Simba haikufanya mazoezi uwanja wa Jamhuri Morogoro ikapoteza mechi muhimu

Simba haikufanya mazoezi uwanja wa Jamhuri Morogoro ikapoteza mechi muhimu

Kuna watu wanachukulia poa utaratibu na haki iliyopewa timu ngeni kufanya mazoezi katika uwanja utakaochezewa mechi siku moja kabla ya mechi.

Wachezaji wanapokuwa wamefanya mazoezi katika uwanja wa vita watakaoenda kuutumia, hili ni suala la kiufundi na linasaidia kuandaa wachezaji kimwili na kisaikolojia. Lengo kuu ni kuweka mizania sawa kati ya timu zote mbili kuelekea mchezo husika. Kumbuka football inaendeshwa na dhana nzima ya "fair play" na kanuni nyingi zimetengenezwa kulinda dhana hii.

Nakumbuka misimu miwili iliyopita Simba ilifanya kosa moja kubwa sana lililoigharimu timu na kufifisha harakati zake za ubingwa.

Simba ilihamishia mechi yake dhidi ya Prisons katika uwanja wa Jamhuri, Morogoro na kupoteza mchezo ule kwa goli 1-2. Sikumbuki sababu hasa ilikuwa nini ila pamoja na kwamba ilikuwa ndiyo mwenyeji wa mchezo, Simba haikufanya mazoezi katika uwanja ule wa Jamhuri kabla ya mchezo husika. Nakumbuka kulaumu kuwa moja ya sababu ya Simba kupoteza mchezo ule hii inaweza kuwa ilichangia pakubwa sana.

Utagundua issue siyo kuwa mwenyeji bali kuwa na familiarity na uwanja husika na kuutumia muda mfupi kabla ya mechi ni jambo muhimu kwa wachezaji wa timu zote mbili.

Kwa kulipanua zaidi hili suala na kuongeza uelewa, ndiyo maana mara nyingi utaona Simba huwa inaenda kufanya mazoezi Uwanja wa Mkapa walau siku moja kabla ya mechi za kimataifa na pia huwa inafanya hivyo pia katika uwanja wa KMC kabla ya mechi ya ligi. Hili ni suala la kiufundi zaidi na usipokuwa mtu wa mpira hauwezi kulielewa.

NYONGEZA: Hapa sijaongelea ukweli kuwa kuizuia timu iliyo na haki ya kutumia uwanja siku moja kabla ya mechi ni kuvuruga ratiba yake ya maandalizi ya mechi husika na inaua dhana nzima ya fair play. Ukiizuia timu kama ilivyotokea kwa Simba, itatakiwa kwenda katika mechi bila kuwa imefanya mazoezi kwa masaa 48. Hapo utimamu wa kimwili wa wachezaji utakuwaje?
Yani ushindwe kufanya mazoezi siku moja kabla ya mechi ndo ufungwe, kwamba siku zngn mlikuwa hamfanyi mazoezi.?
 
Yani ushindwe kufanya mazoezi siku moja kabla ya mechi ndo ufungwe, kwamba siku zngn mlikuwa hamfanyi mazoezi.?
Ni wazi masuala mengine yako juu ya upeo wenu wa uelewa
 
Mechi ya Simba na Azam imechezwa siku 12 zilizopita. Wataalamu wangekuwa na akili kisoda kama zako wangesema haki itolewe kwa kwanza kuangalia ni lini mara ya mwisho timu ilitumia uwanja husika. Badala yake kanuni ipo wazi na clear na kanuni lazima ziheshimiwe maana hazijatungwa kujaza tu makaratasi.
Lakin sasa alieizuia simba sio yanga kwanini yanga awe victim ?
 
