Siku tukijua wanaotusababishia maisha kuwa magumu

Siku tukijua wanaotusababishia maisha kuwa magumu

Burkinabe

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2023
Posts
2,354
Reaction score
4,024
Asalaam Aleykum wana JF.

Moja kwa moja niingie kwenye mada.

Kila siku mambo yanazidi kuwa magumu kwa walio wengi kutokana na gharama za maisha kupanda kila uchao ilhali kipato kikiwa palepale au kikipungua. Hii inawahusu hata wafanyakazi wa umma na sekta binafsi ambao kiukweli hawajaongezewa mshahara kwa muda mrefu.

Ninapoongelea gharama za maisha ni kuanzia gharama za kununua chakula, mavazi, kodi ya nyumba, tozo, usafiri, gharama za matibabu n.k.

Kiukweli ndani ya muda wa miaka 2 hadi 3 kumekuwa na mfumko wa bei ambao hatujawahi kuushuhudia kwa miaka mingi huku viongozi wetu wakituaminisha sababu mbalimbali ambazo kwa sehemu kubwa nyingi hazina mashiko.

Nchi nchi yetu ina vyanzo vingi sana vya mapato kurokana na wingi wa raslimali tulizo nazo mfano ukiwa ni bandari, madini, mbuga za wanyama n.k.

Lakini pia kuna mashirika mengi ambayo kama yangekuwa na usimamizi mzuri, basi Tanzania ingekuwa katika viwango vya juu sana kimaendeleo. Lakini cha kusikitisha ni kwamba haya mashirika badala ya kuingiza faida, yamekuwa kinara kwa kuiingizia serikali hasara! Yaani badala ya yenyewe kutoa fedha kwa serikali, serikali ndo inatoa fedha kuyahudumia tena kwa kodi za wananchi wanyonge kabisa wa nchi hii!

Hii haikubaliki kabisa. Kwa sehemu kubwa ya wanaotusababishia maisha kuwa magumu ni wale ambao tumewaamini na kuwapa mamlaka ya kutusimamia.

Hivyo, siku tukijitambua na kuwaambia ukweli, hapo ndipo hali yetu ya maisha pia itabadilika kwa wema kuliko ilivyo sasa.

Mungu ibariki Tanzania,

Amin.
 
Watanzania ni watu wa amani. Tuilinde amani ya nchi yetu.

Mkitutoa madarakani kisa tunakula hovyo kodi zenu na hatuwaletei maendeleo, mkaipoteza amani mtafaidi nini?

Mtuache tule kwa urefu wa kamba zetu, watoto wetu wasome shule zenye mitaala relevant, wakimaliza shule tuwape kazi zenye mishahara minono, nyie mgombanie udaktari, polisi na ualimu. Sisi tutahakikisha mnaishi kwa amani.

Haya mambo ya gesi, sijui madini na vivutio vya utalii aliweka mungu sio nyie wananchi, hata hivyo tukiwapa nyie madini mtafanyia nini?

Zaidi ya yote mtuombee, kazi ya kujilimbikizia mali na kulinda amani sio ndogo, mtuombee sana wananchi wetu. Asante kwa kunielewa
 
Watanzania ni watu wa amani. Tuilinde amani ya nchi yetu.

Mkitutua madarakani kisa tunakula hovyo kodi zenu na hatuwaletei maendeleo, mkaipoteza amani mtafaidi nini?

Mtuache tule kwa urefu wa kamba zetu, watoto wetu wasome shule zenye mitaala relevant, wakimaliza shule tuwape kazi zenye mishahara minono, nyie mgombanie udaktari na ualimu. Sisi tutahakikisha mnaishi kwa amani.

Haya mambo ya gesi, sijui madini na vivutio vya utalii aliweka mungu sio nyie wananchi, hata hivyo tukiwapa nyie madini mtafanyia nini?

Zaidi ya yote mtuombee, kazi ya kujilimbikizia mali na kulinda amani sio ndogo, mtuombee sana wananchi wetu. Asante kwa kunielewa
🤣
 
Pole Sana. Ngoja tusubiri kizazi kilicho Bora zaidi yako katika kufanya maamuz. Ila usijidanganye kuwa KIONGOZI Yuko Kwa maslahi yako. Hata mwenye nia simuoni.
 

