Ni kweli kwamba kapuku hana thamani, lakini wakati mwingine umasikini tunajitakia tu , kwa umati wa wanachama na wapenzi wa simba nchi nzima timu hii haistahili kuitwa masikini, kama tutapata oganaiza mzuri mwenye ujuzi na mfia Simba, basi timu hii itaweza kujikimu na hivyo kuondokana na dhiki inayolazimika timu yetu kutumika hata kwenye mambo yasiyostahili kwa vile tu anayeitwa mwenye Simba yake anatumika.
Simba si timu ya kucheza bure , ambapo pamoja na kutangaza bure bado ikakosa watazamaji, hili ililofanyiwa timu ya simba ni aibu inayotufanya sisi wanasimba wengine tuinamishe vichwa chini kwa aibu, mara kadhaa nimejipambanua humu kupinga magumashi kwenye uendeshaji wa timu lakini nimeishia kubezwa na kutukanwa, bali sasa uvumilivu umefika kikomo, Simba irudishwe kwa wenyewe.