Kwenye hili bwana, tuseme tu ukweli bila kumung'unya maneno, simba tumeaibisha yaani mazoezi ya dk 30 ndio yafanye tususie mechi? hii mechi kila mtu alijiandaa kuanzia kwa mashabiki mpaka kwa wachezaji iweje sababu ya et kukataliwa kufanya mazoezi siku moja kabla ya mechi iwe nongwa ilihali tulikuwa tumejiandaa?
Kwanini mlikataa wasifanye mazoezi, mlitegemea nini
 
Simba ndo alitumia uwanja wa Taifa dhidi ya Azam week hii, unasema hayupo familiar na uwanja wa Taifa kivipi?

Bodi ya ligi inasema Simba hawakutoa taarifa za mamlaka ya uwanja kuhusu ujio wao.
Walitaka wafanye vip mazoezi usiku bila kuwajulisha wenye mamlaka ili wawake mazingira rafiki ikiwa pamoja na mwanga au walitaka watumie tochi za simu?

Simba waliandaa mangenge Yao ili kutafuta sababu ya kukimbia mechi

Simba wamefanya uhuni hapa laZima kanuni zisimame
taratubu haisemi hivyo ,inasema sikumoja kabla ya game.....
 
Ni wazi masuala mengine yako juu ya upeo wenu wa uelewa
Kwahiyo alieizuia Simba kuzima uwanjani ni Yanga au sio ? Kivipi ? Yanga ndio manager wa uwanja na ndio ana control nani aingie na nani asiingie na kwa muda gani ? Mbona barua Yao haisemi kama Yanga ndio kamzuia huyo Simba kufanya mazoezi?....kama ndio hivyo kwanini yanga awe victim ? How ? Why ?
 
Sasa mkuu kama hamkufanya mazoezi na mkafungwa hiyo game ya uwanja wa jamhuri mbona hamkugomea iyo mechi??
Sema tu jana mliona zile 5 zinarudi mkaacha manyoya..
 
Kwenye hili bwana, tuseme tu ukweli bila kumung'unya maneno, simba tumeaibisha yaani mazoezi ya dk 30 ndio yafanye tususie mechi? hii mechi kila mtu alijiandaa kuanzia kwa mashabiki mpaka kwa wachezaji iweje sababu ya et kukataliwa kufanya mazoezi siku moja kabla ya mechi iwe nongwa ilihali tulikuwa tumejiandaa?
tatizo la nchi yetu kila kitu tunaleta porojo kwani kuna shida gani kuacha kanuni sheria na taratibu zifanye kazi na yule anakiuka taratibu hizo wanahusika wahukumu kwa kufuata kanuni hizo lakini kwetu hatutaki kufuata hata hizo kanunu cio walitungiwa hizo kanunu cio wanaotakiwa kuzisimamia wala cio wale wanaotakiwa kuzitafsiri nchi ya ajabu sana hii NA HAWA WANASEMA HAWATACHEZA TENA MECHI YA MARUDIO NA WALE WANA SEMA HAWATACHEZA MICHEZO ILIYO BANKI MPAKA ALIYEWAAGIZA MAKOMANDOO AJULIKANE NGOJA TUONE WENYE MPIRA WAO WATA SEMAJE. VITUKO VITUKO VITUKO WE NCHI YANGU NO REFORM NO KUCHEZA
 
Sasa mkuu kama hamkufanya mazoezi na mkafungwa hiyo game ya uwanja wa jamhuri mbona hamkugomea iyo mechi??
Sema tu jana mliona zile 5 zinarudi mkaacha manyoya..
Soma tena mada kwa utulivu hadi uielewe kabla haujachangia. Hilo litakusaidia.
 
Badala ya kulalamikia chanzo cha kutofanyika mechi ambacho ni uhuni wa Yanga, unalalamikia Simba. Shenzi kabisa
Kwa nini Yanga walizuia mazoezi kutofanyika?
 
Lakin sasa alieizuia simba sio yanga kwanini yanga awe victim ?

