Ndanda ndiyo anadai point sio Yanga. Lakini nyie eti mnadai point za mechi alizocheza Kessy. Wakati huo huo million 50 mnazitaka.Vipi mmeshapewa pointi 3?Mliambiwa hamna kanuni hiyo hamsikii. Mmeanza kupiga wachezaji sasa?
Yanga wamepanic tu sana baada ya droo!Wanajaribu kuroga mchana kweupee lakini wapi?Wao wanasahau zile point 24 za kumchezesha kessy kinyume na kanuni za tffHebu tutajie kanuni iliyovunjwa ya TFF. TFF wanatoaje leseni bila work permit ikiwa kanuni ni hiyo mnayodai?Ukishatoa leseni ni kwamba mchezaji anaruhusiwa kucheza. Sheria za kusimamia mpira zinaongozwa na kanuni sio matamko.
Mkuu, kama TFF wameweka hiyo kanuni ni sawa lkn usishangae ukikuta hiyo kanuni haipo maana hilo linahusika moja kwa moja na sheria za nchi.
Pia kumbuka kuwa soka ina taratibu zake ambazo sio lazima ziwe chini ya sheria za nchi.
Vv
Ahsante mtu mzima, mwenye akili za kiutu uzima. Utu usimamizi wa kujua kwamba pingamizi na rufaa ni vitu tofauti ambavyo vyote vinaonesha kukubaliana na matokeo, unayeelewa kwamba Kessy hakuwa na leseni ya CAF ila Waghana wa Simba walikuwa na leseni ya TFF, unayeelewa kwamba mchezaji kutoka Simba si sahihi wala halali kuhamia timu nyengine ila wa timu nyengine ni sahihi na halali, unayeelewa kwamba uhalali wa mchezaji aliyeko Simba ni kutokuwa na mkataba na timu nyengine tu hata kama hajakamilisha taratibu zote nyengine za nchi hii. Shkamoo mtu mzima!Acha kutumia akili ya mtoto mchanga kuandika.
Ishu ya kesi ni tofauti na hii!
Kesi amesajili yanga akiwa na mkataba na Simba, na amepewa leseni akiwa si mchezaji halali.
Agyei na kotei ni wachezaji halali wa Simba ila hawakuwa na vibali vya kazi.
Ndanda hawajaweka pingamizi la usajili kwa Simba.
Uwe unasukutua ubongo wako kabla ya kuchangia. Huo ni ushabiki mwiba!