Prince Kunta
JF-Expert Member
- Mar 27, 2014
- 22,797
- 28,904
Wewe jamaa sidhani kama unao ubongoTangu jana baada ya kuwekwa picha kwenye akaunti rasmi za klabu ya Simba zikionesha picha ya Mchezaji Benard Morrison akiwa amevaa jezi zinazovaliwa na Timu hiyo, kumezuka Sintofahamu kwa wapenzi wa Mpira Tanzania.
Picha moja inaonesha kama anaandika (saini?) Na nyingine kama mtu anayeweka dole Gumba kwenye karatasi ambazo zinakisiwa kama mkataba.
Kwenye Caption yamewekwa maneno yanayosomeka MORISSON IS RED.
Baada ya bandiko hilo kumezuka taharuki kwa washabiki wa Yanga na Simba kwa upande mwingine.
Vyombo vya habari navyo havipo nyuma. Vikishadadia kwamba Morrison amesajiliwa Simba.
Kuna mambo ya kujiuliza kuhusu sakata hilo.
1. Je kumuonesha Mchezaji kwenye kurasa rasmi za Klabu ndio uhalali wa kwamba amesajiliwa?
2. Je kuna kiongozi yeyote Simba aliyejitokeza kudai ni kweli imemsajili morrison?
3. Mbona hata picha iliyotolewa hakuna yeyote kati ya Viongozi ambao hupenda kupiga picha na wachezaji wanaowasajili.
4. Hivi usajili mkubwa wa Mchezaji kama Morrison kiongozi asingependa kiki kuonekana?
5. Mbona wandishi tangu jana hawaendi kuwahoji Viongozi wa Simba ambao ndio waliotoa hiyo picha?
6. Chunguza mbona Msemaji wa Simba nae haweki wazi kama kweli Simba imemsajili Morrison? Huyu ndio mpenda kiki namba moja
Kinachooneka ni aina ya maneno ambayo kisheria huwezi kumuhukumu mtu.
Kisheria Simba haiwezi kuhukumiwa kwamba imemsajili Morrison. Inaweza kusema ni utani wa Jadi wa timu hizo mbili.
Kuna kipindi Makamu Mwenyekiti wa Yanga alizungumza kuhusu kumsajili Chama lakini baada ya kuminywa akawataka radhi Simba na kudai ulikuwa utani wa Jadi.
Pia angalia Taarifa ya Uongozi wa Yanga kuhusu sakata hilo la Morrison. Imeandikwa kwa tahadhali na umakini mno bila ya kuishutumu Simba, Morisson wala TFF.
Walichosema kwamba wana mkataba na Mchezaji huyo mpaka mwaka 2022.
Kwenye taarifa hiyo Yanga wamekwepa kuishutumu Simba kwa kujua kilichoonekana kwenye mitandao sio ushahidi sahihi wa kisheria hivyo kujiingiza kwenye matatizo.
Kama picha ni ushahidi tosha, hata Yanga walitoa picha tangu mwezi wa tatu zikionesha Morrison kasaini tena.
Kinachoonekana sakata hili ni nani atakaye mfunga kengele Paka.
Ni mtego kwa kila upande.
Ima umnase Yanga, Simba au TFF. Hili ndio Soka la Bongo vituko haviishi.
Tusubiri Muda utatoa majibu.
Yaani umbumbumbu hautokuisha kamwe