Sikutegemea kama Kariakoo kuna fremu za milioni 12

Sikutegemea kama Kariakoo kuna fremu za milioni 12

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
11,793
Reaction score
22,552
Kama na wewe ulikuwa hujui, ngoja nikujuze!

Katika kumsindikiza rafiki yangu mgeni; mfanya biashara toka Dubai, Ambaye anataka kuweka duka moja la vifaa na simu kariakoo; Tulibahatika kupita sehemu kadhaa tukitafta fremu kupitia kwa madalali, Fremu za biashara ziko juu sana hadi ($3000-$6000) kwa mwezi na lazima malipo huwa ni kwa mwaka au miezi sita, na wenye nyumba/majengo wanapangisha kwa kuringa vibaya!

Na kuna baadhi ya mmiliki mmoja jirani ambaye tayari yeye anabiashara pale alisema hizo bei huwa zinapanda kila mara na pengine watu wengine hufanya fitina kwa wenzao ili wafukuzwe; Cha ajabu baadhi ya wamiliki hata kama hakudai ikitokea katikati akiomba umkopeshe pesa ni sharti umpatie vinginevyo utakuwa hatarini kutokupangishwa tena mkataba wako unapoisha.

Kusema ukweli hatukufanikiwa ikabidi tughairi tukatafte sehemu nyingine mbali na kariakoo, maana gharama ni kubwa sana halafu isitoshe Biashara ya simu ni ngumu sana kariakoo kwa mujibu wa maelezo ya wenyeji kwa kuwa fremu nyingi sasa wengi zinawashinda wanazirudisha.

Kwa akili yangu mwenzenu mwanzo nilijuwa labda ni Tsh milion moja na nusu kwa mwezi, au milion ama laki nane kwa mwezi, kumbe hizo ni bei za mwezi mmoja tu ndani ya fremu husika.
 
kama na wewe ulikuwa hujui, ngoja nikujuze!
katika kumsindikiza rafiki yangu mgeni; mfanya biashara toka Dubai, Ambaye anataka kuweka duka moja la vifaa na simu kariakoo; Tulibahatika kupita sehemu kadhaa tukitafta fremu kupitia kwa madalali, Fremu za biashara ziko juu sana hadi ($3000-$6000) kwa mwezi na lazima malipo huwa ni kwa mwaka au miezi sita, na wenye nyumba/majengo wanapangisha kwa kuringa vibaya! Na kuna baadhi ya mmiriki mmoja jirani ambaye tayali yeye anabiashara pale alisema hizo bei huwa zinapanda kila mara na pengine watu wengine hufanya fitina kwa wenzao ili wafukuzwe; Cha ajabu baadhi ya wamiriki hata kama hakudai ikitokea katikati akiomba umkopeshe pesa ni sharti umpatie vinginevyo utakuwa hatarini kutokupangishwa tena mkataba wako unapoisha.
Kusema ukweli hatukufanikiwa ikabidi tughairi tukatafte sehemu nyingine mbali na kariakoo,maana gharama ni kubwa sana halafu isitoshe Biashara ya simu ni ngumu sana kariakoo kwa mujibu wa maelezo ya wenyeji kwakuwa fremu nyingi sasa wengi zinawashinda wanazirudisha.
Eheeeee
 
mkuu fremu kwa sasa majengo yamekua mengi biashara imepungua kwa miaka kadhaa ni machache sana yatakua bei ghari...
 
kwa hichi kipindi cha magufuri biashara zimekua ngumu fremu zipo nyingi sana njoo sinza/mwananyamala/mwenge/kijitonyama.
Huko bei gan? Speed ya biashara ikoje
 
frem zipo hapo kwa Sauli wanaita saba saba laki sita tuu...mtaa wa nywere na vipodozi na hilo jengo linatizamana na bigbon laki saba mbele hapo...
 
Kuna anguko kubwa sana la biashara K,koo toka December mpakas sasa,tegemea biashara nyingi sana kufungwa na tegemea biashara nyingi mpya kufunguliwa,kwa sasa biashara K,koo imesimama sana na soon bei ya fremu itapungua mno ,nadhani tunao fanya biashara K.koo tunalijua vizuri jambo hili,
 
Njoo sahv magu kawaumuza vibaya nendeni sahv mtagombaniwa kupanga
 
Huko bei gan? Speed ya biashara ikoje
zipo hadi za laki 6 ila speed ipo low sana/chini coz watu wanalalamika hali ngumu ya maisha hivyo "purchading power deteriorated".
 
Kama center ya Biashara Kariakoo imeanguka sasa hawa TRA ukusanyaji wa kodi si unakuwa changamoto sana.
 
Biashara ngumu sana kwa sasa watu wengi wanatoka kuwafuata watu huko huko mf mwenge, tandika, Mbagala r3 nk nk
 
In fact biashara kwa sasa ni ngumu mzunguko wa pesa ni mdogo sana,mfano wafanyabiashara wa jumla wa manzese wameanzisha utaratibu wa kuwafuata retailers hukohuko mashinani na canter zao,awali walizoea kufutwa pale manzese kama wafalme
 
In fact biashara kwa sasa ni ngumu mzunguko wa pesa ni mdogo sana,mfano wafanyabiashara wa jumla wa manzese wameanzisha utaratibu wa kuwafuata retailers hukohuko mashinani na canter zao,awali walizoea kufutwa pale manzese kama wafalme
Wajifunze kutokubweteka pale demand inapokuwa juu
 
Mkuu njoo nikuuzie ya kwangu hipo mchikichi/ manyema karibu na jingo la simba
 
Back
Top Bottom