Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hakika..Simba abaki
mzamiru
Kibu denisi
Kapombe
Zimbwe
Mwenda
Chama abaki ila awe anatokea sub
Inonga
Waliobaki wapumzike
Yanga huyu aliyekandwa na simba goli mbili? au yanga aliyetoka hatua za awali CL?Fanyeni transformation....Ili mfanye usajili mkubwa kama yanga
Watumien sana Yanga as role model wenu
Hakika mtafanikiwa
Kuna mtu juzi juzi aliandika humu Simba walimalizana naye walipoenda Mbeya kucheza na Ihefu.Yahaya mbegu ameshasaini azam miaka 3
Halafu yule zao la Simba, kama walionyesha nia ya kumtaka naamini ataipa kipaumbele zaidi. Ila nasisitiza Simba wazingatie vimo vya wachezaji kama wanataka waende levo za juu zaidi kimafanikio.Muda utaongea mno
Bandiko zuri.Jana nchi ya Morocco ilipata watalii millioni 89. Hatujui uraia wao, hatujui tabia zao, hatujui wameoa au kuolewa, ila tunafahamu jambo moja tu kuhusu watalii hawa, wanapenda soka na jana mechi ya Simba na Wydad ilikuwa mbuga waliyoitembelea.
Usishangae, mech ya jana imetazamwa na watu million 89 duniani kote na hii sio kawaida kwa timu za Afrika mashariki.
SIMBA inajitafuta ndani ya soka la Afrika? Jibu ni hapana tayari imejipata japo haina kombe lolote kama kielelezo cha ukubwa wake ndani ya afrika.
Lakini pamoja na kutochukua kombe lolote kubwa ndani ya Mashindano ya Klabu Bingwa au shirikisho bado hakuna timu Afrika ambayo ikipangiwa Simba italala raha mstarehe, lazima kila mtu afanye homework yake vizuri la sivyo anaweza kutana na lolote linalopatikana ndani ya dakika 90.
Wapi ilipo Simba, inataka kwenda wapi na nani ataambatana nayo (wachezaji), hili linabakia kuwa swali muhimu mnoo kwa wana Msimbazi.
Kuna kauli moja maarufu huwa inatolewa misibani hasa wakati wa kuzika kwamba tulikupenda ila mungu amekupenda zaidi.Kauli hii inawahusu saana baadhi ya wachezaji wa simba.
Kama simba inajiona nusu fainali au fainali kabisa ya Klabu Bingwa Afrika basi kuna wachezaji wakuagana nao. Sio kwamba ni wabaya au hawafai ila kwenye basi la Simba la Nusu Fainali au Fainali Klabu Bingwa hawa hawana siti au nafasi hata ya kusimama tu ndani ya gari. Kifupi hawatakiwi.
Waitwe waambiwe ukweli na waagwe kwa heshima, kama wanaipenda klabu na kama mikataba yao inaelekea mwisho basi waachwe wakatafute malisho kwingine muda wao umeisha. We unaonaje is it a road to hell or road to glory?
Nani aachwe na nani abaki nadhani mechi ya jana imetupa majibu mazuri kabisa. Nini maoni yako juu ya Simba ijayo na safari yao?
Karibu.