Sijui ni uchawi huu?

Sijui ni uchawi huu?

M/Mungu ameeleza kuwepo kwa nguvu za giza(shetani) fanya jitiada za dua, vinginevyo tumia miti aliyoumba Allah kujisaidia.
 
Kapime Kisukari na HIV....Sukari inachosha Sana mwili na HIV kwenye dalili za mwanzoni inanyong'onyeza mwili...Ila usipime hivyo nenda upate ushauri nasaha kwanza
 
Kwemah ndugu zangu?

Moja kwa moja kwenye mada, mimi ni mwanafunzi wa chuo Dodoma, muda kidogo kama miezi 4 iliyopita niliamia katika nyumba moja baada ya kushauriwa na mama mmoja mkazi wa eneo hilo aliyekuwa anasimamia hiyo nyumba ingawa siyo yake, nilikuwa pia namtumia katika kujenga hiyo nyumba yetu kama kuchota maji, mchanga, kujenga.

Nilihamia hapo sababu ni jirani na eneo ambalo nilikuwa nikisimamia ujenzi wa nyumba yetu, nikatafuta na mpangaji mwengine nikamuingiza bila kumshirikisha huyo mama na huyo mama akawa jirani yetu, hivyo tukawa wawili katika nyumba yote hiyo kubwa.

Baada ya kuingia katika ile nyumba nikawa mara nyingi ni mtu wa kulala sana, kushindwa kuamka mapema na kuchoka kupita kiasi, nikasema labda tiba ya hii hali niwe nafanya mazoezi ingawa kilingana na ratiba nikawa nashindwa kufanya labda itokee nimepiga push up kidogo au kuruka kamba.

Siku moja ambayo nilipanga mimi na rafiki yangu tufanye jogging, ikatokea kuna mjusi ambaye mara kwa mara nilikuwa nikimuona hapo ndani hivyo nikasema hiyo siku nimuue(ilikuwa mida ya saa 10). Alikuwa ukutani nikarusha teke nikamkanyaga ila sasa cha ajabu, niliua mjusi mmoja akawa pale chini lakini mikia ilikuwa miwili mizima kabisa, nikashangaa kweli.

Nikaomba kidogo nikapotezea baadae nikaenda mazoezi, hali ya kuchoka ikawa inaendelea baadae nikaanza kuwa najiuliza sasa ni mazoezi gani ambayo nitafanya yanitoe katika hii hali, je,kuruka kamba, kudanceau push up?

Baadae moyo ukawa unaniuma na kujiuliza maswali kama mazoezi nitafanya hadi lini na mbona mtu fulani hafanyi na yupo vizuri, inamaana siku zote maishani nitakuwa mtu wa mazoezi, watu ambao hawafanyi mazoezi wanaishi vipi maisha?!

Nikawa nakosa furaha kabisa, moyo unauma nikasema labda nitatizo la afya ya akili. Nimeenda hospitali nimetumia dawa miezi 2, wananielekeza lakini akili haitulii kabisa. Nafikiria jinsi ya kujitoa maisha.

Nimeenda kwenye maombi nikaanza kuota ndoto nyingi sana, kila siku hususan ile nyumba ninayoijenga inaharibika, mara nimuote yule mama jirani ni mchawi. Nasali sana natamani haya mawazo yatoke, nikitamani pia huyo mama limkute jambo ila bado.

Sasa nashindwa kuelewa je, ni maono, mawazo yangu, athari ya hizi dawa ama nini?!
...Tatizo umeishakuwa na Imani ya Kurogwa! Itakusumbua Sana....
 
Haunted house!
Usipuuze,soma zaburi ya 148 Mara 7,asubuhi na jioni,Kwa Siku tatu,wakati wa kulala paka Mafuta ya mizaituni kwenye nyayo zako,ulete mrejesho hapa.
 
Kwani hiyo nyumba unakaa bure mzee embu hama hapo kapange sehem nyingine!!

Au kma vp kila 9t uwe unavuta msuba then unalala
 
Pole sana.
Nakushauri uwe mtu wa kuomba Toba juu yako kwa yote uliyoyatenda ili upate kusamehe na kusamehewa.
Kwa msamaha soma Zaburi 25,51 na 73.
Kwa ulinzi na uponyaji soma Zaburi 7,13,16,17,18,23,27,35 pia 140 yaani jitahidi kusoma Zaburi.
Jitahidi kujipa muda wa maombi utapata uponyaji
 
Ng'ong'ona hiyo nimeishi hapo miaka 4 unatakiwa uweke bange kwenye mto unaolalia
 
Kwemah ndugu zangu?

Moja kwa moja kwenye mada, mimi ni mwanafunzi wa chuo Dodoma, muda kidogo kama miezi 4 iliyopita niliamia katika nyumba moja baada ya kushauriwa na mama mmoja mkazi wa eneo hilo aliyekuwa anasimamia hiyo nyumba ingawa siyo yake, nilikuwa pia namtumia katika kujenga hiyo nyumba yetu kama kuchota maji, mchanga, kujenga.

Nilihamia hapo sababu ni jirani na eneo ambalo nilikuwa nikisimamia ujenzi wa nyumba yetu, nikatafuta na mpangaji mwengine nikamuingiza bila kumshirikisha huyo mama na huyo mama akawa jirani yetu, hivyo tukawa wawili katika nyumba yote hiyo kubwa.

Baada ya kuingia katika ile nyumba nikawa mara nyingi ni mtu wa kulala sana, kushindwa kuamka mapema na kuchoka kupita kiasi, nikasema labda tiba ya hii hali niwe nafanya mazoezi ingawa kilingana na ratiba nikawa nashindwa kufanya labda itokee nimepiga push up kidogo au kuruka kamba.

Siku moja ambayo nilipanga mimi na rafiki yangu tufanye jogging, ikatokea kuna mjusi ambaye mara kwa mara nilikuwa nikimuona hapo ndani hivyo nikasema hiyo siku nimuue(ilikuwa mida ya saa 10). Alikuwa ukutani nikarusha teke nikamkanyaga ila sasa cha ajabu, niliua mjusi mmoja akawa pale chini lakini mikia ilikuwa miwili mizima kabisa, nikashangaa kweli.

Nikaomba kidogo nikapotezea baadae nikaenda mazoezi, hali ya kuchoka ikawa inaendelea baadae nikaanza kuwa najiuliza sasa ni mazoezi gani ambayo nitafanya yanitoe katika hii hali, je,kuruka kamba, kudanceau push up?

Baadae moyo ukawa unaniuma na kujiuliza maswali kama mazoezi nitafanya hadi lini na mbona mtu fulani hafanyi na yupo vizuri, inamaana siku zote maishani nitakuwa mtu wa mazoezi, watu ambao hawafanyi mazoezi wanaishi vipi maisha?!

Nikawa nakosa furaha kabisa, moyo unauma nikasema labda nitatizo la afya ya akili. Nimeenda hospitali nimetumia dawa miezi 2, wananielekeza lakini akili haitulii kabisa. Nafikiria jinsi ya kujitoa maisha.

Nimeenda kwenye maombi nikaanza kuota ndoto nyingi sana, kila siku hususan ile nyumba ninayoijenga inaharibika, mara nimuote yule mama jirani ni mchawi. Nasali sana natamani haya mawazo yatoke, nikitamani pia huyo mama limkute jambo ila bado.

Sasa nashindwa kuelewa je, ni maono, mawazo yangu, athari ya hizi dawa ama nini?!
Acha Kuvuta Bange Mkuu
Eventually uta data
 
Back
Top Bottom