Siku ya kwanza kuona Maiti

rikiboy

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2017
Posts
21,952
Reaction score
43,265
Hakika kila nafsi itaonja mauti japo kifo hakizoeleki kabisa ndo maana huwa tunaumia sana tukifiwa.

Kuna siku niliona maiti ya mmama aliegongwa na gari nikiwa la saba aisee ile picha haijawahi potea kichwani mwangu ubaya alikuwa bado amefungua macho[emoji24][emoji24][emoji24] Baada ya lile tukio alifariki rafiki yangu hakika sikuweza kwenda kuaga nilishindwa kabisa! Mungu awalaze mahali pema peponi.

Je siku ya kwanza kuona maiti ilikuwaje?? Hii memory ni mimi tu nashindwa kuifuta au?
 
Ilikuwa ni ajali ya gari mlima meta, nilikuwa darasa la 6. Nikajiapiza sitarudia tena kushuhudia ajali.
 
Ilikuwa ni ajali ya gari mlima meta, nilikuwa darasa la 6. Nikajiapiza sitarudia tena kushuhudia ajali.
Yani yataka roho ngumu sana tena wa ajali aisee[emoji24][emoji24]
 
Je, uliisikia ile ya Musoma? Boti ilipinduka watu wakazama, wakaokotwa wachache tu. Siku ya siku mvuvi si akavua Sato mkubwa? Alipomchinja akakuta mkono wenye saa tumboni. Hii ilivuma sana tu
Duuh hii hapana sijaisikia mkuu aise
 
Pole sana mkuu, upande wangu ni tofauti sana nimeona maiti mara ya kwanza kwenye ajali ya gari nikiwa darasa la tano na nyingine kuna jamaa aliuwawa na tembo lakini niliona easy tu kwa kweli mpaka leo hata ikitokea msiba wananiambia nikakague maiti.
 
Pole sana mkuu, upande wangu ni tofauti sana nimeona maiti mara ya kwanza kwenye ajali ya gari nikiwa darasa la tano na nyingine kuna jamaa aliuwawa na tembo lakini niliona easy tu kwa kweli mpaka leo hata ikitokea msiba wananiambia nikakague maiti.
Duuh una moyo mkuu...Tembo ana hatari aisee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…