Simba na Yanga ni dhahabu mchangani

Simba na Yanga ni dhahabu mchangani

babacollins

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2010
Posts
901
Reaction score
212
Pamoja na kubezwa mara kwa mara, kupondwa na wakati mwingine baadhi ya watu kutoa wito wa vilabu hivi vikongwe vitoweshwe kwenye ulimwengu wa soka kwa kudaiwa kwamba vinadidimiza mchezo wa soka, ni ukweli usiopingika vilabu hivi viwili ni dhahabu mchangani kwa maendeleo ya soka na nchi kwa ujumla.

Mpaka sasa vimewavuta maelfu ya watu kujiingiza kwenye soka, vimeongeza umaarufu wa vyombo vingi vya habari na wanahabari wenyewe, vimeingiza mabilioni ya pesa kupitia viingilio vya getini na wadhamini, maelfu ya vijana wamepitia katika vilabu hivi kama wachezaji na baadhi yao kuboresha maisha yao na wakati mwingine vimetumika hata kuleta utulivu na amani. Huu ni baadhi tu ya utajiri kwenye vilabu hivi.

Kifupi Simba na Yanga ni vilabu kiongozi kwenye soka la Tanzania. Viongozi wanaojiingiza katika vilabu hivi wana nafasi kubwa ya kuendeleza vilabu hivi na kuacha " legacy" ya "watu" na "vitu" kwenye vilabu hivi na kuendelea kuvuna utajiri tele uliopo kwenye hivi vilabu, jambo ambalo litaendelea kuvuta wengi kwenye soka na hata wengi kuingiza fedha zao na kuwekeza kwenye umiliki wa vilabu na kuwa na sekta bora ya michezo kupitia soka.

Mchezaji kiongozi.
 
Mimi sikubaliani nawe mkuu,Simba na yanga vilabu hivi vimesababisha soka letu kama taifa listened popote, ushindani wetu ni wa ndani tu,vilabu hivi vimekua a big elephants in the room na kila mmoja wetu tunaogopa kuwaeleza ukweli, pls MO nunua Simba iwe ya kwako na iendeshe kibiashara na GSM nunua yanga iwe yako nao ufanye kama Mamelodi sundown ya pale SA.
 
Pamoja na kubezwa mara kwa mara, kupondwa na wakati mwingine baadhi ya watu kutoa wito wa vilabu hivi vikongwe vitoweshwe kwenye ulimwengu wa soka kwa kudaiwa kwamba vinadidimiza mchezo wa soka...
Una upeo wa mbali sana Babacollins ila kwa mtu wa kawaida kukuelewa .Inataka elimu kubwa kukuelewa badala ya kubisha tu bila kusikiliza na kujifunza kile unachokisema
 
dhahabu ni hiyo tim ya wananchi Yanga, hilo li tim linguine la wachawi na ulozi ulozi yaani makolo haliwezi kuwa hata silver au Shaba
 
Hizi timu ndo muhimili wa SOKA la Tanzania,watu wamenufaika kiuchumi,kisiasa na kadhalika.Bila hizi timu hakuna mpira Tanzania.Kuuzwa jumla haiwezekani,zinauzwa asilimia 49 tu na 51 zinabaki kwa wanachama.

Anayetaka kumiliki timu hajazuiliwa,aanzishe yake kama Bakhresa.
 
Back
Top Bottom