Simba kuweni makini na AS Vita

pamba boy

Senior Member
Joined
Jun 26, 2013
Posts
181
Reaction score
266
Leo nimepita mitandaoni na kukuta kuna taarifa inasambazwa kuwa mchezaji mahiri wa as vita alieisumbua ngome ya simba Djuma hatakuwepo kutokana na kupata majeraha yatakayomweka nje kwa miezi 6.

Ndugu wana simba wenzangu hii ni mbinu ya as vita, huyo mchezaji atakuwepo na atacheza mchezo huo, simba inabidi wawaandae wachezaji wao mbinu za kumzuia asilete madhara langoni mwao kama ilivyokuwa mechi ya awali kule Congo DR
 
Mbinu zao zimechelewa na za kizamani kikosi Cha Simba lipo imara kukabiliana na team yoyote Africa muda wowote..
 
Mbinu zao zimechelewa na za kizamani kikosi Cha Simba lipo imara kukabiliana na team yoyote Africa muda wowote..
Ni kweli ila tahadhari ni muhimu sana, as vita ni wazoefu wa michuano hii kuliko simba.
 
Djuma Shabani amepata injury na hatakuwepo, wakala wake amethibitisha hatakuwepo kwa muda mrefu, hayupo katika msafara wa Vita kuja Tanzania na hajaombewa viza ubalozi wa Tanzania nchini Congo kuja TZ, haji.
 
Kwani mechi ya kwanza hakuwepo na kama alikuwepo matokeo yalikuwaje? Awepo asiwepo Simba wamejiandaa vizuri kuwakabili sisi sio kama utopolo walioshangilia wakafikiri Kapombe hatacheza baada ya kumwona wakataka kukata rufaa ila kwa busara za wachache wakatulia
 
Djuma Shabani amepata injury na hatakuwepo, wakala wake amethibitisha hatakuwepo kwa muda mrefu, hayupo katika msafara wa Vita kuja Tanzania na hajaombewa viza ubalozi wa Tanzania nchini Congo kuja TZ, haji.
Djuma shaban amewasili leo na timu ya as vita na TBC wamethibitisha, hivyo simba tuwe makini na mpango wa as vita
 
Djuma Shabani amepata injury na hatakuwepo, wakala wake amethibitisha hatakuwepo kwa muda mrefu, hayupo katika msafara wa Vita kuja Tanzania na hajaombewa viza ubalozi wa Tanzania nchini Congo kuja TZ, haji.
Huyo wakala ni muhuni, Djuma amemaliza mechi na Gambia dakika 90, hizo injury amezipata lini? Aliyeumia ni Luzolo Sita, beki wa kushoto wa DRC na Vita
 
Hata kama akiwepo uwanjani bado Simba wana nafasi kubwa ya kushinda hiyo mechi, mbona walipigwa kwao huyo Djuma akiwepo.
 
Mpira wa sasa unachezwa ndani ya uwanja tusubiri hiyo kesho Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Simba kila la heri wazingatie ushauri wa kocha ili kupata matokeo mazuri.
 
Hata aje Bayern au Barcelona sembuse hao AS Vita. Watoto wadogo sana Simba ikiwa kwa Mkapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…