Nebuchadneza
JF-Expert Member
- Oct 6, 2023
- 435
- 1,093
Salamu hazina maana tunazeeshana bure.
Ukiangalia mechi ya kwanza hapa kwa Mkapa wenyewe mtayaamini maneno yangu, Simba walikuwa vizuri sana, Waarabu wapo hovyo, upangaji wa kikosi wa Robertinho umewafelisha Simba kushinda nyumbani.
Unaanza na Luis Miquissone wa kazi gani na kumuacha Baleke na Phiri kwenye benchi? Kocha anawafelisha sana Simba.
Waarabu wabovu wanaacha magepu sana, wangepatikana wachezaji wawili kama Kibu nakuhakikishia Simba wangeshinda hapa kwa Mkapa.
Saido anachoka mapema, Chama naye ndio umri unamtupa mkono, najiuliza wamemsajilije Onana, huyu ndio yule walikuwa wanamsifu Onana somba somba, yaani akipewa mipira anapiga chenga chenga, bado anampira wa kitoto wakucheza na jukwaa.
Mechi ya pili Simba wamefeli tena kumalizia mchezo, Waarabu walishakubali kufa dakika ya 70 umepata goli, mnashindwa kuwatoa mchezoni kwa kujiangusha angusha, mbona hao wanafanyaga hivyo?
Unaongoza goli moja bado unashindana na Waarabu kweli kocha anazingua! Ndo ilikuwa muda wa kuwatoa mchezoni kwa kufanya vitendo vya kuwakera.
Unamuingiza Kennedy wanini wakati unaongoza goli moja? Ni Bora ungemuingiza Mzamiru afunge kiungo kati, maana Ngoma alishazidiwa, Kanoute alifichwa, unamuingiza Onana badala ya kumuingiza Israeli Mwenda! Mpaka hapo unaona madhaifu ya benchi la ufundi, nawahakikishia Robertinho mwezi wa 2 hafiki lazima atimuliwe tu.
Angalizo: Kila anayemtoa Simba Robo Fainali anafika Finali, Simba jiangalieni hapo.
Mimi Yanga ila nimetoa yangu ya moyoni, nakaribisha mapovu.
Ukiangalia mechi ya kwanza hapa kwa Mkapa wenyewe mtayaamini maneno yangu, Simba walikuwa vizuri sana, Waarabu wapo hovyo, upangaji wa kikosi wa Robertinho umewafelisha Simba kushinda nyumbani.
Unaanza na Luis Miquissone wa kazi gani na kumuacha Baleke na Phiri kwenye benchi? Kocha anawafelisha sana Simba.
Waarabu wabovu wanaacha magepu sana, wangepatikana wachezaji wawili kama Kibu nakuhakikishia Simba wangeshinda hapa kwa Mkapa.
Saido anachoka mapema, Chama naye ndio umri unamtupa mkono, najiuliza wamemsajilije Onana, huyu ndio yule walikuwa wanamsifu Onana somba somba, yaani akipewa mipira anapiga chenga chenga, bado anampira wa kitoto wakucheza na jukwaa.
Mechi ya pili Simba wamefeli tena kumalizia mchezo, Waarabu walishakubali kufa dakika ya 70 umepata goli, mnashindwa kuwatoa mchezoni kwa kujiangusha angusha, mbona hao wanafanyaga hivyo?
Unaongoza goli moja bado unashindana na Waarabu kweli kocha anazingua! Ndo ilikuwa muda wa kuwatoa mchezoni kwa kufanya vitendo vya kuwakera.
Unamuingiza Kennedy wanini wakati unaongoza goli moja? Ni Bora ungemuingiza Mzamiru afunge kiungo kati, maana Ngoma alishazidiwa, Kanoute alifichwa, unamuingiza Onana badala ya kumuingiza Israeli Mwenda! Mpaka hapo unaona madhaifu ya benchi la ufundi, nawahakikishia Robertinho mwezi wa 2 hafiki lazima atimuliwe tu.
Angalizo: Kila anayemtoa Simba Robo Fainali anafika Finali, Simba jiangalieni hapo.
Mimi Yanga ila nimetoa yangu ya moyoni, nakaribisha mapovu.