Mmakua Mmakonde
Member
- Aug 23, 2016
- 61
- 144
Klabu ya Simba imejiridhisha na kupeleka ushahidi kwenye kamati ya sheria na hadhi za wachezaji kuhusu sakata la usajili linalomhusu beki wa kulia wa Yanga Hassan Kessy Ramadhani na wanaamini endapo haki itasimamiwa vilivyo basi watashinda kesi hiyo.
“Yanga walituandikia barua, TFF wakiomba kupewa leseni ya mchezaji Kessy kabla ya June 15 ambapo ndio ulikuwa mwisho wa mkataba wake, tena walikuwa wanamuombea leseni ya CAF lakini kimantiki huwezi kupewa laseni ya CAF bila kuwa na leseni ya ndani”, amesema Haji Manara afisa habari wa Simba wakati akizungumza na waandishi wa habari.
“Kwahiyo kimsingi, Kessy alivunja mkataba, Yanga walimchezesha mchezaji ambaye aliwekewa pingamizi.”
Wakati huohuo klabu ya Simba imepanga kumpeleka Kessy mahakamani wakimtuhumu kuwatuhumu baadhi ya viongozi wa Simba kutaka kumpa rushwa wakati akiwa Mtibwa Sugar.
“Hatutaki kuombwa radhi kwasababu katutuhumu kila mtu kasikia nchi nzima, lazima akathibitishw mahakamani. Lakini akanithibitishie mimi niliwahi kumwambia yeye atachoma banda”, alimalizia Manara.
SOURCE; ShaffihDauda | Sports News and Scores
Hawa Simba na Yanga ni tatizo ktk kuendeleza vipaji vya vijana wetu nchini. Sasa kwa suala kama hili la Kessy Simba wana haja gani ya kumsumbua huyu kijana wakati ni wao wenyewe ndio walioanza kumdhalilisha na kuonyesha kutumuhitaji na kutomuamini?. Wanadai wanataka kumshitaki kwa kosa alilowafanyia akiwa Mtibwa hii kama sio Nongwa ni nini maana kama kumshitaki ilitakiwa muwe mumemshitaki akiwa Simba maana baada ya kutoka huko alikowafania kosa mkawanae. Mnawaharibia maisha vijana wetu hawa vijana hii ndio ajira yao na wanaendesha maisha kwenye mpira sasa kuwabudhi ni kuwawekea njia mbaya ktk maisha yao ya soka. Wakifanikiwa kwenda kucheza nje mnaanza kupiga kelele kuwa alipita kwetu na sifa kibao wakati mnaonyesha kabisa hamuwatakii mema. Na nyie wachezaji ebu mpate ushauri wa kitaalamu kabla hamjafanya maamuzi ya kuwa na hizi timu na msirubuniwe na pesa za muda mfupi wakati kiundani hawana nia njema nanyi.
“Yanga walituandikia barua, TFF wakiomba kupewa leseni ya mchezaji Kessy kabla ya June 15 ambapo ndio ulikuwa mwisho wa mkataba wake, tena walikuwa wanamuombea leseni ya CAF lakini kimantiki huwezi kupewa laseni ya CAF bila kuwa na leseni ya ndani”, amesema Haji Manara afisa habari wa Simba wakati akizungumza na waandishi wa habari.
“Kwahiyo kimsingi, Kessy alivunja mkataba, Yanga walimchezesha mchezaji ambaye aliwekewa pingamizi.”
Wakati huohuo klabu ya Simba imepanga kumpeleka Kessy mahakamani wakimtuhumu kuwatuhumu baadhi ya viongozi wa Simba kutaka kumpa rushwa wakati akiwa Mtibwa Sugar.
“Hatutaki kuombwa radhi kwasababu katutuhumu kila mtu kasikia nchi nzima, lazima akathibitishw mahakamani. Lakini akanithibitishie mimi niliwahi kumwambia yeye atachoma banda”, alimalizia Manara.
SOURCE; ShaffihDauda | Sports News and Scores
Hawa Simba na Yanga ni tatizo ktk kuendeleza vipaji vya vijana wetu nchini. Sasa kwa suala kama hili la Kessy Simba wana haja gani ya kumsumbua huyu kijana wakati ni wao wenyewe ndio walioanza kumdhalilisha na kuonyesha kutumuhitaji na kutomuamini?. Wanadai wanataka kumshitaki kwa kosa alilowafanyia akiwa Mtibwa hii kama sio Nongwa ni nini maana kama kumshitaki ilitakiwa muwe mumemshitaki akiwa Simba maana baada ya kutoka huko alikowafania kosa mkawanae. Mnawaharibia maisha vijana wetu hawa vijana hii ndio ajira yao na wanaendesha maisha kwenye mpira sasa kuwabudhi ni kuwawekea njia mbaya ktk maisha yao ya soka. Wakifanikiwa kwenda kucheza nje mnaanza kupiga kelele kuwa alipita kwetu na sifa kibao wakati mnaonyesha kabisa hamuwatakii mema. Na nyie wachezaji ebu mpate ushauri wa kitaalamu kabla hamjafanya maamuzi ya kuwa na hizi timu na msirubuniwe na pesa za muda mfupi wakati kiundani hawana nia njema nanyi.