Sijui nitamsaidiaje huyu rafiki yangu, uume wake haufanyi kazi kabisa

Sijui nitamsaidiaje huyu rafiki yangu, uume wake haufanyi kazi kabisa

Mi nawalaumu wazazi wake haiwezekani kidume kinafika hadi miaka 29 hasimamishi wakati ilibidi waangalie mienendo ya mtoto wao toka akiwa na miaka 12's...bora dudu liwe linasimama lakini halina uwezo wa kumpa mimba mwanamke kuliko kulala kabisa kama puto..pole yake najua atapata dawa za kubusti ila atafurahi kwa muda mchache tu
Ujue mara nyingi wazazi wetu wanashindwa kabisa kufuatilia nyendo za mtoto, cha kushangaza wazazi wake wote wawili hawajui, sasa wanamlazisha kuoa lakini anawambia bado. Alikuwa anafanya tiba kwa siri sana huko kwa waganga lkn naona imeshindikana ameona aseme wazi. Inauma sana
 
Dah........!!!!!ni mtihani huo mungu amempa,Allah amjalie subra na ampe siha njema inshaallah,hakika Allah yupo pamoja na wenye kusubiri.
 
Aende hospitalini
Kama nilivyosema mkuu jamaa alikuwa ananificha, inavyooneka kwa mazongira yake hospitali kaende. Kuna siku aliniambia nimsidikize kwa Dr mwaka huyu aliyefungiwa. Nikamuuliza anaumwa nini? Akaniambia tumbo linamsumbua sana kaenda kapewa midawa kibao ya kutumia, nakumbuka alitumia km laki 3.5 kwa zile dawa.
Sasa ndio nimepata akili zile dawa hazikuwa za tumbo kama alivyodai zilikuwa za dushe. Katumia ajapona kabisa sasa kaona ngoja tu aseme
 
Mtafute @mzizimkamvu yeye hajafungiwa. Kama mpaka mzazi hajajua basi sio kawaida hiyo.

Kama unaesema hiki sawa na kilema. Kuna kilema cha hivi kweli? Mi sijawahi sikia
 
Ila ndugu zangu ,kama huna cha kumsaidia huna haja kumdhihaki mleta uzi ,haya ni maisha tu yaweza nawe siku moja ukakutwa na tatizo hilo,na kibaya zaidi bora ya yeye ambae hajawahi kufanya kuliko wewe uliekua unafanya.Nimefarijika kuna watu wameonyesha nia ya kumsaidia ndugu yetu.
 
Ni kitu cha kawaida mbona. Hicho ni kilema amezaliwa nacho. Na Mungu ana makusudi yake. Tatizo naona watu wamekalia kumtibu, anyway labda mjaribu huo utashi wenu. But literally hicho ni sawa na kilema, the same same kama mtu anavozaliwa hana mguu.
Hakuna kilema cha namna hiyo ilo n tatzo
 
duh pole sana....Sasa mpe matumaini rafiki yako,Pengine tatizo lake lina ufumbuzi..
 
Nina rafiki yangu kipenzi tumetoka nae mbali sana siri zangu zake. Tunaisha pamoja kama ndugu sasa. Tulikutana Alevel huko Moshi na ndipo urafiki wetu ulipoanzia, bahat nzuri tulichaguliwa chuo kimoja mim na yeye lkn kozi tofauti. Lkn bado tulikuwa karibu sana tukisaidia.Mpaka tunamaliza chuo.

Lakini kuna jambo moja alikuwa ananificha kwa kipindi kirefu bila kuniambia, lkn kwa tabia yake sikuwah kujua kabisa kama huyu rafiki yang dudu yake aifanyi kazi. Alikuwa karibu na mademu sana na alipendwa na kila demu kwa ucheshi wake, utanashati na vituko. Nilijua jamaa yangu huyu ni kicheche kweli.

Siku zimeenda baada ya kuhitim Mungu alijalia tulipata kazi wote hapa Dar, lkn sector tofauti, yeye akaenda kupanga Mwenge na mim nikapanga zangu Mbagala mji wa kijanja. Mi nikavuta jiko fasta maana wakati nikiwa chuo nilimpa mwanachuo mwenzangu mimba ndie niliyemchukua na kumuweka ndan na harusi ilifanyika na shega alikuwa rafiki yangu.

Sasa siku zikawa zinakwenda sioni shemeji yangu kila nikimuuliza anasema muda bado. Lkn akija kwangu aktazama mwanangu machozi yanamtoka. Nikawa najiuliza kwanini huyu rafiki akimuona mwanangu analia? Kuna siku nikamuuliza sababu nini?

Alichonijibu akaniambia moyo wa mtu kichaka. Ila ipo siku atanimbia. Muda mwingine alikuwa na mawazo sana, nikawa nashindwa kumwelewa jamaa kama maisha anayo mazuri, gari ya kutembelea anayo na hana familia ya kumusumbua sasa tatizo ni nin?

leo kaja kwangu asubuh, akanambia rafiki kuna jambo nataka nikwambia. Akaanza kunipa stori, alianza kusema huku analia, akasema toka amezaliwa mpaka leo miaka 29 hajawahi kulala na mwanamke yaani dudu yake aifanyi kazi kabisa. Nilisikitika sana nakulia sikujua nianzie wapi kumshauri. Nilichomwambia anipe muda nitafakari nini cha kumsaidia rafiki yangu kipenzi. Nimetafakari wee Nikaona nije kwa wana JF hawakosi ushauri.
Ande kwa Dr Mwaka
 
Kama nilivyosema mkuu jamaa alikuwa ananificha, inavyooneka kwa mazongira yake hospitali kaende. Kuna siku aliniambia nimsidikize kwa Dr mwaka huyu aliyefungiwa. Nikamuuliza anaumwa nini? Akaniambia tumbo linamsumbua sana kaenda kapewa midawa kibao ya kutumia, nakumbuka alitumia km laki 3.5 kwa zile dawa.
Sasa ndio nimepata akili zile dawa hazikuwa za tumbo kama alivyodai zilikuwa za dushe. Katumia ajapona kabisa sasa kaona ngoja tu aseme
Huyo ndo bas tena,
 
Tatizo hilo lilianxa lini na lilianza vipi au tangu kutoka tumboni hakuwahi kusimamisha mtambo?
 
Back
Top Bottom