Simba kwenda kote uturuki mnacheza na madereva taksi, mmepoteza pesa na muda kijinga

craq

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2017
Posts
859
Reaction score
1,866
Yaani simba wamepoteza pesa kwenda uturuki wameishia kufanya mazoezi Gym kwa kuwa uturuki kulikuwa na mvua kubwa sana na wakabahatika kucheza mechi na timu ya umoja wa madereva taksi wenye asili ya palestina

Kama Gym hivi simba sc hawana Gym kweli si wanayo sasa kupoteza pesa kote ndio mnaenda gym na kucheza na madereva taksi ?

Bora hata mngecheza na vilabu vikubwa kidogo tungewaelewa

 
Mwandishi wa hilo gazeti aliandika kwa uchungu kweli! Atulie anywe maji kwanza
 
Hii habari imeandikwa na gazeti la watu wa yanga, linaitwa Jangwani. Toleo la jumatatu ya August 6/2018, nililiona kwa abiria niliyekaa nae siti ya jirani aliyekuwa akilisoma. Ila ni katika hali ya kujifariji tu na njaa iliyopo vyurani. Lakini kila wakiamka afadhali ya jana! Mtazidi kupata tabu sana. Lazma mnyooke.
 
Kwani unaposikia timu ya wakata miwa unaelewa nini kibongobongo?

Kwani io timu ni wakata miwa kweli?


Au watoto wa jangwani ni watoto kweli?

Mashetani wekundu ni mashetani
 
hata mwanaspoti waliandika hii
 
Watu wameweka kambi morogoro wanakula magimbi na kunywa maji ya mito lazima kiwaume, endeleeni kukaa vibarazani na kopo la maji mmepanga foleni kwenda chooni
Hahahahah dah utani bwana raha sana
 
Hata Stand United ukiiita Wapiga Debe hujakosea, hata Azam ukiiita Wauza Ice Cream hujakosea, Hata Alliance ukiwaita Watoto wa Sekondar hujakosea, Hata Biashara United ukiiita Wauza Mayai wa Kitunda/Wamachinga ni sahihi tu soo hata hao Waturuki wakiitwa dereva Bajaj ni poa tu
 
Hivi hizo sandals za plastiki nazo ni jezi ya simba??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…