Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 6,514
- 15,247
Ningependa Leo nizungumzie maswala ya kiroho na walengwa ambao Nataka niwakumbushe neno la Mungu ni Wale wanao mwamini Mwenyezi Mungu. Kama wewe humwamini Mwenyezi Mungu au unaamini Mungu hayupo basi huu Uzi haukufai.
Mwenyezi Mungu anasema katika Kitabu chake katika Suratul Ibrahim Aya ya 31:
''Waambie waja wangu walio amini, washike Sala, na watoe katika tulivyo waruzuku, kwa siri na dhaahiri, kabla haijafika Siku isiyo kuwa na biashara wala urafiki.''
Mwenyezi Mungu katika Kitabu chake amekuwa na kawaida ya kuongea na watu Kwa daraja zao, ndio maana kuna Aya anazungumza Kwa kusema Enyi watu na Aya nyingine anasema Enyi mlioamini. Anapozungumzia Enyi watu mara nyingi huzungumza na viumbe wake wote wanao mwamini yeye na wasio mwamini yeye na wanaomini Mungu zaidi ya mmoja. Na mara nyingi huwapa hoja mbali mbali za kufikirisha akili zao na bongo zao juu ya kuumbwa Kwa ulimwengu na viumbe wake pamoja na yaliyomo ndani yake, je hayo wanayo yaona hayatoshi kuwafanya wao kutafakari na kuona kuwa hayo hayakutokea bure Tu Ila kuna Mwenyezi Mungu aliyeumba mambo yote hayo? Huo ni mfano mmoja Tu nilio ugusa hapo.
Na anapo ongea na walioamini, anaongea na watu ambao tayar wamemwamini Mungu Mmoja na hawa ndio wamesalimika,kwasababu Mwenyezi Mungu hana ushirika wala usaidizi toka Kwa kiumbe kingine chochote kile, yeye ndio mkuu na ndiye aliye juu, sifa zake amezieleza vizuri katika Suratul Bakara Aya ya 255:
''Mwenyezi Mungu - hapana mungu ila Yeye Aliye hai, Msimamia mambo yote milele. Hashikwi na usingizi wala kulala. Ni vyake pekee vyote viliomo mbinguni na duniani. Ni nani huyo awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao; wala wao hawajui chochote katika vilio katika ujuzi wake, ila kwa atakalo mwenyewe. Enzi yake imetanda mbinguni na duniani; na wala haemewi na kuvilinda hivyo. Na Yeye ndiye aliye juu, na ndiye Mkuu.''
Baada ya kuona sifa zake..turudi kwenye lengo kuu la Aya ambayo nimeshaitaja awali. Kwanza Mwenyezi Mungu anasema Waambie waja wangu walioamini wasimamishe Sala, ndugu zangu katika Imani, Sala au Swala ndio amali au kitendo cha Kwanza kuhesabiwa siku ya hukumu,hapo unaona ni jinsi gani Swala ilivyo na umuhimu mkubwa mbele ya Allah, na katika nguzo tano ambazo Uislamu umejengwa juu yake basi Swala ndio Nguzo ya pili kusimikwa mara baada Tu ya kukiri kuwa Hapana Mola apasae KUABUDIWA Kwa haki isipokuwa Allah/Mwenyezi Mungu. Na anayesimamisha au anayedumu na ibada hii basi hakika amesimamisha Dini,na ikasemwa pia tofauti ya walioamini na waliokufuru ni Swala.
Na Mtume (rehma na Amani iwe juu yake) akasema '' mfano wa swala tano ni kama mtu ambaye nyumba yake ipo karibu na mto, na anaoga mara tano Kwa siku. Je, mtu kama huyo atakuwa na uchafu mwilini mwake?'' Hapo inaonyesha hakika kila kipindi kimoja cha swala kinafuta madhambi ya mja wa Allah,hakika amali hii ni muhimu hivyo hatuna budi kujitahidi kuifanya kwa uwezo wetu wote Mjumbe wa Allah alisema ukimuona mtu anapenda kwenda msikitini basi yatosha kusema huyu mtu ana Imani.
Pili Mwenyezi Mungu anasema tutoe katika vile alivyoturuzuku Kwa Siri na dhahiri...ni mtu asiye mwamini Mwenyezi Mungu Tu ndio anaamini kuwa mafanikio aliyonayo kayapata Kwa ujanja wake au Kwa maarifa yake,lakini mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu hakika anajua vyote alivyonavyo amepewa na Mola wake mlezi,na hivyo Hana budi kutoa sadaka,zaka na kuwasaidia wenye uhitaji kwakuwa anajua ndani ya nafsi yake kuwa IPO siku ataulizwa juu ya neema aliyopewa.
