Sijui nitamsaidiaje huyu rafiki yangu, uume wake haufanyi kazi kabisa

Siasa Basi

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2016
Posts
1,493
Reaction score
4,281
Nina rafiki yangu kipenzi tumetoka nae mbali sana siri zangu zake. Tunaisha pamoja kama ndugu sasa. Tulikutana Alevel huko Moshi na ndipo urafiki wetu ulipoanzia, bahati nzuri tulichaguliwa chuo kimoja mimi na yeye lakini kozi tofauti. Lakini bado tulikuwa karibu sana tukisaidia.Mpaka tunamaliza chuo.

Lakini kuna jambo moja alikuwa ananificha kwa kipindi kirefu bila kuniambia, lakini kwa tabia yake sikuwah ikujua kabisa kama huyu rafiki yang dudu yake haifanyi kazi. Alikuwa karibu na wasichana sana na alipendwa na kila msichana kwa ucheshi wake, utanashati na vituko. Nilijua jamaa yangu huyu ni kicheche kweli.

Siku zimeenda baada ya kuhitimu Mungu alijalia tulipata kazi wote hapa Dar, lakini sector tofauti, yeye akaenda kupanga Mwenge na mimi nikapanga zangu Mbagala mji wa kijanja. Mi nikavuta jiko fasta maana wakati nikiwa chuo nilimpa mwanachuo mwenzangu mimba ndie niliyemchukua na kumuweka ndani na harusi ilifanyika na shega alikuwa rafiki yangu.

Sasa siku zikawa zinakwenda sioni shemeji yangu kila nikimuuliza anasema muda bado. Lakini akija kwangu akitazama mwanangu machozi yanamtoka. Nikawa najiuliza kwanini huyu rafiki akimuona mwanangu analia? Kuna siku nikamuuliza sababu nini?

Alichonijibu akaniambia moyo wa mtu kichaka. Ila ipo siku atanimbia. Muda mwingine alikuwa na mawazo sana, nikawa nashindwa kumwelewa jamaa kama maisha anayo mazuri, gari ya kutembelea anayo na hana familia ya kumusumbua sasa tatizo ni nini?

Leo kaja kwangu asubuhi, akanambia rafiki kuna jambo nataka nikwambia. Akaanza kunipa stori, alianza kusema huku analia, akasema toka amezaliwa mpaka leo miaka 29 hajawahi kulala na mwanamke yani dudu yake haifanyi kazi kabisa. Nilisikitika sana nakulia sikujua nianzie wapi kumshauri. Nilichomwambia anipe muda nitafakari nini cha kumsaidia rafiki yangu kipenzi.

Nimetafakari wee nikaona nije kwa wana JF hawakosi ushauri.
 
Hiyo hiyo noma sana...Jamaa anahitaji maombezi. Sasa siku zote hizo kwa nini hajajitokeza akasaidiwa?? 29 yrs ni mingi ila ngoja wataalamu waje. Hakuna linaloshindikana
 
kama upo siriaz nicheq pm nitamsaidia ndani ya siku saba tu
 
Mi nawalaumu wazazi wake haiwezekani kidume kinafika hadi miaka 29 hasimamishi wakati ilibidi waangalie mienendo ya mtoto wao toka akiwa na miaka 12's...bora dudu liwe linasimama lakini halina uwezo wa kumpa mimba mwanamke kuliko kulala kabisa kama puto..pole yake najua atapata dawa za kubusti ila atafurahi kwa muda mchache tu
 
Ni kitu cha kawaida mbona. Hicho ni kilema amezaliwa nacho. Na Mungu ana makusudi yake. Tatizo naona watu wamekalia kumtibu, anyway labda mjaribu huo utashi wenu. But literally hicho ni sawa na kilema, the same same kama mtu anavozaliwa hana mguu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…