Simba kubadili logo yao, kipi ungependa kiongezwe?

mikedean

JF-Expert Member
Joined
Mar 15, 2018
Posts
3,267
Reaction score
4,634
Klabu ya Simba ipo njiani kuifanyia marekebisho nembo yao ili iwe ya kisasa na iendane na wakati.Inasemekana kuwa wapenzi wa Simba hawataki kumwona Simba aliyekonda katika nembo hiyo, hivyo wanahitaji kuweka kichwa tu cha Simba dume.

Wewe kama mwanachama na mpenzi wa klabu ya Simba unakaribishwa kutoa maoni kuhusu maboresho hayo yaani nini kiondoke, kiongezwe au ibaki kama ilivyo sasa.

Simba Nguvu moja.

NB: Nembo au logo haibadilishwi ila unaweza kuimodify kwa kupunguza au kuongeza baadhi ya vitu ikiwepo rangi.

WAPE SALAAAAAAM!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu acha kutia chumvi,nani kasema logo ya simba ina simba aliyekonda na wanataka kichwa tu au umekimbia na comment moja kwenye comments za mashabiki kule Instagram, simba bado wanachukua maoni hakuna waliolalamika logo ina simba aliyekonda, ukiamua kutoa taarifa ilete ilivyo siyo unaongeza chumvi zako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uko sahihi comment nimechukua kule lakin mi pia japo mwana Yanga naona huenda ikawa na mashiko.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hayo hliyosema ni mazuri ila bado kuiweka ndani ya umbo fulani ni vema.kuliko kuiachaikiwa inahang
Waambie watoe hilo duara, halafu waongeze simba jike na cub yaani wawe simba dume na jike na cub waweke na kaswala kwa image ya Mpira kakiwa chini kanaliwa na hao simba. Tutarepresent timu ya wanaume, wanawake na vijana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakubaliana na kubadilisha au kurekebisha logo.

Kwanza Simba anayeonekana anapaswa kuonekana kichwa tu.
Na kama italazimika abaki hivyo basi achorwe kwa rangi nyeusi na miguu iwe imejaa msuli(minene)

Pili katika hiyo duara inabidi kuwe na mistari miwili ina iliyo bold miekundu na kati kati rangi nyeupe ambayo itakuwa kama kimstari chembamba kuliko hiyo miekundu.Hii ni kuipa boundary inapochorwa popote tofauti na sasa ikichorwa kwenye white plane haionekani uduara wake badala yake inakuwa kama mtu aliyekuwa anajifunza kuchora Simba.

Mengine watasema wengine

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…