Na sadaka waeza Toa Kwa Siri au Kwa dhahiri lakini kitu kibaya ni kutoa Kwa kutaka Sifa mbele za watu uonekane kuwa wewe ni mtoaji mzuri,hapo hautapata malipo toka Kwa Mwenyezi Mungu kwakuwa ulikusudia ktk moyo wako usifiwe na watu,lkn kama ulitoa mbele za watu Kwa Nia ya kutaka radhi za Mwenyezi Mungu basi hakika utapata malipo toka Kwa Mola wako.
Lakini tunaambiwa kutoa sadaka Kwa Siri ndio Bora zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu,na hapo unakuja ule msemo kuwa ukitoa sadaka Kwa mkono wa Kulia basi mkono WA kushoto usijue,maana halisi ndiyo utoe Kwa Siri sadaka yako...ingawa baadhi ya watu unakuta wakitoa hela zao msikitini basi daah wanazikunja hizo hela mpaka zinakosa hewa! Yaani kama zingekuwa zinapumua basi zingekosa pumzi na kufa hahah! Kutokutoa Kwa Siri ni kama vile unatoa huku unatangaza Kwa watu,Mimi bwana nimetoa shilingi kadhaa au unamuona Fulani alikuwa hana hela ya kula ujue Mimi ndio nimemsaidia,hakika sadaka za namna hiyo hazina malipo mbele ya Mwenyezi Mungu hata kidogo.
Mwisho Mwenyezi Mungu anawaonya waumini kuwa washike sala na kutoa katika vile walivyoruzukiwa kabla haijaja siku isiyo na biashara wala Urafiki, tunajua hapa duniani huwa tunanufaishana na kusaidiana Kwa kuwa ni marafiki,kuna watu hawafungwi jela kwasababu ya Urafiki,hawalipi Kodi stahiki kwasababu ya Urafiki, wanafanya dhuluma mbali mbali kisa Tu Wana Urafiki na polisi hivyo huwezi kuwagusa,yote hayo siku ya hukumu hakuna habari hizo....
Ukija upande WA biashara nako hivyo hivyo,hapa duniani ndio sehemu nzur ya kufanya biashara na Mwenyezi Mungu,ukitenda mema utalipwa mema zaidi ya hayo uliyotenda,ni sehemu ya kuchuma thawabu zitakazo kufaa huko mbele ya safari,lakini kama hakufanya biashara hiyo wakati huko hai basi siku hiyo ya hukumu hakutakuwa na nafasi nyingine ya kuchuma mema.
Namalizia na dua ya Nabii Ibrahim pale alipo muomba Mola wake Mlezi amsaidie kusimamisha Sala pamoja na familia yake:
"Mola wangu Mlezi! Nijaalie niwe mwenye kushika Sala, na katika dhuriya zangu pia. Ewe Mola wetu Mlezi, na ipokee dua yangu."
Surah Ibrahim :40
Ni hayo Tu.
Mwenyezi Mungu anasema katika Kitabu chake katika Suratul Ibrahim Aya ya 31:
''Waambie waja wangu walio amini, washike Sala, na watoe katika tulivyo waruzuku, kwa siri na dhaahiri, kabla haijafika Siku isiyo kuwa na biashara wala urafiki.''
Mwenyezi Mungu katika Kitabu chake amekuwa na kawaida ya kuongea na watu Kwa daraja zao, ndio maana kuna Aya anazungumza Kwa kusema Enyi watu na Aya nyingine anasema Enyi mlioamini. Anapozungumzia Enyi watu mara nyingi huzungumza na viumbe wake wote wanao mwamini yeye na wasio mwamini yeye na wanaomini Mungu zaidi ya mmoja. Na mara nyingi huwapa hoja mbali mbali za kufikirisha akili zao na bongo zao juu ya kuumbwa Kwa ulimwengu na viumbe wake pamoja na yaliyomo ndani yake, je hayo wanayo yaona hayatoshi kuwafanya wao kutafakari na kuona kuwa hayo hayakutokea bure Tu Ila kuna Mwenyezi Mungu aliyeumba mambo yote hayo? Huo ni mfano mmoja Tu nilio ugusa hapo.
Na anapo ongea na walioamini, anaongea na watu ambao tayar wamemwamini Mungu Mmoja na hawa ndio wamesalimika,kwasababu Mwenyezi Mungu hana ushirika wala usaidizi toka Kwa kiumbe kingine chochote kile, yeye ndio mkuu na ndiye aliye juu, sifa zake amezieleza vizuri katika Suratul Bakara Aya ya 255:
''Mwenyezi Mungu - hapana mungu ila Yeye Aliye hai, Msimamia mambo yote milele. Hashikwi na usingizi wala kulala. Ni vyake pekee vyote viliomo mbinguni na duniani. Ni nani huyo awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao; wala wao hawajui chochote katika vilio katika ujuzi wake, ila kwa atakalo mwenyewe. Enzi yake imetanda mbinguni na duniani; na wala haemewi na kuvilinda hivyo. Na Yeye ndiye aliye juu, na ndiye Mkuu.''
