Siku 100 Toka Mauaji Ali Kibao: Ukimya Watanda Juu ya Hatma ya Uchunguzi

Manyanza

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
16,464
Reaction score
35,629
Leo Disemba 16, 2024, zinatimia siku 100 tangu aliyekuwa mwanasiasa mwandamizi wa chama cha upinzani cha CHADEMA, Ali Mohamed Kibao, alipotekwa Septemba 6, 2024, na mwili wake kupatikana Ununio, Dar es Salaam, Septemba 7, 2024, akiwa ameuwawa huku mwili wake ukiwa umeharibiwa vibaya.

Tukio hilo liliteka hisia za wengi, na Septemba 8,2024, siku ambayo ndugu walienda kuutambua mwili wa Kibao katika hospitali ya Mwananyamala, Rais Samia Suluhu Hassan kupitia kurasa zake mitandaoni aliagiza uchunguzi ufanyike.

Soma Pia:
“Nimeagiza vyombo vya uchunguzi kuniletea taarifa ya kina kuhusu tukio hili baya kabisa na mengine ya namna hii haraka. Nchi yetu ni ya kidemokrasia na kila raia ana haki ya kuishi. Serikali ninayoiongoza haivumilii vitendo vya kikatili vya namna hii,”alieleza Rais Samia.
 
Uliamini kuwa rais alikuwa serious na alichosema? Na unaamini kweli alihitaji hiyo taarifa?
 
Huyo aliyeshika beleshi alitakiwa apigwe mawe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…