Siku ya Baba Duniani: Kwanini katika familia nyingi akina baba hutangulia kufariki?

Siku ya Baba Duniani: Kwanini katika familia nyingi akina baba hutangulia kufariki?

Walker Water

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2022
Posts
842
Reaction score
3,357
Leo ikiwa ni siku ya Baba duniani, naomba tutafakari swali hili na kujijibu. Kwanza natoa angalizo kuwa huwa napenda sana kuangazia sababu za kiroho katika kila jambo, hivyo usipende sana kusoma mada zangu kimwili maana itakuwia vigumu kidogo kuelewa. Utangulizi; Ukifanya uchunguzi kama niliofanya mimi utagundua kuwa idadi kubwa ya wanaotangulia kufariki katika familia ni wababa.

Zipo sababu nyingi zinazochangia hali hii, na nyingi ni za kiroho. Nitaangazia chache za kimwili na za kiroho na nyingine wadau mtaongezea. KIMWILI. a) Kibaolojia. Ukiangalia kwa kawaida wanaume wengi hupenda kuoa wanawake wenye umri mdogo kuliko wao. Kibaolojia seli ambazo ndizo kiini cha uhai hutangulia kufa mapema kwa kadri umri wa mtu unavyozidi kuongezeka, na ukizingatia wengi wetu elimu ya lishe hatuna na hali ya uchumi pia si nzuri. b) Kisaikolojia. Wanawake wengi kisaikolojia hujiona duni mbele ya wanaume na hivyo huweza kulia hadharani (kulia ni tiba), kutoa maneno ya uchungu moyoni na kuwa na washauri wengi na watetezi hivyo kupata faraja zaidi ya mwanaume. C) Kiuchumi.

Hali ya uchumi ya mwanaume ikiwa mbaya ndani ya familia, maneno ya mkewe na malalamiko ya watoto yanatosha kukupa mawazo ambayo yanaweza kukumaliza mapema sana. KIROHO. Hapa jibu ni moja tu, mwanaume kushindwa kusimama katika NAFASI yake. Kwa kawaida mwanaume ni kiongozi na mtawala wa mwanamke katika kila kitu ( kumbuka tunazungumzia kiroho).

Mwanaume ukishindwa tu kushika hii nafasi vizuri na zana zote za utawala upewa, kama akili za juu, maono na maneno yenye mamlaka, basi tambua kabisa itakupasa tu ufe mapema ili uondoe kikwazo katika nafasi hiyo na mwingine aitumie kuitawala. Nafasi hii inatawaliwa vizuri kwa kutumia AKILI. Ukiona mwanaume anatawala nafasi hii kwa kutumia nguvu (udikteta) tambua kuwa akili zake zimeharibika.

Kwa nini nakazania sana "akili!?", Ni kwa sababu akili nzuri za mwanaume ndizo pekee zenye uwezo wa kumshepu mwanamke kadri unavyopenda wewe mume wake. Huwa nashangaa sana kuona wanaume wanalalamikia wake zao kuwa hawapo vizuri kitabia au kimuonekano!, sijui kama huwa wanajua kuwa wanajishangaa wenyewe na kujilalamikia!, yaani wewe unamshepu mke wako kadri unavyopenda wewe alafu uanajishangaa tena!

Ni sawa na kumlalamikia mwanamke kwa nini anapata watoto wa njisi moja tu wakati wewe ndiye mwenye gameti XY na yeye ni mpokeaji tu ( ina maana kiroho ya kuwa mwanamke kazi yake ni kupokea tu uongozi kutoka kwako). Mwanamke ameletwa kwako kula raha tu na kukusaidia kukubebea watoto unaotaka na uwezo wa kuwalea na kukusaidia katika ushauri na kwenye mambo madogo madogo.

Laiti wanaume tungeitambua na kusimama katika nafasi hii ya dhahabu tuliyopewa, hakika hakuna mwanamke angetamani kuwa mwanaume na kutudharau. Sasa tunaitimisha mada kwa kusema kuwa, nafasi ni "majukumu", endapo mwanaume utashindwa kutawala nafasi hii ( majukumu yako), mwanamke kazi yake ni kupeleka malalamiko yake mbele ya "KITI KIKUU" kwa kujua au kutokujua kuwa anakuombea ufe mapema huku akisindikizwa na watoto kama mashaidi.

Endapo ushaidi ukithibitika ni wa kweli, basi ataulizwa swali moja tu mara tatu kwa nyakati tofauti, ya kuwa "tukimwondoa huyu wewe utaweza kushika hii nafasi kuendesha familia?" akijibu ndiyo, tunakupoteza kweli. Ukiona mwanamke ameweza kuendesha familia baada ya mume wake kufa, tambua kuwa huyo mwanaume siku yake sahihi ilikuwa imefika au alipenda tu yeye atangulie au alikuwa kikwazo kweli kwa mkewe. Ukiona mwanamke ameshindwa kuendesha familia baada ya mumewe kufa, tambua kuwa huyo mwanamke alikurupuka kumshtaki mumewe kwa tamaa ya hiyo nafasi akifikiri ataweza kuitumia kirahisi. Naomba nikuulize hili swali, "wewe unafikiri kati ya mtawala na mtawaliwa yupi kikawaida angepaswa kutangulia mapema?".
 
Nilipoanza kusoma tu, macho yakaanza kuniuma kwasabu maandishi yameungana kama mistari mingiii iliyo jipanga..
Ila zamamani ulikua unakuta baba mmoja ana watoto wanne.
Skuizi unakuta baba wanne wana mtoto mmoja....🤣labda ndio mabadiliko ya tabia ya nchi...teh😜
 
Wanasema ukipiga bao moja unapunguza masaa maatatu ya kuishi duniani. Ila sijui sana

Wakuu naombeni mukanipie kura shindano linakaribia kufungwa
 
Mikikimikiki yote ya dunia hii anapambana nayo Baba, angalia hapo Dar es salaam idadi ya wapiga debe na makondakta wa daladala wanaume ni wangapi na wanaume ni wangapi

JWTZ wamepeleka jeshi DRC kupambana na M23 angalia idadi ya akinamama Vs akinababa.

Mida hii tunavyoongea huko baharini deep sea mameli yanapigwa na mawimbi kaangilie idadi ya akina Baba Vs idadi ya akinamama.

Mida hii jua kali linawaka nenda chini ya migodi kaangalie akina mama ni wangapi na akinababa NI wangapi?

Kifupi Wanaume ndio wapo exposed kwenye hatari nyingi zinazowafanya miili yao kuchoka au hata kuumia na kufa mapema.

Gari inayotembea 1000km kwa siku na lile linalotembea 5km kwa siku sijui ni lipi litachoka mapema na kuwa scrap.
 
Back
Top Bottom