Siku ya Wanawake Duniani: Itafutwe namna ya kuonyesha jitihada za wanaume kifamilia na kijamii

Siku ya Wanawake Duniani: Itafutwe namna ya kuonyesha jitihada za wanaume kifamilia na kijamii

CHOTABUSARA

Member
Joined
Feb 6, 2012
Posts
47
Reaction score
48
Ni vyema kuwashukuru na kuwapongeza mama zetu kwa kutulea toka tumboni mpaka leo. Watu husema wababa wengi hufa mapema kuliko wamama kutokana na kutokuongea na hivyo kupata magonjwa yatokanayo na misongo ya mawazo.

Jana ilikua siku ya wanawake duniani, wanawake wengi waliongelea ubora wao na jitihada katika kazi, wamesifiwa na watoto wao wa kiume na wa kike, utasikia huyu anasema mama aliuza maandazi ili kunisomesha mpaka nikamaliza, huyu anasema mama aliuza pombe za kienyeji ili nisome nk.

Kwa sababu hii ya wanawake kubarikiwa kuongea na kutokana na hali halisi na maumbile mama huwa karibu zaidi na watoto, ni kama ambavyo jogoo hatembei na vifaranga, watoto hawa hushawishiwa kuwa mama yao amehangaika sana kuwalea kuliko baba yao na hii huwafanya watoto hawa wanapokua watu wazima kuelekeza mapenzi mengi zaidi kwa mama kuliko kwa baba.

Lakini nani atawasemea wababa wale wanaolala baharini na maziwani ili kuvua na kupata kipato kwa ajili ya familia zao, nani atawasemea wababa wale walio chini ya migodi na wakati mwingine kufia huko wakitafuta kwa ajili ya familia zao, na bahati nzuri baba akipata furaha inaongezeka katika familia, yaani baba atalea mama na watoto,

Tatizo kubwa huwa kipato kikizidi baba ataongeza mpenzi wa pembeni lakini bado nia ni kusambaza furaha, wamama wengi wakipata kipato kikubwa ndio chanzo wa kuvunjika kwa ndoa, huwa wanasema ndoa ya nini naweza kulea watoto wangu, mwanaume wa nini kama ninamudu maisha yangu, ni ngumu sana ndoa kuendelea kama mama ana kipato zaidi ya baba labda baba awe tayari kwa fedhea zote.

Wanaume inabidi kutafuta jinsi ya kuonyesha jitihada na umuhimu wetu kwenye jamii, na hii tabia iliozuka ya mwanamke kusifiwa sababu tu kapata nafasi fulani hata kabla hajafanya lolote haiwajengi bali inawafanya watukuze zaidi uwanamke wao, ili tutaliongea siku nyingine.

Nani atawasemea wababa wanaopandisha zege gorofa ya kumi kwa ajili ya familia zao, wale waliolala chini ya magari na mitambo mikubwa (mafundi) kwa ajili ya familia zao, wanaokesha wakiendesha ndege, meli, magari moshi, mabasi, taxi, dala dala nk. kwa ajili ya familia zao, wapiga Debe, madalali, waliopo maofisini na viwandani kwa ajili ya familia zao nani atawasemea.

Leo hii Ukraine wababa wameambiwa wabaki kupigania nchi yao, watoto wako na mama zao wanakimbia nchi, watoto wale wataambiwa na mama zao nakupenda mwanangu tutakufa wote, Nani atawasemea waliobaki wanapishana na mabomu na wengi watakufa

Kama wanaume hatukubarikiwa kuongea itafutwe jinsi ya kuonyesha jitihada zetu pia katika familia na jamii.

