Sijui Nitakumbukwa kwa Lipi Baada ya Maisha Yangu Hapa Duniani.

Ryzen

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2012
Posts
7,301
Reaction score
8,706
Nalala usingizi hauji, Nimejigeuza Mara kibao kuutafufuta usingizi lakini wapi, mwili unataka lakini akili haitaki..

Mara Nakumbuka Nimeishi kwenye hii Dunia zaidi ya Miaka 20 ila hakuna nililolifanya.. Hata Baiskeli sina.. Elimu sina.. Hakuna hata fununu wala tetesi ya Jina Langu Kukumbukwa au Kuenziwa Mara baada ya Maisha yangu Kufikia kikomo hapa duniani..

Nitafanya nini Jina langu Libaki? Nifanye nini?
 
Umeishi zaidi ya miaka ishirini... hata ukiifikiria miaka uliyoipoteza wala haitarudi na zaidi utakata tamaa na kupoteza miaka mingi zaidi. Jifikirie kuanzia hapo ulipo kaka maana hiyo tu ndo itakubadilisha na wala sio manung'uniko yako.. Siamini katika kuishi kwako kote hakuna usichokijua au kile unachokiamini..pengind tupo katika umri mmoja na hili ndilo nakuambia, safari tuliyotoka bado sanaaa maana tupo karibu na kufika katikati ya safari..usipoteze nusu nyingineyo
 
Kaka Asante kwa kUchukua Muda wako na kubandika wazo la kitukufu kama hilo, tunafanyeje??
 
Tenda wema kwa jirani yako, pia kua MTU positive utafariki USO ukiwa unang'aa nuru
Ndugu yako Pamoja na Vipaji Lukuki na u tunu wake aliokuwa nao katika uso wa sayari hii alidiriki kusema wakati wa kifo chake kuwa anaomba msamaha kwa Mungu na Wanadamu kwani Hajatenda Kadri ya alivyotakiwa Kutenda
 
Ndugu yako Pamoja na Vipaji Lukuki na u tunu wake aliokuwa nao katika uso wa sayari hii alidiriki kusema wakati wa kifo chake kuwa anaomba msamaha kwa Mungu na Wanadamu kwani Hajatenda Kadri ya alivyotakiwa Kutenda
Naam aliyasema maneno hayo coz alikosa the so-called inner peace. Tengeneza inner peace utafariki ukiwa umetabasamu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…