Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
SIKU YA WANAWAKE DUNIANI/SIKU YA WANAWAKE TANZANIA
NYANGE BINT CHANDE MWANAMAMA ALIYEJITOLEA NYUMBA YAKE KUWA OFISI YA TANU KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA
Kuna mtu alipata kusema kuwa utafika wakati watoto na wajukuu wa wapigania uhuru wataingia katika makabati na masanduku ya wazee wao kutaka kuimarisha historia za wazee wao waliopigania uhuru wa Tanganyika.
Leo nimepokea picha ya Bi. Nyange bint Chande mmoja wa akina mama waliokuwa mstari wa mbele katika TANU Tabora.
Bi. Nyange alijitolea nyumba yake kuwa ofisi ya TANU.
Vyama vya akinamama - Nujum ul Azhar, Waridatil Hubb na Egyptian Club vilivyokuwapo mjini Tabora chini ya Bi. Nyange binti Chande na Zarula binti Abdulrahman vilisaidia sana kuipa TANU nguvu katika Jimbo la Magharibi.
Tanzania ina deni kubwa sana kwa hawa wazalendo.
Nyange bint Chande
NYANGE BINT CHANDE MWANAMAMA ALIYEJITOLEA NYUMBA YAKE KUWA OFISI YA TANU KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA
Kuna mtu alipata kusema kuwa utafika wakati watoto na wajukuu wa wapigania uhuru wataingia katika makabati na masanduku ya wazee wao kutaka kuimarisha historia za wazee wao waliopigania uhuru wa Tanganyika.
Leo nimepokea picha ya Bi. Nyange bint Chande mmoja wa akina mama waliokuwa mstari wa mbele katika TANU Tabora.
Bi. Nyange alijitolea nyumba yake kuwa ofisi ya TANU.
Vyama vya akinamama - Nujum ul Azhar, Waridatil Hubb na Egyptian Club vilivyokuwapo mjini Tabora chini ya Bi. Nyange binti Chande na Zarula binti Abdulrahman vilisaidia sana kuipa TANU nguvu katika Jimbo la Magharibi.
Tanzania ina deni kubwa sana kwa hawa wazalendo.
Nyange bint Chande