Simba imewezekanaje kuanza msimu bila kusoma mapato na matumizi kwa wanachama wake?

Simba imewezekanaje kuanza msimu bila kusoma mapato na matumizi kwa wanachama wake?

Mmeambiwa imetumika bilioni 7. Tulieni msisumbue watu
 
Mimi mwenyewe ni muhasibu kwenye jumuiya sijasoma mapato na matumizi maisha yanaendela...ila kikubwa hesabu zipo vzr wakitaka nawapa shida muda unabana..nadhani na Simba ni kama mimi..
😃😃😃😃😃😃
Jumuiya ya mtakatifu nani?
 
Timu inajiendea tu; wanaona mashabiki hawana maana ya kusomewa taarifa.
Kuna tatizo kubwa sana hapo Simba ni vile tu wanachama wenyewe ni wapiga kelele, hivi timu ya wanachama inawezaje kumaliza msimu wa kimashindano ika anza mwingine bila mkutano mkuu hata ndondo hatufanyi hivyo
 
Kuna tatizo kubwa sana hapo Simba ni vile tu wanachama wenyewe ni wapiga kelele, hivi timu ya wanachama inawezaje kumaliza msimu wa kimashindano ika anza mwingine bila mkutano mkuu hata ndondo hatufanyi hivyo
Inamaanisha Hakuna wanachama hapo bali kuna mashabiki kwa maana mwanachama ana haki kikatiba ya kuhoji mapato na matumizi na mambo mengine yaliyomo,(yaliyo ainishwa), kwenye katiba yanayo kuhusu, mimi sina haki ya kuhoji kwasababu siyo mwanachama ila huwa napenda mawazo fikirishi
 
Mangunga pia anategemea nguvu ya wanachama kama haipo waache kulalamika kwenye blanketi na mashuka
Kuna mfumo flani wa uchawa umekopiwa kutoka kwenye vyama vya siasa umeingizwa kwenye mpira wale wanachama maarufu kwenye online TV wanapewa fungu kazi yao ni kusifia tu hata ujinga
 
Hii kitu imenipa maswali kadhaa kichwani je club yetu bado ni ya wanachama au ishakua ya mtu binafsi?

imewezekanaje msimu wa 23/24 umeisha na mwingine huu wa 24/25 ume anza bila kua na mkutano mkuu wala kusomewa budget ya mapato na matumizi?

Ina maana timu yetu inajiendea tu kama timu ya ndondo au ni nini hasa kinafichwa?mwaka jana walitusomea bajeti na mafanikio ya WhatsApp channel japo ya uongo na kweli lakini afadhari walitimiza wajibu , hii club ina shida sehemu ndio maana Mzee Rage alituita jina la ajabu na Kaduguda akakazia
Unatupigia kelele tu, timu ni ya Mudi ns Dada zake!
 
Baada ya kusomewa mapato na matumizi huko Yanga familia yako imeambulia shilingi ngapi
 
Back
Top Bottom