃
 
Huyo mdada ulimsaidia hela ambayo ingetosha matibabu yote kwa hiyo kukuandika hapo status ingezua taharuki kwa wale wengine waliochanga pesa ndogo ndogo .HAPO HAJAKUWEKA WW ILI KUJILINDA YEYE SIO KWAMBA AMEKUDHARAU .ILA AMESHINDWA KUKUPA TAARIFA NA PIA HANA AKILI NZURI MANA ANGEWEZA HATA KUKUWEKA STATUS UONE PEKE YAKO MUAMALA ULIO MTUMIA.
Duuh, kwakweli
 
Huyu bidada siyo chuma au jiwe ni binadamu lazima atamani na yeye kutambuliwa mchango wake kwa vile msaidiwa kaamua kuwataja wahisani wake naye alipaswa kumtaja.
Tusiweke unafiki hata wewe na sisi tungeumia.
Huoni mfano mabango ya KWA HISANI YA WALIPA KODI WA MAREKANI au JAPAN?
Barikiwa sana mkuu, Umenena vyema
 
Pole sans mkuu, lakini jifunze siku nyingine mwanamke aliezaliswha na mtu usihangaike nae utapotea. Shukuru kaposti miamala, je angepost kaenda kwa jamaa na alisema hapokei simu kumpa hela ya matibabu ya mtoto ungejisikiaje japo sio mpenzi wako. Anyway huend anataka kuja kukupa SPECIAL THANKS kuwa mvumilivu ule tunda.
Duuh 🤔
 
Ubinadamu kazi my dear

And it's okay moyo kukuuma

Lakini usiruhusu kuumia sana

Take it easy, umefanya kwa nafasi yako kadri ulivoweza

Mengine mwachie yeye na Mungu wake watajuana wenyewe
Namshukuru Mungu niko good saizi
 
Kaa kimyaaa kama vile hakuna kitu kilitokea.
Nakurudia tena,kaa kimya mdogo wangu.
Kaa kimya kuna jibu linakujaa.
We kaa kimya tuu na usisimulie saana kwa watu.
 
Kinacho uma ni vile hâta kutambua msaada wako. Anawashukuru wengine na anakuacha wewe. Hama huo mtaa mkimbie na Blocks juu
 
Bora wewe mtu baking, mi niliwahi uguza bamkwe katokea kijijini singida nimempambania tezi dume tena hakua hata na Bima.
Nilitoboka kisawasawa na madeni juu niliingia.
Alivyoruhusiwa hosi akarudi kwao singida hata asiniage, yaani alimuaga bintiye tu akamwambia ataniagia. Kumbuka kafikia kwangu kila siku tunaonana.
Niko zangu job ndio natumiwa message wasap mzee anakuaga anaondoka.
Sikujibu wala nini, nilipotezea ila kwakweli niliumia.
 
Bora wewe mtu baking, mi niliwahi uguza bamkwe katokea kijijini singida nimempambania tezi dume tena hakua hata na Bima.
Nilitoboka kisawasawa na madeni juu niliingia.
Alivyoruhusiwa hosi akarudi kwao singida hata asiniage, yaani alimuaga bintiye tu akamwambia ataniagia. Kumbuka kafikia kwangu kila siku tunaonana.
Niko zangu job ndio natumiwa message wasap mzee anakuaga anaondoka.
Sikujibu wala nini, nilipotezea ila kwakweli niliumia.
Hilo ndo kubwa zaidi mkuu.. Pole sana aisee
 
Kaa kimyaaa kama vile hakuna kitu kilitokea.
Nakurudia tena,kaa kimya mdogo wangu.
Kaa kimya kuna jibu linakujaa.
We kaa kimya tuu na usisimulie saana kwa watu.
Nashukuru lilipita mkuu, niko vizuri saizi
 
Back
Top Bottom