MWANAUME
 
ili la wanaume kutoongea upuuzi wa mama zetu nimeliona sana, mama yangu mzazi ni sana kunipa background ya father akiwa ameboreka, atanieleza ad maisha yake ya ulevi na michepuko yake ya ujanani, lakin baba yangu hakuwai kunipa background mbaya ya mamaangu adi ivi leo. adi najiuliza ivi inamaana mama yangu alikuwa mwema sana enz za ujana wao ata ndondo kuliwa na waume za watu, kufumaniwa maeneo, yaan alikuwa malaika au baba kaamua kukaa kimya.

mama yangu ndio tabia yake kunilisha chuki za baba anahis ataniBrain wash hajui kuwa namim pia ni baba na use*nge wa wanawake nauona kwa macho na akili zangu.
 
ili la wanaume kutoongea upuuzi wa mama zetu nimeliona sana, mama yangu mzazi ni sana kunipa background ya father akiwa ameboreka, atanieleza ad maisha yake ya ulevi na michepuko yake ya ujanani, lakin baba yangu hakuwai kunipa background mbaya ya mamaangu adi ivi leo. adi najiuliza ivi inamaana mama yangu alikuwa mwema sana enz za ujana wao ata ndondo kuliwa na waume za watu, kufumaniwa maeneo, yaan alikuwa malaika au baba kaamua kukaa kimya.

mama yangu ndio tabia yake kunilisha chuki za baba anahis ataniBrain wash hajui kuwa namim pia ni baba na use*nge wa wanawake nauona kwa macho na akili zangu.
Bora wewe mwenye akili mkuu
 
Ndio maana tunaitwa wanaume.
Hii ndio maana halisi.
Sisi ni makatapila, baada ya kutengeneza njia vizuri, tunakuja kuondolewa huku tukiambiwa tutaharibu barabara tuliyoitengeneza wenyewe.
Hivo usilalamike, maana ndio hali halisi ya uanaume aka Ubaba.
Cha muhimu tafuta sana mkwanja
 
Ni vyema kuwashukuru na kuwapongeza mama zetu kwa kutulea toka tumboni mpaka leo. Watu husema wababa wengi hufa mapema kuliko wamama kutokana na kutokuongea na hivyo kupata magonjwa yatokanayo na misongo ya mawazo.

Jana ilikua siku ya wanawake duniani, wanawake wengi waliongelea ubora wao na jitihada katika kazi, wamesifiwa na watoto wao wa kiume na wa kike, utasikia huyu anasema mama aliuza maandazi ili kunisomesha mpaka nikamaliza, huyu anasema mama aliuza pombe za kienyeji ili nisome nk.

Kwa sababu hii ya wanawake kubarikiwa kuongea na kutokana na hali halisi na maumbile mama huwa karibu zaidi na watoto, ni kama ambavyo jogoo hatembei na vifaranga, watoto hawa hushawishiwa kuwa mama yao amehangaika sana kuwalea kuliko baba yao na hii huwafanya watoto hawa wanapokua watu wazima kuelekeza mapenzi mengi zaidi kwa mama kuliko kwa baba.

Lakini nani atawasemea wababa wale wanaolala baharini na maziwani ili kuvua na kupata kipato kwa ajili ya familia zao, nani atawasemea wababa wale walio chini ya migodi na wakati mwingine kufia huko wakitafuta kwa ajili ya familia zao, na bahati nzuri baba akipata furaha inaongezeka katika familia, yaani baba atalea mama na watoto,

Tatizo kubwa huwa kipato kikizidi baba ataongeza mpenzi wa pembeni lakini bado nia ni kusambaza furaha, wamama wengi wakipata kipato kikubwa ndio chanzo wa kuvunjika kwa ndoa, huwa wanasema ndoa ya nini naweza kulea watoto wangu, mwanaume wa nini kama ninamudu maisha yangu, ni ngumu sana ndoa kuendelea kama mama ana kipato zaidi ya baba labda baba awe tayari kwa fedhea zote.

Wanaume inabidi kutafuta jinsi ya kuonyesha jitihada na umuhimu wetu kwenye jamii, na hii tabia iliozuka ya mwanamke kusifiwa sababu tu kapata nafasi fulani hata kabla hajafanya lolote haiwajengi bali inawafanya watukuze zaidi uwanamke wao, ili tutaliongea siku nyingine.