Kwahiyo alieizuia Simba kuzima uwanjani ni Yanga au sio ? Kivipi ? Yanga ndio manager wa uwanja na ndio ana control nani aingie na nani asiingie na kwa muda gani ? Mbona barua Yao haisemi kama Yanga ndio kamzuia huyo Simba kufanya mazoezi?....kama ndio hivyo kwanini yanga awe victim ? How ? Why ?
Mkishavurunda mnatafuta sketi za kujifichia. Juzi mlikana "makolo" siyo Simba, leo hii mnawakana watendaji wenu mnaowatuma kufanya uhuni.
 
Hakuna haki isiyoambatana na wajibu
Haki ya kufanya mazoezi kabla ya mechi walikuwa nayo sawa
Kwanini hawakutimiza wajibu wa kuwapa taarifa kamshina wa mchezo, wamiliki wa uwanja na mwenyeji wa mchezo kuwa timu utafika muda fulani Kwa ajili ya mazoezi ili wawapokee na kuwaandalia mazingira rafiki kwanini walivizia
Kwa hoja hii inamaana wasingezuiwa kuingia na polisi na mabaunsa, wangeingia ila mazoezi yangeshindikana au yangechelewa sababu ya kutokuwepo kwa maandalizi yaliyosababishwa na kutokutoa taarifa.

Uwepo wa walinzi wanaosemekana ni wa Yanga ndo imemaanisha kuwa taarifa ilikuwepo ndo maana kukawekwa ulinzi.
 
Kwahiyo alieizuia Simba kuzima uwanjani ni Yanga au sio ? Kivipi ? Yanga ndio manager wa uwanja na ndio ana control nani aingie na nani asiingie na kwa muda gani ? Mbona barua Yao haisemi kama Yanga ndio kamzuia huyo Simba kufanya mazoezi?....kama ndio hivyo kwanini yanga awe victim ? How ? Why ?
Ukomo wa majukumu wa timu mwenyeji inapokabidhiwa uwanja unakomea wapi?
 
Badala ya kulalamikia chanzo cha kutofanyika mechi ambacho ni uhuni wa Yanga, unalalamikia Simba. Shenzi kabisa
Kwa nini Yanga walizuia mazoezi kutofanyika?
Yanga sio mmiliki wa uwanja
Yanga hatunzi funguo za mageti ya uwanja
Yanga hana wataalam wa taa za uwanjani kumbuka Simba walitaka kufanya mazoezi usiku
Yanga atazuiaje Simba yenye msafara wa police
Yanga alikuwa mwenyeji kiitafaki tu lakini analoweza kuzuia Kwa Simba kufanya mazoezi
Hilo haliwezekani Simba walikimnia mechi
 
Mechi ya Simba na Azam imechezwa siku 12 zilizopita. Wataalamu wangekuwa na akili kisoda kama zako wangesema haki itolewe kwa kwanza kuangalia ni lini mara ya mwisho timu ilitumia uwanja husika. Badala yake kanuni ipo wazi na clear na kanuni lazima ziheshimiwe maana hazijatungwa kujaza tu makaratasi.

Tatizo mnadekezwa saa kumbe mpaka huku kwenye soka la wanawake mnadeka. Tabia za kudeka mmezitoa kwenye soka la wanawake mmezileta kwenye soka la wanaume.
 
Kwa hoja hii inamaana wasingezuiwa kuingia na polisi na mabaunsa, wangeingia ila mazoezi yangeshindikana au yangechelewa sababu ya kutokuwepo kwa maandalizi yaliyosababishwa na kutokutoa taarifa.

Uwepo wa walinzi wanaosemekana ni wa Yanga ndo imemaanisha kuwa taarifa ilikuwepo ndo maana kukawekwa ulinzi.
Toka lini ukaona Yanga ana walinzi?
Kwanini Simba hawakupoga simu hapo Chang'ombe police station waje kuwaondoa hao waharifu na wafanye mazoezi
 
Back
Top Bottom