Attachments

  • JamiiForums1374067312.jpeg
    JamiiForums1374067312.jpeg
    43.1 KB · Views: 6
Kulijua tatizo ndio kujitambua kwenyewe.

Shida ni kwamba watanzania ni waoga kuchukua hatua stahiki.
 
Ufukara wawatanzania ni mtaji mzuri kwa ccm
Ukishakuwa fukara ni ngumu kufuatilia haki zako
Ukishakuwa fukara ni ngumu kuhoji upigaji unaofanyika

Watu kama Hawa ukimpa 5000 yupo tayari kuja kwenye mkutano
 
Mnajua sana ila sababu hamna mmoja, mtaendelea kupigika na vizazi vyenu
Tufanyeje ili tuwe na umoja?
Maana najua na wewe pia unaumizwa na ali hii ya watu wachache kujinufaisha ilhali wengi wakizidi kudidimia kila uchao!
 
Ufukara wawatanzania ni mtaji mzuri kwa ccm
Ukishakuwa fukara ni ngumu kufuatilia haki zako
Ukishakuwa fukara ni ngumu kuhoji upigaji unaofanyika

Watu kama Hawa ukimpa 5000 yupo tayari kuja kwenye mkutano
Ufukara hudumaza uwezo wa kufikiri.
Nalubaliana na wewe Mkuu.
Lakini tuwafanyeje hawa wanaotusababishia ufukara huu ?!
 
Tufanyeje ili tuwe na umoja?
Maana najua na wewe pia unaumizwa na ali hii ya watu wachache kujinufaisha ilhali wengi wakizidi kudidimia kila uchao!
Ni rahis sana lazima jamii nzima ikubali kuondokana na ujinga ( hii ni turufu kubwa wanayoitumia) , vijana mnaowasomesha warudi vijijini kutoa elimu. Jamii iamke

Familia zijitoe kutoka kwenye uchawa , uchawa upigwe vita kuanzia ngazi ya familia.

Ujinga ukipungua hata viongoz hawatowachukulia poa otherwise endeleeni kuumia tu
 
Watanzania ni watu wa amani. Tuilinde amani ya nchi yetu.

Mkitutua madarakani kisa tunakula hovyo kodi zenu na hatuwaletei maendeleo, mkaipoteza amani mtafaidi nini?

Mtuache tule kwa urefu wa kamba zetu, watoto wetu wasome shule zenye mitaala relevant, wakimaliza shule tuwape kazi zenye mishahara minono, nyie mgombanie udaktari na ualimu. Sisi tutahakikisha mnaishi kwa amani.

Haya mambo ya gesi, sijui madini na vivutio vya utalii aliweka mungu sio nyie wananchi, hata hivyo tukiwapa nyie madini mtafanyia nini?

Zaidi ya yote mtuombee, kazi ya kujilimbikizia mali na kulinda amani sio ndogo, mtuombee sana wananchi wetu. Asante kwa kunielewa
Mkuu umeongea kwa uchungu sana, lakini hivi ndo vichaka wanavyotumia viongozi wetu kuendelea kujinufaisha wao na familia zao.

Zaidi zaidi watakwambia fanyeni kazi maana hakuna serikali itakayokuletea chakula mezani!!

Sasa swali la msingi, Je, ni kweli hatufanyi kazi?!

Kazi tunafanya sana, tena sana lakini kinachopatikana chote kinakombwa na serikali kwa njia ya tozo na kodi mbalimbali achilia mbali mfumko wa bei unaosababishwa na usimamizi mbovu wa hawa hawa viongozi waliojawa na kejeli kwa raia!
 
Mkuu umeongea kwa uchungu sana, lakini hivi ndo vichaka wanavyotumia viongozi wetu kuendelea kujinufaisha wao na familia zao.
Zaidi zaidi watakwambia fanyeni kazi maana hakuna serikali itakayokuletea chakula mezani!!
Sasa swali la msingi, Je, ni kweli hatufanyi kazi?!
Kazi tunafanya sana, tena sana lakini kinachopatikana chote kinakombwa na serikali kwa njia ya tozo na kodi mbalimbali achilia mbali mfumko wa bei unaosababishwa na usimamizi mbovu wa hawa hawa viongozi waliojawa na kejeli kwa raia!
Mwananchi wa kawaida amepewa tunu iitwayo amani, kiongozi amejipatia tunu iitwayo utajiri.