Nani atawasemea wababa wanaopandisha zege gorofa ya kumi kwa ajili ya familia zao, wale waliolala chini ya magari na mitambo mikubwa (mafundi) kwa ajili ya familia zao, wanaokesha wakiendesha ndege, meli, magari moshi, mabasi, taxi, dala dala nk. kwa ajili ya familia zao, wapiga Debe, madalali, waliopo maofisini na viwandani kwa ajili ya familia zao nani atawasemea.

Leo hii Ukraine wababa wameambiwa wabaki kupigania nchi yao, watoto wako na mama zao wanakimbia nchi, watoto wale wataambiwa na mama zao nakupenda mwanangu tutakufa wote, Nani atawasemea waliobaki wanapishana na mabomu na wengi watakufa

Kama wanaume hatukubarikiwa kuongea itafutwe jinsi ya kuonyesha jitihada zetu pia katika familia na jamii.

MWANAUME

Haina hata haja yakusema mkuu!!! Na iyo ndo sifa ya baba kwenye Jamii yoyote ile...... sisi tunatimiza wajibu wetu kwa hawa wanawake zetu!!! Biblia ilishasema tuishi nao kwa akili, wanawake ni watu ambao wanahitaji zaidi kubembelezwa na kupewa raha.....!!!!
Sasa hii siku ya wanawake huwa ni ya kwao wao wanafarijiana Na sisi kuwafariji kwakutambua umuhimu wao kwenye jamii.... sisi tayari tumepewa nafasi kubwa sana kwenye jamii mkuu kuitwa baba tayari kwetu ni heshima tosha,

Lakini pia ipo siku ya kina baba duniani hii ni kwa wababa tu na sio vijana..... kwaiyo kila mtu anapata anachostahili, hawa wanawake tuwe nao karibu na kuishi kwa akili zaidi,

Umegusia swala la mama na mtoto, jipe muda wakuwa karibu na watoto, kuwaelekeza, kujua wanachanga moto gani, nakuwashauri, sisi kuhudumia familia bado haitoshi kutufanya tuwe mbali na wapendwa wetu (wanetu) so ili mtoto asiambiwe na mama jiweke karibu na mtoto ndo akili tulizoambiwa izo. Uko ndo kuishi kwa akili na mwanamke sio kutaka mashindano mkuu.......!!!!!!
 
hata mungu akuweka siku ya wanawake duniani na yeye ndie muumba. hakumchagua mwanamke yoyote kuwa nabii au mtume yeye ndie anaewajua. tanzania imezidi sana kuwa weka mbele mbele wakina mama wakidhani ndio viongozi bora na kumbe sio waangalie vitabu vya mungu vinasema nini
 
Mwanaume halalamiki.

Hata wakiwa na siku 100 ndani ya mwaka.

Haibadilishi uanaume wako.
 
Mimi mpaka pale ambapo wanawake wa Ukraine watakataa ruhusa waliyopewa ya kukimbia vita ili wabaki wapigane, na wanaume waruhusiwe kuondoka ndipo usawa wa kijinsia nitaona unawezekana. Na ndo nitawaelewa wazungu mnaojitapa nao kuwa wana usawa wa kijinisia. Tofauti na hapo wanawake muache kudanganywa.
 
Chotabusara, hoja yako ni ya msingi sana. Naelewa sio wengi wanaweza kuelewa kwa uzito unaostahili madhara yanayotokea kwetu Wanaume kutokana na wawama kupandikiza chuki kwa watoto na kupelekea kuleta msongo wa mawazo na madhara yanayotokea kwa wababa. Wababa wengine wamepata madhara makubwa na hata kupoteza maisha kwasababu hii. Kama Wanaume pamoja na kumtanguliza Mungu katika maisha haya, kuna haja ya kuwa na rafiki au ndugu wa karibu wa kushare na kushauriana ili kupunguza msongo wa mawazo
 
Back
Top Bottom