Baada ya kuona sifa zake..turudi kwenye lengo kuu la Aya ambayo nimeshaitaja awali. Kwanza Mwenyezi Mungu anasema Waambie waja wangu walioamini wasimamishe Sala, ndugu zangu katika Imani, Sala au Swala ndio amali au kitendo cha Kwanza kuhesabiwa siku ya hukumu,hapo unaona ni jinsi gani Swala ilivyo na umuhimu mkubwa mbele ya Allah, na katika nguzo tano ambazo Uislamu umejengwa juu yake basi Swala ndio Nguzo ya pili kusimikwa mara baada Tu ya kukiri kuwa Hapana Mola apasae KUABUDIWA Kwa haki isipokuwa Allah/Mwenyezi Mungu. Na anayesimamisha au anayedumu na ibada hii basi hakika amesimamisha Dini,na ikasemwa pia tofauti ya walioamini na waliokufuru ni Swala.
Na Mtume (rehma na Amani iwe juu yake) akasema '' mfano wa swala tano ni kama mtu ambaye nyumba yake ipo karibu na mto, na anaoga mara tano Kwa siku. Je, mtu kama huyo atakuwa na uchafu mwilini mwake?'' Hapo inaonyesha hakika kila kipindi kimoja cha swala kinafuta madhambi ya mja wa Allah,hakika amali hii ni muhimu hivyo hatuna budi kujitahidi kuifanya kwa uwezo wetu wote Mjumbe wa Allah alisema ukimuona mtu anapenda kwenda msikitini basi yatosha kusema huyu mtu ana Imani.
Pili Mwenyezi Mungu anasema tutoe katika vile alivyoturuzuku Kwa Siri na dhahiri...ni mtu asiye mwamini Mwenyezi Mungu Tu ndio anaamini kuwa mafanikio aliyonayo kayapata Kwa ujanja wake au Kwa maarifa yake,lakini mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu hakika anajua vyote alivyonavyo amepewa na Mola wake mlezi,na hivyo Hana budi kutoa sadaka,zaka na kuwasaidia wenye uhitaji kwakuwa anajua ndani ya nafsi yake kuwa IPO siku ataulizwa juu ya neema aliyopewa.
Na sadaka waeza Toa Kwa Siri au Kwa dhahiri lakini kitu kibaya ni kutoa Kwa kutaka Sifa mbele za watu uonekane kuwa wewe ni mtoaji mzuri,hapo hautapata malipo toka Kwa Mwenyezi Mungu kwakuwa ulikusudia ktk moyo wako usifiwe na watu,lkn kama ulitoa mbele za watu Kwa Nia ya kutaka radhi za Mwenyezi Mungu basi hakika utapata malipo toka Kwa Mola wako.
Lakini tunaambiwa kutoa sadaka Kwa Siri ndio Bora zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu,na hapo unakuja ule msemo kuwa ukitoa sadaka Kwa mkono wa Kulia basi mkono WA kushoto usijue,maana halisi ndiyo utoe Kwa Siri sadaka yako...ingawa baadhi ya watu unakuta wakitoa hela zao msikitini basi daah wanazikunja hizo hela mpaka zinakosa hewa! Yaani kama zingekuwa zinapumua basi zingekosa pumzi na kufa hahah! Kutokutoa Kwa Siri ni kama vile unatoa huku unatangaza Kwa watu,Mimi bwana nimetoa shilingi kadhaa au unamuona Fulani alikuwa hana hela ya kula ujue Mimi ndio nimemsaidia,hakika sadaka za namna hiyo hazina malipo mbele ya Mwenyezi Mungu hata kidogo.
Mwisho Mwenyezi Mungu anawaonya waumini kuwa washike sala na kutoa katika vile walivyoruzukiwa kabla haijaja siku isiyo na biashara wala Urafiki, tunajua hapa duniani huwa tunanufaishana na kusaidiana Kwa kuwa ni marafiki,kuna watu hawafungwi jela kwasababu ya Urafiki,hawalipi Kodi stahiki kwasababu ya Urafiki, wanafanya dhuluma mbali mbali kisa Tu Wana Urafiki na polisi hivyo huwezi kuwagusa,yote hayo siku ya hukumu hakuna habari hizo....
Ukija upande WA biashara nako hivyo hivyo,hapa duniani ndio sehemu nzur ya kufanya biashara na Mwenyezi Mungu,ukitenda mema utalipwa mema zaidi ya hayo uliyotenda,ni sehemu ya kuchuma thawabu zitakazo kufaa huko mbele ya safari,lakini kama hakufanya biashara hiyo wakati huko hai basi siku hiyo ya hukumu hakutakuwa na nafasi nyingine ya kuchuma mema.
Namalizia na dua ya Nabii Ibrahim pale alipo muomba Mola wake Mlezi amsaidie kusimamisha Sala pamoja na familia yake:
"Mola wangu Mlezi! Nijaalie niwe mwenye kushika Sala, na katika dhuriya zangu pia. Ewe Mola wetu Mlezi, na ipokee dua yangu."
Surah Ibrahim :40
Ni hayo Tu.