Siku ya Kupinga Adhabu ya Kifo Duniani - LHRC Kuadhimisha na Jukwaa la Wahariri (TEF)

Siku ya Kupinga Adhabu ya Kifo Duniani - LHRC Kuadhimisha na Jukwaa la Wahariri (TEF)

Mwambie henga huku uraiani
Kuna watu wana vibali vya kuua

Ova
Wengine Wamejitungia sheria ya kuua na inafanyakazi yaani wanaruhusiwa kuua hata bila kujulikana na jamii, wanakuteka kwa kuwambia wanao shuhudia unatekwa wao ni akina nani kesho yake unatupwa kama mbwa, lakini ni binadamu aliyeumizwa vibaya na kumwagiwa tindikali, hapa nimekumbuka enzi zangu za somo la kemia kuhusu, hydrochloric acid

Kibaya zaidi hicho kifo hata tume ikiundwa inapata ugonjwa wa usingizi, (sleeping sickness), ambao hauna dawa
 
Swali fikirishi je mamlaka zinazo ruhusiwa kuua?
Hii ni ajabu Sana.
Kumetolewa ushuhuda hapa huyu dada mrembo alituhumiwa kuua na kuadhibiwa adhabu ya kifo kwa kunywongwa hadi kufa, huyo dada alikata rufaa, na akashinda na rufaa na kuachiwa huru, akikumbuka aliyokutana nayo, machozi yamemtoka.

P
Hivyo ni Visa vichache Sana, it is a rare cases.

Naendelea kusisitiza kwamba Kamwe siungi mkono kabisa kuondolewa kwa adhabu ya kifo hapa Tanzania na hata katika nchi zingine zote kabisa, hususani nchi za Afrika. Sikubaliani kabisa na Hoja hii ya kufuta adhabu ya kifo.
Wapo baadhi ya Wahalifu wanastahili kupewa adhabu ya kifo, na pia wanastahili kunyongwa hadi kufa.
Matahalani, kwa hapa Tanzania kuna Askari Polisi wengi Sana wamekuwa wakifanya vitendo vya uhalifu wa kupora Mali za raia na kisha raia hao wamekuwa wakiuawa makusudi ili kupoteza Ushahidi, watu wengi pia wamekuwa wakiuawa kwa makusudi wakiwa mikononi mwa Askari Polisi au wakiwa kwenye Vituo vya Polisi, na Wauaji wamekuwa hawachukuliwi hatua zozote zile Kali za kuwapa fundisho juu ya uhalifu wao huo. Askari Polisi wamekuwa wakihusika katika uhalifu kama huo kwa kuwa Wana uhakika kuwa na wao hawatauwa badala yake wanahamisika zaidi na zaidi kuendelea kuua watuhumiwa. Mimi binafsi naamini kwa dhati kabisa kwamba Endapo kama Rais wa nchi hii angesaini Hati ya Kifo dhidi ya OCD Christopher Bageni, yule Askari Polisi aliyewaua kikatili wale Wafflanyabiashara wa madini kutoka huko Mahenge Morogoro, Basi Polisi wangeogopa kufanya matukio mengine ya uporaji na mauaji dhidi ya Wananchi.

Aidha, Endapo kama OCD Christopher Bageni angenyongwa hadi kufa Basi lile tukio la mauaji la Bw. Hamza Mohamed pale Selander Bridge Dsm kamwe lisingeweza kutokea, na hata yule Mfanyabiashara kijana wa madini kule Mtwara pia asingeweza kuuawa na wale Askari Polisi walioongozwa na OC-CID Kalanje.

Mwisho:
Namshauri Rais SSH akubali kusaini Hati ya Kifo ili aliyekuwa OCD Christopher Bageni aweze kunyongwa hadi kufa, kwa sababu Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani tayari zimeshatoa idhini na baraka zote kabisa kwamba mtu huyo anastahili kunyongwa hadi kufa. Huku mitaani kuna chuki kubwa sana dhidi ya hao Watu.
Endapo kama Rais anaona labda pengine kutokana na Imani yake ya kidini hawezi kusaini Hati za Kifo ili Watu hao wanyongwe, Basi namshauri AKASIMISHE MADARAKA hayo kwa Watu wengine walio chini yake ili waweze kutekeleza jukumu hilo kwa niaba yake.

Inakera Sana kwa kweli kuendelea kuwaona Watu wauaji ambao waliua wenzao kwa makusudi Halafu wao bado wanaachwa waendelee kufaidi maisha, Kamwe jambo hili halikubaliki hata kidogo.
 
Kuna wengi wamehukumiwa kifo kwa kunyongwa mpaka kufa, lakini hawajakata rufaa kwasababu wala hawajui kuwa wana haki ya kukata rufaa. Hivyo wanasubiri tuu kutekelezwa kwa adhabu hiyo.
Wafungwa wa kunyongwa hawafanyi kazi yoyote, ni kula tuu na kulala, ila wanakuwa na mateso makubwa sana ya kisaikolojia.
P
Wanaishi bila matumaini ya kuishi lakini wanaishi
 
Saa hizi ni Saa 7 kamili mchana, event hii imemalizika rasmi,
Asanteni kwa kufuatilia.
Pasco
 
Wanabodi

Tarehe 10 ya October kila mwaka, ni siku ya Kimataifa ya Kupinga Adhabu ya Kifo Duniani.