Solution ni mbili tu, moja: serikali iruhusu wananchi kumiliki silaha kisha tutadeal nao in a hard way

Mbili: kwakuwa viongozi wanalinda amani kwa kula kodi zetu kwa ulafi, jeshi liache kuwalinda viongozi. Lilinde maslahi ya wananchi na raslimali zao

Mambo ya kusema watz ni waoga, wewe utasimama mbele ya mtu mwenye manati ya mzungu na mabomu ya rambo?

Mimi naona tuendelee kuwaombea viongozi wetu, wapate maisha marefu na amani idumu. Kidumu chama cha mapinduzi. Wote tuseme tawilee
 
Asalaam Aleykum wana JF.

Moja kwa moja niingie kwenye mada.

Kila siku mambo yanazidi kuwa magumu kwa walio wengi kutokana na gharama za maisha kupanda kila uchao ilhali kipato kikiwa palepale au kikipungua. Hii inawahusu hata wafanyakazi wa umma na sekta binafsi ambao kiukweli hawajaongezewa mshahara kwa muda mrefu.

Ninapoongelea gharama za maisha ni kuanzia gharama za kununua chakula, mavazi, kodi ya nyumba, tozo, usafiri, gharama za matibabu n.k.

Kiukweli ndani ya muda wa miaka 2 hadi 3 kumekuwa na mfumko wa bei ambao hatujawahi kuushuhudia kwa miaka mingi huku viongozi wetu wakituaminisha sababu mbalimbali ambazo kwa sehemu kubwa nyingi hazina mashiko.

Nchi nchi yetu ina vyanzo vingi sana vya mapato kurokana na wingi wa raslimali tulizo nazo mfano ukiwa ni bandari, madini, mbuga za wanyama n.k.

Lakini pia kuna mashirika mengi ambayo kama yangekuwa na usimamizi mzuri, basi Tanzania ingekuwa katika viwango vya juu sana kimaendeleo. Lakini cha kusikitisha ni kwamba haya mashirika badala ya kuingiza faida, yamekuwa kinara kwa kuiingizia serikali hasara! Yaani badala ya yenyewe kutoa fedha kwa serikali, serikali ndo inatoa fedha kuyahudumia tena kwa kodi za wananchi wanyonge kabisa wa nchi hii!

Hii haikubaliki kabisa. Kwa sehemu kubwa ya wanaotusababishia maisha kuwa magumu ni wale ambao tumewaamini na kuwapa mamlaka ya kutusimamia.

Hivyo, siku tukijitambua na kuwaambia ukweli, hapo ndipo hali yetu ya maisha pia itabadilika kwa wema kuliko ilivyo sasa.

Mungu ibariki Tanzania,

Amin.
Ongeza Juhudi katika kufanya kazi kwani mtaji ulionao ni nguvu zako mwenyewe 🐒
 
Watanzania ni watu wa amani. Tuilinde amani ya nchi yetu.

Mkitutoa madarakani kisa tunakula hovyo kodi zenu na hatuwaletei maendeleo, mkaipoteza amani mtafaidi nini?

Mtuache tule kwa urefu wa kamba zetu, watoto wetu wasome shule zenye mitaala relevant, wakimaliza shule tuwape kazi zenye mishahara minono, nyie mgombanie udaktari, polisi na ualimu. Sisi tutahakikisha mnaishi kwa amani.

Haya mambo ya gesi, sijui madini na vivutio vya utalii aliweka mungu sio nyie wananchi, hata hivyo tukiwapa nyie madini mtafanyia nini?

Zaidi ya yote mtuombee, kazi ya kujilimbikizia mali na kulinda amani sio ndogo, mtuombee sana wananchi wetu. Asante kwa kunielewa
🫢🫢🫢
 
Mimi nawajua ni ccm. Na ndiyo siku zote huwa ninawaombea tu washindwe na kulegea.
 
Back
Top Bottom