Mtasema yote Simba ni Wababe wa kimataifa kwa Tanzaniawatanzania ni wagumu sana kuambiwa wakaelewa ndioc maana tunafail sana maeneo mengi..
Simba wamecheza mechi 4 ugenini ukiacha mechi ya nkana wameruhusu mabao 17 na kufunga goli 1 pia wamecheza michezo 4 nyumbani wamefunga magoli 6 na kuruhusu 1. Huwezi ukasema una timu nzuri kwa hesabu hizi..
Pia tukumbuke wote waliocheza Dar es salaam wamelalamikia hujuma mpaka pale Mazembe walipokuja na kuitahadharisha CAF juu ya hayo malalamiko na kila mtu Simba alivyoshindwa kumfunga Mazembe Nyumbani..
Ulikuwa ulevi wa sifa. Eti hata aje Barcelona anapigwa. Kabla ya Barca, wangeanza na TP Mazembe kwanza.Kufa ni kufa tu nyingine ni mbwembwe!!! Kikubwa kujipanga upya msimu ujao!!! Poleni wafiwa!! Ila marehemu alikuwa na majigambo sana na mdomo usiokuwa na staha akidiriki kusema hata waje barcelona.. Ama kweli dunia hadaa ulimwengu shujaa
Nyie wajuaji miaka 3 mfululizo mlifika wapi?Mpira wa jana ndio nimetanabahisha kinagaubaga kwamba Simba hawajui soka asilan!
Uko sahihi! Hao Esperance na Wydad hatari mno hata wakiwa ugenini.Simba wamejitahidi sana makosa waliyonayo Timu nyingi wanayo inatakiwa wajitathmini katika hilo kutofungwa idadi kubwa ya magoli ugenini...Al Ahly ni wa kawaida sana sio wa kutolewa mfano kwa sasa hivi kwa Timu zenye viwango bora kabisa ni Esperance, Wydady na Sundown hao Mazembe nao sio hatari sana kama hao wajuba watatu juu...
Uko sahihi mkuu! Defense ya Simba sio imara kuhimili mashambulizi hasa mechi za ugenini.Nadhani faraja zisizo na tija hazijengi.Kuna jambo ambalo watu hawasemi ukweli , Simba imefungwa magoli rahisi kuliko timu nyingi. Ndiyo, Simba imefika robo fainali LAKINI katika match dhidi ya Mazembe iwapo Simba ingekuwa na kocha kama yule wa Sundon au yule mfaransa aliyeondoka mwaka jana Simba ingeweza shinda match au kufungwa kwa Small margin.Kocha ameshindwa kutengeneza water tight defence hebu angalia Simba away record kuanzia group stage ya kufungwa 16 : 1, hiyo sio sawa.Siandiki kama mnazi wa Yanga au Simba lakini kama mtanzania anayeipenda nchi yake.Najaribu kuota match Simba vs Al Masiri kule Misiri (Last year) ambapo matokeo yalikuwa 0:0 pia .najaribu kuota match ya Yanga Vs Timu ya Zimbabwe sometime back iliyochezwa Harare matokeo : 2 for Yanga na mwisho Match Uganda crane Vs Taifa star kule Uganda matokeo 0 :0. Hizi match tatu hapo juu zinaonyesha pakiwapo na mipango Timu za Tanzania zinaweza kushinda away au kushindwa kwa magoli machache.Samahani kwa kuandika Gazeti LAKINI naomba MO alisome.Kabla ya ku comment maoni yangu soma kila neno kwa makini.Ahsante