Manyanza
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 16,464
- 35,629
Leo Disemba 16, 2024, zinatimia siku 100 tangu aliyekuwa mwanasiasa mwandamizi wa chama cha upinzani cha CHADEMA, Ali Mohamed Kibao, alipotekwa Septemba 6, 2024, na mwili wake kupatikana Ununio, Dar es Salaam, Septemba 7, 2024, akiwa ameuwawa huku mwili wake ukiwa umeharibiwa vibaya.
Tukio hilo liliteka hisia za wengi, na Septemba 8,2024, siku ambayo ndugu walienda kuutambua mwili wa Kibao katika hospitali ya Mwananyamala, Rais Samia Suluhu Hassan kupitia kurasa zake mitandaoni aliagiza uchunguzi ufanyike.
Soma Pia:
“Nimeagiza vyombo vya uchunguzi kuniletea taarifa ya kina kuhusu tukio hili baya kabisa na mengine ya namna hii haraka. Nchi yetu ni ya kidemokrasia na kila raia ana haki ya kuishi. Serikali ninayoiongoza haivumilii vitendo vya kikatili vya namna hii,”alieleza Rais Samia.
Tukio hilo liliteka hisia za wengi, na Septemba 8,2024, siku ambayo ndugu walienda kuutambua mwili wa Kibao katika hospitali ya Mwananyamala, Rais Samia Suluhu Hassan kupitia kurasa zake mitandaoni aliagiza uchunguzi ufanyike.
Soma Pia:
“Nimeagiza vyombo vya uchunguzi kuniletea taarifa ya kina kuhusu tukio hili baya kabisa na mengine ya namna hii haraka. Nchi yetu ni ya kidemokrasia na kila raia ana haki ya kuishi. Serikali ninayoiongoza haivumilii vitendo vya kikatili vya namna hii,”alieleza Rais Samia.