Siku nasikia DSM, nilijua kuna minazi mingi kuliko mti wowote, cha ajabu miarobaini ndio imejaa kila kona

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
wakuu mara ya kwanza nasikia dar es salaam.
nilijua ni marufuku kula wali bila nazi.
nilijua kila hatua tano, unabishana na minazi ya kutosha.
Nilijua Minazi ndio ilipelekea nembo ya jiji kuwa minazi.

cha ajabu nimekagua na kuzunguka kona nyingi miti ya Mwarobaini ni mingi kuliko hata minazi.
sijajua tatizo ni nini, miarobaini hawakuiona? au kwa sababu minazi inasura nzuri.
 
Si kweli we utakuwa unapita sana mitaa ya kivule,chanika,mliganzila na mitaa ya njee ya mji.
 


Mkuu unachosema kina karibia ukweli. By the way siku za nyuma Dar ilikuwa na minazi, miembe na mikorosho kila baada ya nyumba kwa sababu ilikuwa kama mazao. lakini hivi sasa miti ya miarobaini inachukua nafasi Kama miti ya kivuli na mfumuko wa ujenzi wa nyumba za makazi pia umesababisha miti hiyo kukatwa.
Lakini inabakii kuwa alama ya Dar esalaam kiasili
 
Nazi zipo shamba jamani, mjini zinaua watu, Ile nazi ikikuangukia ikagonga medula umekwenda. Zinapasua vioo vya magari hata bati hutoboka.
 
Mkuu ulikuwa umepotelea wapi?
Siku nyingi sikuoni.
 
Mkuu ubarikiwe maana hata mimi nilitaka nijibu kama wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…