Sikutegemea nilichokikuta ukweni

K
Khaaa aisee
 
Kwanza unataka kuoa ili iweje?
Tuanzie hapo kwanza!
 
Sasa wewe ujiingize kuoa Msukuma halafu ulete mahari 1m? Utatimuliwa asubuhi na mapema! Kila mwanaume akaoe kwao, wenye tamaduni zao waachieni!
Mimi nlienda kulipa mahari huko maswa mtoto wa dada alikua kamchumbia mahari walitaka 6m na kijana ni mtumishi wa halmashauri akaniomba anko tuwalioe tu hiyo ...nkamwambia top 2m hatununui shamba.tulivyorudi ndani nkawaambia 2m kma haiwezekani tuondoke kijana atapata mwingine...waliongea kilugha karibia saa nzima wanaitana nje mwisho wa cku wakapokea pesa
 
Ulijitoa ukweni, wewe n mjinga. Kwa ndezi kama wewe kukomolewa ukweni ni kawaida.
 
Wanataka wakugeuze chuma ulete, shtuka mwanangu huo ni mtego
 
Msingeaga mngeondoka tu
 
Usishangae kukuta mko wawili watatu mnaojikamua kuwaridhisha wakwe. Kila mmoja anapangiwa dau lake. Familia nyingi wanamuona mtoto wa kike kam kitega uchumi. Kukata kwako tamaa ndio kuingizwa mkenge kwa mwingine
 
Hio laki4 uliemtolea alikua ni bikra au ndio haohao panya road
 
Ok
 

Siku zote tulikuwa tunakwambia ufanye kazi kwa bidii ili upate pesa siku ukija kutajiwa mahari usije kuona unaonewa, ukaona kama na tulikuwa tunakupigia makelele😂
 
Hio mahar ni zawad ya nini rafiki
 
Wala sio shida, mnashindwa kujua mila za kibantu nyie, wakikomaa wakubalieni wala sio shida ila zinatangulia laki 7.5 zingine huwa ni kudaiana hadi mnakufa. Hizo ni mila tu msibishane sana
 
Huyo ndugu anayekushauri uendelee kulipa ama anashirikiana na wakwe zako kaweka Cha juu au ni bumunda!

KIUFUPI VUNJA HIYO NDOA TARAJIWA.

HATA HIYO MILIONI MOJA NI NYINGI SANA.

MAHALI ISIZIDI LAKI SABA .
 
Kuna hii LIVE imefanyika Kiambuu, Kenya. Wiki hii. Msichana kapata mchumba wa kizungu. Mchumba kaambiwa twende home kwa WAZAZI. Walipofika WAZAZI wakasema kijana unatakiwa ulipe mahari milioni sita ya Kenya. Mzungu kasema no problem, nipeni account nihamishe pesa now now. Hapo ndio Mambo yalipoharibika. Mzee kasema hamishia kwangu, mama akasema, haiwezekani, kwako tatu, kwangu tatu, mzee kasema usinitanie, msichana kasema Basi ihamishiwe kwangu nitakuja kueagawia. Mzee kasema hamniambii kitu,pesa yote kwa account yangu. Mzungu kamwambia mchumba, hebu tuwape nafasi wakufikia muafaka watatuambia. Mzungu kwenye gari na mchumba fyuu wakarudi zao town.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…