Siku ya kisukari duniani

Fadhili Paulo

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2011
Posts
3,211
Reaction score
993
Wakuu habari zenu humu ndani,

Leo ni siku ya kisukari duniani, jana wakati nikitazama kipindi cha Hot Mix cha EATV nilimsikia daktari akisema mpaka sasa hakuna dawa ya kisukari na akaongeza hata hao wa tiba mubadala bado hawawezi kuponya kisukari. Je:

1. Ni kweli kisukari hakitibiki hata kwa tiba mubadala?
2. Hakuna mtu humu jamvini amepona kisukari?.

Karibuni tujadili.
 
Kisukari kinatibika ikiwa kiko katika hatua za mwanzo kabisa, na dawa kuu ni kufuata masharti. Masharti ndio dawa kuu ya kisukari mimi ninacho na mara ya kwanza nilikuwa na 32.7 ikawa nikikijitahidi kushusha inafika 28 ila baada ya kuanza kufuata masharti ilishuka na kufika 11 hadi 2 ambapo ilikuwa mbaya zaidi. Ila kwa sasa nashukuru bada ya kutumia Dawa aina ya Andybete ya Kampuni ya Neptunus inakuwa 4.5 hadi 6
 
tufanye mazoezi jamani kupunguza uwezakano wa kupata ugonjwa huu. Pole kwa wote wenye ugonjwa, zingatieni masharti.
 
kwa hiyo umepona?
 

Hiyo dawa ni vidonge au sondano?na hapa Tanzania vinapatikana wapi?Mzazi wangu anasumbuliwa sana na kisukari,labda dawa hii inaweza kumfaa.
 
Wakuu,
Inaonekana hakuna ambaye ameshapona kisukari humu mpaka sasa. Sasa natoa offer, mtu yeyote anayesumbuliwa kisukari aniandikie katika fadhilipaulo@gmail.com tuwasiliane na tuone namna gani unaweza kuondokana na tatizo hili. Karibuni.
 
Wakuu,
Inaonekana hakuna ambaye ameshapona kisukari humu mpaka sasa. Sasa natoa offer, mtu yeyote anayesumbuliwa kisukari aniandikie katika fadhilipaulo@gmail.com tuwasiliane na tuone namna gani unaweza kuondokana na tatizo hili. Karibuni.

Aina hii ya kupeana matumaini hewa ni mbaya sana. Naamini hauna kisukari, mimi ninacho (IDDM) kwa miaka 12 sasa. Don't do this, you know better!
 
Aina hii ya kupeana matumaini hewa ni mbaya sana. Naamini hauna kisukari, mimi ninacho (IDDM) kwa miaka 12 sasa. Don't do this, you know better!

Mkuu, usiwe mtu wa kukata tamaa, wewe niandikie shida ipo wapi?.
 
Tupe siri ya hayo mafanikio mujydebubyz, ni masharti gani unayazungumzia? maana kutoka ishirini naa mpaka 2 inaonesha mafanikio makubwa sana, ilikuchukua mda gani kufikia hayo mafanikio?
 
Hajapona, ila anaendelea kutumia dawa kwa ajili ya kucontrol sukari. Akiacha hapo anarudi upya.

Kisukari ni ugonjwa hatari. Mungu atuepushie.

Je, unajua kuwa unene kupindukia, kutofanya mazoezi, kunywa pombe kupita kiasi, na kuvuta sigara ni mojawapo ya mambo yanayokuweka hatarini sio kupata kisukari tu bali hata kansa na magonjwa mengine yasiyo ya kuambukizwa?
kwa hiyo umepona?
 
KISUKARI! Ni nini? Inakuwaje ata aambiwe kuwa ana ugonjwa huu? Nini kinatokea kitaalamu mwilini, mtu kupata ugonjwa huu? Mtu awezaje kujikinga nao? Twaambiwa kwamba 2030 kwa Afrika utakua kwa 160% (Dr Mzige) Bila shaka JF kuna wataalamu watatusaidia, kwani sote tungependa tuishi bila maradhi.
 
Je ni asilimia ngapi ya Watanzania wanakisukari?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…