Shark
JF-Expert Member
- Jan 25, 2010
- 29,775
- 29,746
Wakuu Kwema?
Hapo Kabla kwa mara ya kwanza, timu ya Yanga ilifanya tamasha lake la kutambulisha wachezaji wake wapya iliyowasajili msimu huu, pamoja na wanaoendelea. Tamasha hili lilikwenda kwa jina la Wananchi Day.
Kwa upande wa watani wao wa jadi, Wekundu wa Msimbazi, Simba S. C nao walifanya tamasha lao kama kawaida yao hapo jana ili kutambulisha kikosi chao nao, wapya na wanaoendelea.
Sasa basi ningependa tujadili juu ya matamasha haya mawili, utani wa jadi hauko kwenye pitch tu, hata matukio kama haya tunashindana pia kujua nani kafanikiwa zaidi ya mwengine. Nitaanza kulinganisha kama ifuatavyo,
KUJAZA UWANJA
Ni Wazi kwa matamasha yote mawili uwanja ulijaa. So kila timu imefanikiwa kwa hilo. Ila Simba inafanikiwa zaidi sababu imeweza kujaza Uwanja siku Kazi (Jumanne) wakati Yanga ilijaza Uwanja siku ya Mapumziko.
Inawezekana kabisa Simba wangefanya tamasha lao siku ya Mapumziko basi Uwanja "Ungetapika" zaidi ya Jana. Au Yanga wakafanya tamasha lao siku ya kazi basi wangeshuhudiwa na Mashabiki Wachache + Viti Vitupu!!
VIKOSI
Simba inaonekana kua na kikosi bora kuliko Yanga, sababu kwa hesabu za kawaida tu Simba imeshinda kwa tofauti ya Magoli mawili wakati Yanga imesuluhu.
Pia ikumbukwe kua Zambia wako juu kisoka kuliko Kenya, hivyo inawezekana kabisa Simba imecheza na timu bora zaidi kuliko Yanga.
Kwa muono wangu huu, juu ya haya machache basi Simba imefanikiwa zaidi kuliko Yanga. Karibuni kwenye mjadala...!!!
Hapo Kabla kwa mara ya kwanza, timu ya Yanga ilifanya tamasha lake la kutambulisha wachezaji wake wapya iliyowasajili msimu huu, pamoja na wanaoendelea. Tamasha hili lilikwenda kwa jina la Wananchi Day.
Kwa upande wa watani wao wa jadi, Wekundu wa Msimbazi, Simba S. C nao walifanya tamasha lao kama kawaida yao hapo jana ili kutambulisha kikosi chao nao, wapya na wanaoendelea.
Sasa basi ningependa tujadili juu ya matamasha haya mawili, utani wa jadi hauko kwenye pitch tu, hata matukio kama haya tunashindana pia kujua nani kafanikiwa zaidi ya mwengine. Nitaanza kulinganisha kama ifuatavyo,
KUJAZA UWANJA
Ni Wazi kwa matamasha yote mawili uwanja ulijaa. So kila timu imefanikiwa kwa hilo. Ila Simba inafanikiwa zaidi sababu imeweza kujaza Uwanja siku Kazi (Jumanne) wakati Yanga ilijaza Uwanja siku ya Mapumziko.
Inawezekana kabisa Simba wangefanya tamasha lao siku ya Mapumziko basi Uwanja "Ungetapika" zaidi ya Jana. Au Yanga wakafanya tamasha lao siku ya kazi basi wangeshuhudiwa na Mashabiki Wachache + Viti Vitupu!!
VIKOSI
Simba inaonekana kua na kikosi bora kuliko Yanga, sababu kwa hesabu za kawaida tu Simba imeshinda kwa tofauti ya Magoli mawili wakati Yanga imesuluhu.
Pia ikumbukwe kua Zambia wako juu kisoka kuliko Kenya, hivyo inawezekana kabisa Simba imecheza na timu bora zaidi kuliko Yanga.
Kwa muono wangu huu, juu ya haya machache basi Simba imefanikiwa zaidi kuliko Yanga. Karibuni kwenye mjadala...!!!