Kwa Tanzania kwa mwaka huu, Kituo cha Sheria na Haki za Binaadamu Tanzania, LHRC kinazungumza na Wahariri wa Jukwaa la Wahariri Tanzania, TEF, katika ukumbi wa hoteli hii ya Holiday Inn ya hapa jijini Dar es Salaam.

Mimi mwana jf mwenzako ambaye ni mwandishi wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea, ambaye pia ni mtetezi mkubwa wa haki za binaadamu na haki ya kuishi, niko hapa ukumbini kukuletea kile kinachoendelea hapa.

Wakati ukisubiria hii shughuli hapa ianze, karibu nyuzi zangu hizi uanze refreshing
Hii event iko live kwenye
View: https://www.youtube.com/live/74qsu__92pM?si=_9Et_u9v2jIC2aN_

Na hapa
View: https://www.youtube.com/live/oJDwqRmsSPE?si=ueIE-gkjwkNpFwPb


Karibu

Paskali

Huu ni mpumbavu huu! Ukiua kwa upanga na wewe utauawa kwa upanga! Upumbavu huu kwa jina l hako haki ya binadamu
 
Wanabodi

Tarehe 10 ya October kila mwaka, ni siku ya Kimataifa ya Kupinga Adhabu ya Kifo Duniani.

Kwa Tanzania kwa mwaka huu, Kituo cha Sheria na Haki za Binaadamu Tanzania, LHRC kinazungumza na Wahariri wa Jukwaa la Wahariri Tanzania, TEF, katika ukumbi wa hoteli hii ya Holiday Inn ya hapa jijini Dar es Salaam.

Mimi mwana jf mwenzako ambaye ni mwandishi wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea, ambaye pia ni mtetezi mkubwa wa haki za binaadamu na haki ya kuishi, niko hapa ukumbini kukuletea kile kinachoendelea hapa.

Wakati ukisubiria hii shughuli hapa ianze, karibu nyuzi zangu hizi uanze refreshing
Hii event iko live kwenye
View: https://www.youtube.com/live/74qsu__92pM?si=_9Et_u9v2jIC2aN_

Na hapa
View: https://www.youtube.com/live/oJDwqRmsSPE?si=ueIE-gkjwkNpFwPb


Karibu

Paskali

Fulgence Masawe akimaliza mada, atueleze kwa nini kituo kimejaa wachaga na wapare tu.
 
Capital punishment iwepo for heinous crimes.
 
Fulgence Masawe akimaliza mada, atueleze kwa nini kituo kimejaa wachaga na wapare tu.
Hili mbona sio swali, kwani kwenye nafasi za kazi, kuna mahali popote pameandikwa utajaza kabila lako?, ikitokea walioomba ni wengi, na wenye sifa wote ni Wachagga, utashindwa kuwaajiri kwasababu ni Wachagga, hivyo lazima utafute kabila jingine hata kama hana sifa?.

Kuna makabila fulani ni wazuri maeneo fulani. Wachagga ni wazuri kwenye pesa, wamejaa TRA. Musoma wazuri jeshini, Tangu JWTZ imeanzishwa watu wa Kanda ya Ziwa ni wengi majeshini, tena wengi ni kabila fulani, mbona huulizi?.

Nenda majiji yote, ma shoe shiners ni kabila fulani, mbona huulizi?
Wapima nyama na waajiriwa mabuchani kote ni kabila fulani mbona huulizi?.
Wachonga vinyago ni kabila fulani!,
Hata wafanya biashara ile the oldest profession wengi walikuwa kabila fulani!.
Waacheni shemeji zangu!.
Hata yule Blaza wangu, aliwahi kunyooshewa kidole cha ukabila!, tukamtetea humu Tuhuma za Ukabila: Wasukuma si Miongoni mwa Makabila yenye Ukabila, tatizo ndio walio wengi!
P
 
Kaka Paskali mimi sijui mambo mengi ya kisheria. Kifupi mimi ni maamuma kwenye Sheria. Lakini nina uwezo wa kufikiri. Logic ya haki ya mtu kuishi ni ipi?

Mfano, kwenye makongamano yenu, kuna mtu ameishawahi kutoa mada akisema ya kwamba kuna mtu aliwaua wanae watatu (mfano), mkewe (mfano) na msaidizo wake wa kazi (mfano), lakini yeye anaamini mtu huyo anastahili kuishi licha ya mauaji aliyofanya dhidi yake na yupo tayari kumtetea Mahakamani asipate Hukumu ya Kifo?
Nakuhakikishia siku akitokea mtu huyo, nami nitaunga mkono kuondolewa kwa adhabu ya Kifo!

Natanguliza shukrani!🙏🙏🙏🙏
 
Back
Top Bottom